Friday, January 29, 2010

Mkutano mkuu wa KPC ni Februari 12,2010 !

Wanachama wote wa Kagera Press Club mnatangaziwa kuwa mkutano mkuu wa mwaka uliokuwa ufanyike novemba 2009 sasa utafanyika februari 12,2010 kwenye ofisi za KPC.

Maelezo zaidi yatawekwa kwenye blog hii,kutumiwa barua na kupigiwa simu.

kwa waliooko bukoba mjini mnaweza kusoma tangazo la mkutano huo kwenye ubao wa matangazo wa KPC.

Imetolewa na
G.Makwabe
Mwenyekiti KPC

Wednesday, January 27, 2010

Ukweli kuhusu 'Mzungu' anayecharaza wananchi viboko Kagera !

Baadhi ya waandishi wakifanya mahojiano na wakazi wa kijiji cha Ijumbi wanaoishi kwa mashka.





Licha ya kucheka lakini wanacharazwa bakora,wengine ni wazee sana


Taarifa za kuwepo raia mmoja wa kigeni anayenyanyasa wananchi zimekuwa zikiripotiwa na vyombo kadhaa vya habari lakini kagera press club iliwatuma waandishi 7 wa vyombo kadhaa kuchunguza chanzo cha mgogoro huo.


kilichobainika ni hiki hapa.


Na Mwandishi wa Blogspot

KATIKA hali isiyo ya kawaida wananchi wapatao 100 wa kitongoji cha Bujenjeke kijiji cha Ruhija kata ya Ijumbi wamekuwa waakilazimika kuhamisha makazi yao porini kukwepa kipigo kutoka wanamgambo wakishirikiana na askari polisi wanaodaiwa kununuliwa na raia wa kigeni.

JESHI la polisi mkoani Kagera limejikuta likiwa katika lindi la mgogo mkubwa kwa kile kinachodaiwa kuwa kumkingia kifua raia wa kigeni anayedaiwa kuwanyanayasa wananchi na kuwalazimu kukimbia nyumba zao na kulala vichakani zaidi ya mwezi mmoja sasa.

Hayo yamebainika jana baada ya kundi la waandishi wa habari wa mkoani Kagera kulazimika kufanya ziara ya siku moja ya kwenda kuchunguza malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wananchi ya kudai kunyanyaswa na Mzungu ambaye ni anadaiwa kuwa ni raia wa nchini Uingereza.

Wakizungumza na waandishi wa habari wakazi wa kijijini hapo, walidai kuwa kwa kipindi kirefu wamekuwa wakilala na kushinda porini, kukwepa kupigwa na askari polisi wanaodaiwa kuwa katika ofisi ya Kamanda wa polisi Mkoani Kagera na wanamgambo wanaokodishwa kutoka maeneo yaasiojulikana kutokana na mavazi wanayovaa aina ya kininja.

Katika uchunguzi uliofanywa na kundi hilo la wandishi wa habari kutoka chama cha waandishi mkoa wa Kagera(Kagera Press Club) uliweza kubaini kutokuwepo kwa dhana ya utekelezaji wa kilimo kwanza kutokana na kutokuwepo hata shamba jipya linaloonesha kulimwa hivi karibuni zaidi ya zamani kukanda, huku wananchi wakidai kuwa wanashindwa kujishughulisha na kazi za kilimo kutokana na vitisho, vipigo na kuswekwa rumande kwa kubambikiziwa kesi.

Mmoja wa wakazi hao aliyejitambulisha kwa jina la Bahabti Mussa (32) alisema chanzo cha migogoro hiyo ni baaada ya mzungu huyo raia wa Uoingereza, Robert Maintland kwenda kijijini hapo, mwaka 2003 ambapo alifika na kuweka kuanza kuweka vigingi bila kuishirikisha jamii iliokuwa ikiishi hapo, na baadaye kuondoka na kurudi Uingereza.

Alisema mwaka 2008 Maintland alirejea tena nchini na baada ya siku tano kupita badhi ya wananchi walienda kumsalimia kama jirani yao, ambapo katika hali isiyo ya kawaida aliwataka waondoke katika eneo hilo.

Hata hivyo, Musa alisema kuwa walilazimika kumhoji wakiondoka wakiondoka atawalipa, ambapo aliwajibu kuwa angewalipa kuanzia sh. 100,000 hadi 350,000 na kumwambia Mussa kuwa kwa kuwa yeye ni msemaji sana angweweza kumlipa sh. 500,000 kitu ambacho wanchi hao hawakuweza kuafikiana naye, ambapo aliwaambia kuwa asiyeafikiana naye atakipata cha 'moto'.

Naye Elenestina Eleneus (74) alisema yeye kutokana na kutokuwa na nguvu anapata shida kwa kipindi kwa vurugu na vitisho vinavyofanywa askari hivyo amekuwa akishinda vichakani ili kunusuru uhai wake.

Alisema tangu uhai wake hajawahi kushuhudia hali hiyo hapa nchini hasa katika kitongoji hicho.
Alisema kwa sasa hata vifaa vyajke vya kupikia vimsombwa na askari hao na kwenda navyo kusikojulikana na hivyo kulazimika kulia kwenye majani ya migomba.

Jenipha Romwad (29) alidai Novemba 2, 2008 saa 2 asubuhi alipata kipigo kikali kutoka kwa askari akiongozwa na mwanagambo mmoja aliyemtambua kwa jina moja la James huku mzungu akivurumisha risasi kadhaa hewani ya kuwatishia ulifanya mimba yake miezi minane kutoka na kufariki, pamoja na maumivu hayo alisondekwa rumande siku mbili katika kituo cha Muleba kwa madai kuwa ni wavamizi wa ardhi ya Mzungu.

"Nikiwa na mtoto wa mwingine, nilipigwa teke la kiunoni na tumboni na huyo askari hadi kusababisha mimba yangu ya miezi minane kutoka, cha kushanga pamoja na ugonjwa wangu wala polisi pale Muleba hawakunijali hata kunipa huduma na hata sijui kichanga alikozikwa wala hata jinsi yake"alisema.

Mzee Kasenene (80) anayedaiwa kuwa alikuwa mpishi wa mmiliki wa shamba hilo aliyejulikana kwa jina la Peter Pantelakis alisema kwamba wamekuwa wakiishi kwa matesho makubwa kutoka na uwepo wa raia huyo wa kigeni.

Kwa upande wa Mzungu Robert Maintland ambaye hakuwepo katika eneo hilo akizungumza na waandishi wa habari kwa njia ya simu, alisema kuwa ardhi yake na hakuna hata raia wa Tanzania anayeishi pale kwani wote ni Warundi waliokuwa vibarua wa babu yake.

"Hakuna hata mtu wa Mtanzania nayeishi katika eneo lile, wote ni Warundi, ambao wanatabia mbaya za kubaka kuua,wakata miti ovyo"alisema.

Hata hivyo, Maintlanda alidai watu hao wanatumwa na Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini Wilson Masuilingi kuendeela kusihi karika ardhi yake ili aendelee kupata wapiga kura wengi.

Kuhusu kuwavamia na kuwapiga wananchi kulazimika kuhama makazi yao kwa kushirikiana na askari na wanamgambo anaowakodi kutoka katika maeneo yasojulikana, alikataa na kusema kuwa yeye hajui na wala hajui kufanya hivyo na kwamba hayo ni majungu anayopikiwa juu yake ya kumpaka matope.

Halikadhalika kuhusu kuwazuia wananchi kuchukua aina yoyote ya mazao kutoka kwenye msitu unaowanguka, mazao kuvuna mazao waliolima na hata kulima na kutumia maji ya Kurumiyo yalioko katika kitongoji hicho kwa matumizi ya nyumbani alidai kuwa hakuwahi na kwamba yote hayajui.

Mbunge wa Jimbo la Kusini, Masilingi akuzunguzia sakata hilo, alikiri kupokea taarifa za malalamiko ya manyanyaso waofanyiwa wananchi hao na huyo raia wa Kigeni na kufanya mikutano wa hadhara katika kitongoji hicho akiwa na Mkuu wa wilaya ya Muleba, Angelina Mabula ambapo waliagiza raia huyo wa kigeni akamatwe na kuchukuliwa hatua, lakini anashangaa hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kwake.

Alisema wananchi walitakiwa kubaki katika kitongoji chao na kuendelea na shughuli zao kama wananchi wa kawaida.

Alisema katika suala nzima ya Kitingoji hicho kutaka taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa kuingilia kati na kuchunguza mgogoro wake ambao umegubikwa na harufu za rushwa.

Alisema mzungu huyo anataka kumiliki kitongoji kizima wakazi wakazi hao waliwepo katika eneo hilo miaka mingi, na kwamba katika eneo hilo kuna mgogo wa wanafamilia baina ya mzungu na ndugu zake, mgogoro ambao wananchi hawahusiki kabisa.

Kuhusu ujenzi wa vigingi alisema kuwa unatokana na maafisa wa ardhi kula rushwa, kwani ujenzi huo haujahusisha wakazi wa eneo lile, kwa nini ijengwe vigingi wakati serikali.

Naye Kamanda wa polisi Mkoa Kagera Bw Henery salewi alipotakiwa na waandfishi wa habari kuelezea juu ya mgogoro huo unaodaiwa kuwa polisi wake ndiyo wamekuwa wakitumiwa na mzungu huyo kwenda katika kitongoji kuwatishia wananchi na kuwapora mali zao huku wenginew akiwapiga hadi kuharibiwa kwa mimba zao , alikataa kuonana hata kuzungumza na waandishi wa habari na kuwataka waandishi hao wamuulize mkuu wa mkoa ambaye hakuweza kupatikana mara moja.

"Ninashughuli nyeti, kama mtakataka kushuhudia njooni kwa Mkuu wa Mkoa, au nendeni mkaongee naye atawapa jibu"alisema licha ya waandishi wa habari kufika ofisini kwake jana saa 4. asubuhi na kuwajibu kupitia msaidizi wake kuwa tumpigie simu saa nane mchana ili aaweze kutuambia yuko wapi tuweze kuzungumza naye.

Eneo linalogombaniwa na mzungu na wananchi hao mwanzoni kabla ya uhuru lilikuwa na ukubwa wa hekari 900 na baadaye hekari zaidi ya 200 ziligawiwa kwa wananchi na kubaki hekari 741.34 ambapo ardhi hiyo ilipimwa mwaka Septemba 15, mwaka 1927 na kugawawia wananchi mwaka 1961.

vyombo vingine vilivyochapisha habari za raia huyo ni tanzania daima na Channel ten tv

Friday, January 22, 2010

Ni kweli Uchumi wa wanahabari Nchini Tanzania u mikononi mwa wahariri

Na Gordon Kalulunga

TASNIA ya habari ni taaluma kama zilivyo taaluma nyingine ingawa tofauti yake moja kubwa ni kwamba iko karibu zaidi na wananchi.

Vyombo vya habari vimekuwa vikiibua mijadala mingi kupitia makala mbalimbali. Si wote wangependa mijadala hiyo kuibuliwa kwa kuwa inawagusa.

Lakini pamoja na vyombo vya habari kuwa na nguvu hiyo, waandishi wamekuwa wakikabiliwa na matatizo mbalimbali.

Kuna matukio mengi yanayowakumba waandishi nchini na duniani kwa ujumla na hivyo wengi kuogopa kufanyiwa unyama kama walivyowahi kutendewa wenzao.

Hapa nataka kuweka wazi kuwa kuna waandishi wa habari wengi ambao wamekufa hapa nchini na vifo vyao havielezeki kutokana na ama kuuliwa kikatili au kuuliwa kibaiolojia. Lakini pia baadhi kulundikwa kwenye mahabusu za polisi kwa visingizio vya sheria.

Hali ya namna hii inawatia hofu waandishi wengi hasa yanapotokea matukio ya kutisha ya namna hii kama lile lililotokea mkoa wa Mbeya ambako mwandishi John Lubungo amekufa na kifo chake kimeacha maswali mengi yasiyo na majibu kwa wanahabari wenyewe na wadau wengine wa habari hapa nchini.

John Lubungo alikuwa Mtangazaji wa ITV; alifariki akiwa na umri wa miaka 34 siku ya Ijumaa ya Januari 25, 2008 majira ya saa 5.00 usiku akiwa anaendesha gari dogo akitokea mjini Mbeya akielekea Tunduma, wilayani Mbozi, mkoa wa Mbeya yalikoweko makazi yake.

Nikimnukuu aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Mbozi, Halima Kihemba, aliyesema kwa masikitiko: “Lubungo alikuwa mtu wa karibu sana na serikali na alipigania sana maendeleo ya mji wa Tunduma, wilaya ya Mbozi na mkoa kwa ujumla; na hapa nimetumwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile, kuweka shada la maua kama ishara ya pole kwa familia na ndugu wengine.”

Naye aliyekuwa kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya, wakati huo, Suleiman Kova, ambaye ni mdau mkubwa wa wanahabari nchini, alisema alisikitishwa sana na kifo cha John Lubungo ambapo alimtaja John Lubungo kuwa mmoja wa waandishi ambao walikuwa wakiutetea na kuutangaza mkoa wa Mbeya na Tanzania kwa ujumla.

Kwa upande wake aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoani hapa kwa kipindi hicho, Christopher Nyenyembe, alisema kuwa kifo cha mwanahabari huyo kilitokea ghafla na kilileta mshtuko mkubwa kwa taaluma ya wanahabari na wadau wote waliokuwa wakishirikiana vyema na marehemu katika uhai wake.

Si hayo tu bali hata ofisi aliyokuwa akiitumikia wakati wa uhai wake ilitoa masikitiko makubwa sana kwa kumpoteza kati ya makamanda wake wa kampuni lakini cha ajabu licha ya kusikitika kote huko likaibuka sula moja nyeti kuwa mwandishi huyo hakuwa na mkataba na kampuni hiyo!

Jambo hilo halikuwashangaza waandishi wengi bali lilisikitisha sana kutokana na kumjua vema marehemu Lubungo wakati wa uhai wake hasa uchapaji kazi wake wa muda mrefu katika chombo chake.

Sina nia ya kumwelezea binafsi ndugu yetu huyo aliyetangulia mbele ya haki lakini nia ya makala hii ni kuweka bayana mateso wayapatayo waandishi wa habari hapa nchini hasa waandishi wa mikoani.

Moja ya kero kubwa kwa waandishi hao hasa wa mikoani ni malipo kidogo wanayoyapata kutoka kwenye vyombo vyao vya habari wanavyovifanyia kazi na kutopewa mikataba kama sheria za kazi za nchi zinavyoelekeza.

Suala hilo limezua kansa ya manug’uniko kwa waandishi wa habari kutokana na kutoweza kutafutiwa ufumbuzi wala mjadala wa kitaifa jambo ambalo linatafsiriwa na baadhi yao kuwa ni kuvunja haki za binadamu na kiraia.

Mmoja wa waandishi ambao wamelaani vikali suala la mapunjo ya malipo kwa waandishi wa habari hapa nchini ni Mkurugenzi wa Chuo cha Uandishi wa Habari (MIJO) kilichoko mkoani Mbeya, Jonas Mwasumbi.

Katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima kuhusu suluhisho la malalamiko ya muda mrefu ya waandishi wa habari juu ya malipo madogo wanayoyapata kutoka kwenye vyombo vyao wanavyofanyia kazi, alisema kuwa umefika wakati wahariri wa vyombo vya habari kubadilika kifikra na kimtazamo na waandishi wenyewe kujiendeleza zaidi kitaaluma.

Mwasumbi ambaye ni mwandishi mwandamizi wa magazeti ya Serikali hapa nchini na kiongozi wa muda mrefu wa MISA na taasisi nyeti za habari alisema kuwa tatizo hilo ni kubwa na linatokana na waandishi wenyewe na baadhi ya wahariri wao.

“Malalamiko hayo yanatokana na elimu ndogo waliyonayo baadhi ya waandishi ambayo haimwezeshi mwandishi kupata ajira na baadhi hawafahamu haki zao za msingi juu ya ajira.”

“Pamoja na hilo tatizo, lingine liko kwa wahariri ambao hawana utu wala dini na kuendelea kuwanyonya waandhishi wao hasa wa mikoani huku wakiendelea kutumia kwenye magazeti yao habari za waandishi hao ambao hawawalipi ipasavyo jambo ambalo ni dhambi mbaya sana,” alisema Mwasumbi.

Mkurugenzi huyo aliendelea kueleza kwamba wahariri wa vyombo mbalimbali hapa nchini wanapaswa kubadilika na kuheshimu haki za binadamu; vilevile kwa upande wa waandishi wa habari wanapaswa kuongeza viwango vyao vya elimu ili kupambana na utandawazi na soko la ajira kwa ujumla hasa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kwa mtazamo wangu na kutokana na malalamiko ya waandishi wa habari hapa nchini ni muhimu ikaibuliwa hoja na mjadala stahiki juu ya mustakabali wa waandishi wa habari Tanzania ili kutambua dhana nzima ya utawala bora kwa viongozi wetu waliokabidhiwa dhamana na kuwawezesha waandishi wa nchi hii kukabiliana na hali mbaya ya kiuchumi inayowakabili.

Pamoja na kuibua hoja ya maslahi ya waandishi wa habari hapa nchini, pia mjadala ulenge kutambua na kuthamini kivitendo si kinadhalia thamani ya waandishi wa habari katika taifa hili ili kujua mustakabali wa waandishi wa habari wa Tanzania.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.


Imetolewa kwenye gazeti la Tanzania Daima Toleo la januari 19,2010

unaweza kuisoma kwa kuki click hapa

kazi njema.

Thursday, January 14, 2010

Grants for investigative reporters to attend Global Investigative Journalism Conference 2010 at Geneva, Switzerland.

Jamani tunaendelea kuwaltea link ambazo mnaweza kunufaika

ebu jisomee mwenyewe kwa kugonga hapa
Imetolewa na Uongozi
Kagera Press Club

Wanaotaka kujitosa kwenye tuzo za CNN

Ndugu
Napenda kuwajulisha kwamba wale wote wanataka kushiriki katika tuzo za CNN muda unakaribia kwisha.

wenye kazi zao na maelezo zaidi ebu fungua hapa

au soma maelezo haya hapa chini(not edited)

2010 CNN MultiChoice African Journalist Awards>> CNN International and MultiChoice recently launched the CNN> MultiChoice African Journalist 2010 Awards.>> The winners will be announced at a gala ceremony to be held in> Kampala, Uganda in May 2010.>> John-Allan Namu, from Kenya, was awarded the top prize at the CNN> MultiChoice African Journalist 2009 Awards ceremony. Namu, reporter> for Kenya Television Network, won for his stories "In the shadow of> the Mungiki" and "Inside Story: Scars and Sufurias," which were chosen> from among 1665 entries from 38 nations across the African continent.>> Over the past fifteen years, the competition has grown in size and> status. In 2009, it attracted entries from 38 African countries and a> Highlights Programme of the ceremony, held in Durban, South Africa,> was broadcast in 44 African countries, on the Africa Channel in the> US, OBE TV and Southern Africa Direct in the UK and RTP Africa.>> Awards categories:>> - Arts & Culture Award> - Digital Journalism Award> - Economics & Business Award> - Environment Award> - Free Press Africa Award> - The HIV/AIDS Reporting Award> - Mohamed Amin Photographic Award> - MSD Health & Medical Award> - Print General News Award> - Radio General News Award> - Sport Award> - Television Features Award> - Television News Bulletin Award> - Tourism Award> - Francophone General News Awards> - Portuguese Language General News Award> - From these category winners, the judges choose the overall winner -> the CNN MultiChoice African Journalist 2010.>> Finalists in the 2010 competition will participate in a four day> finalists' programme that will include a media forum and networking> opportunities with senior journalists, editors, business leaders and> media owners from across the continent, culminating in a gala awards> ceremony in May, 2010.>> All finalists receive a cash prize and each category winner also> receives a laptop and printer. The CNN MultiChoice African Journalist> 2010 will receive an additional cash prize and a trip to the CNN> Center in Atlanta.>> The competition is open to African nationals who are professional> journalists including freelancers across print, television, internet,> photographic and radio.>> Full details on how to enter can be found by logging on at> www.cnn.com/africanawards.>> The closing date for entries is 28 January 2010. There will not be any> extensions of this closing date, and entries received after this date> may be disqualified.>> The judging will take place in March 2010.>> All entries should be broadcast or published during January 2009 -> December 2009.

Thursday, January 7, 2010

Waandishi tuweni makini kipindi cha lawama kwetu kimekwisha anza !



Wapendwa wanachama wa Kagera Press Club wanaofuatilia taarifa kama hizi kupitia blog hii na hasa waliko nje ya Manispaa ya Bukoba tunawaomba na kuwatahadharisha sana kuwa makini katika shuguli zao za kila siku za kuhabarisha jamii hasa katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

mfano tazama taarifa kama hii hapo juu iliyotolewa na CCM Bukoba mjini,ni taarifa nzuri lakini yenye kuitaji uangalizi mkubwa wakati wa kuandika stori kutoka kwenye taarifa hiyo kwa kutazama taratibu za kupata wagombea wa vyama,mapenzi ya watu nk.

Tumeweka taarifa hii si kwa lengo la kuibeza bali kuwalewesha kwamba kupitia taarifa hii waandishi wanaweza kulisha wananchi umbea,au kutumika kama kasuku tu.

Hata hivyo tunachukua nafasi hii kuwapongeza redio Kasibante Fm ya mjini bukoba kwa jinsi ilivyotanagaza habari hiyo (ya jana saa 3:00 usiku) kutoka kwenye taarifa hii na kuwaomba waandishi wengine ambao ni wanachama wa Kagera Press Club kuiga mfano wa uhariri uliofanywa na wahariri wa redio hiyo.

Tofauti na hapo waandishi tutaendelea kuwa 'makasuku' tu na kutumiwa na vyama badala ya kuchambua hoja kuhusu yale wanayotueleza na mwisho wake ni kupotosha jamii ambayo inakosa umakini katika kuchagua viongozi wanaowafaa na wenye kuwaletea tija.

Imetolewa na Uongozi
Kagera Press Club
Januari 7,2009

Tuesday, January 5, 2010

'Dili' la mafunzo huko Geneva Uswizi kuhusu Habari za Uchunguzi

Wapenzi Wanachama wa Kagera Press Club na wadu wengine wa habari,

Kama unataka kujiongeza ujuzi wa namna ya kuandika habari za uchunguzi unaweza kuomba kuhudhuria mafunzo yatakayofanyika Geneva Uswizi hapo April mwaka huu.

Kama una nia soma hapa kujua namna ya kuomba kuhudhuria kwa kufadhiliwa

kazi kwenu

Imetolewa na uongozi
Kagera Press Club