tag:blogger.com,1999:blog-85619792941449015672024-02-19T15:18:00.828-08:00KAGERA PRESS CLUBKagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.comBlogger24125tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-21081260692851896762010-09-12T07:43:00.000-07:002010-09-12T07:53:46.318-07:00Mwandishi Raymon Owaman wa RFA na Stav TV augua gafla!<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgcdFc_tHXyaYF7L0YfI9Jt1jMBO-kVbuE-u91S_JcTNe5aqO9D_CpK9RRIKdK5OmzmWSrpDhCUBJvJMZYsCCuFN18si6gtxyOr6G4Am3Ybp9Ox6NRXv1O_-TKTQSVvKiz7ekW8V4HqMSTw/s1600/1.png"><img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5516039588326183202" style="DISPLAY: block; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 200px; CURSOR: hand; HEIGHT: 150px; TEXT-ALIGN: center" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgcdFc_tHXyaYF7L0YfI9Jt1jMBO-kVbuE-u91S_JcTNe5aqO9D_CpK9RRIKdK5OmzmWSrpDhCUBJvJMZYsCCuFN18si6gtxyOr6G4Am3Ybp9Ox6NRXv1O_-TKTQSVvKiz7ekW8V4HqMSTw/s200/1.png" border="0" /></a> Mwandishi huyo pichani juu aliugua gafla nyumbani kwake maeneo ya Kashabo na kukimbizwa katika hospitali ya Mkoa Kagera jana jumamosi na hadi sasa amelazwa hapo.<br /><br />Taarifa kutoka kwa ndugu zake ni kuwa ugonjwa unaomsumbua mwandishi huyo bado haujajulikana na kwamba alianguka na kupoteza fahamu<br /><br />tutawajuza maendeleo ya mchapakazi huyo.<br /><br />imetolewa na Chama cha waandishi wa Habari Mkoani Kagera(KPC)Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com1tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-60166651880486316812010-09-07T02:06:00.000-07:002010-09-07T02:08:43.332-07:00Huyu 'Muhuni" kwenye msafara wa Kikwete analipwa na nani<p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Na <?xml:namespace prefix = st1 ns = "urn:schemas-microsoft-com:office:smarttags" /><st1:city st="on"><st1:place st="on">Antony</st1:place></st1:City> Mayunga<?xml:namespace prefix = o ns = "urn:schemas-microsoft-com:office:office" /><o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">NDEGE wa aina moja huruka kwa pamoja ,ni msemo wa wahenga wetu waliotutangulia,wakimaanisha watu wa itikadi moja hufanya mambo yao kwa pamoja.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Lakini msemo huo unakuwa kinyume kwa viongozi na wanachama wa baadhi ya vyama vya siasa kutokana na kampeni za uchaguzi mkuu unaoendelea kutawaliwa na vibweka vingi .<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Miongoni mwao ni kauli ya iliyotolewa na Katibu wa CCM<span style="mso-spacerun: yes"> </span>Taifa Yusuph Makamba kuhusiana taarifa kuwa kuna baadhi ya waandishi wa Habari walizuiwa kushiriki katika msafara wa Mgombea urais kupitia CCM<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Makamba alikaririwa na vyombo vya Habari akidai kuwa mtu aliyefanya hivyo ni mhuni mmoja bila kumtaja jina.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">“Huyo si uamuzi wa Chama ,ili uwe wa chama lazima uafikiwe na kamati kuu,Nec au uamzi afanye Katibu mkuu,vikao hivi havikufanyika kokote na mimi<br />katibu mkuu sijaagiza mtu awafukuze waandishi,fuatilia vizuri habari yako utagundua kuwa yupo mhuni amekosana nao akawafukuza,”mwisho wa kumnukuu Makamba wakati akihojiwa na gazeti la kila siku la Mwananchi.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Mimi nikiwa Mwandishi wa Habari kauli hiyo inanipa mashaka juu ya umakini wa chama hicho kikongwe<br />kuwa na ‘mhuni’ mmoja katika timu <st1:city st="on"><st1:place st="on">yao</st1:place></st1:City> ya kampeini ambaye anaweza kuamua kuwafukuza waandishi harafu wakaishia kumkandia huku akiendelea na uratibu.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Kwa mjibu wa kamusi mhuni ni Mwanamme ambaye hajaoa,kapera,mseja,mtu asiyekuwa na mahali maalum pa kuishi,mwizi ,mvunjaji<br />sheria,mnyang’anyi,mchopozi.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;"><st1:place st="on"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt">Kama</span></st1:place><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"> maana ni hiyo Makamba anataka kuwaambia wanachama wake kuwa wamekosa watu makini mpaka wakachukua watu wa namna hiyo.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><br /><span style="font-family:Times New Roman;">Anataka watanzania waamini kuwa Mgombea Urais wa CCM<span style="mso-spacerun: yes"> </span>katika timu ya kampeini ya mgombea huyo kuna baadhi ya watu ambao ni wavunjaji wa sheria,wasiojulikana makazi <st1:city st="on"><st1:place st="on">yao</st1:place></st1:City>.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Hivi kweli mhuni ambaye hajulikani anawezaje kupewa jukumu kubwa kama <st1:city st="on"><st1:place st="on">hilo</st1:place></st1:City> na akaharibu wakaishia kudai ni mhuni mmoja bila kuchukua hatua,hii si ni danganya toto?<br /><st1:place st="on">Kama</st1:place> ni kweli ‘mhuni’ huyo aliwafukuza waandishi kwenye msafara wa Kikwete ataachwa aendelee na kuratibu kazi za wasiokuwa wahuni, tutaraji nini.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Hivi watazinduka siku akimfukuza kiongozi wa CCM kwenye msafara ,na ni nani anamlipa mhuni huyo kwa kuzunguka na msafara huo?.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Inawezekanaje mhuni akapewa kitengo kizito cha kuamua mwandishi gani ashiriki msafara na nani abaki.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Je kwa kauli hiyo inamaanisha nani alimchagua na<span style="mso-spacerun: yes"> </span>alipewaje nafasi hiyo ili hali wakijuakuwa<br />ni mhuni.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Nadhani ipo haja ya kutueleza jina kamili la mhuni huyo<span style="mso-spacerun: yes"> </span>kwani Makamba alidhani kwa kusema hivyo kunatosha kuwaridhisha wananchi kuwa chama kimesikitishwa na kitendo hicho haramu.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Kwa kweli hizo ni porojo ambazo kwa zama hizi hazitakiwi kuvumiliwa maana kwa kufanya hivyo ,inatia shaka juu ya utendaji wa chama hicho kinachojigamba kila kukicha kuwa ni makini .<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Maana huwezi kupata chama makini bila kuwa na watendaji makini,kwanza.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Kwanini uhuru wa waandishi uingiliwe, na kwa maslahi ya nani.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Katika katiba ya Jamhuriya Muungano ya mwaka 1977 ibara ya18(d),kifungu hiki kinampa haki mwananchi ya kupewa taarifa mbalimbali muhimu kuhusu maisha na shughuli za wananchi na pia kuhusu masuala<br />muhimu kwa jamii na watu wa kufanya kazi hii ni waandishi wa Habari kama waliofukuzwa.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Hivyo kwa chama makini kukaa kimya kwa mtu kuvunja katiba ibara hiyo kwa kifungu (b)na (c)kwa waandishi wa habari,inawapa mashaka watanzania wanaotaraji kufanya maamzi yao sahihi oktoba 31 .<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Maana kwa kuwazuia waandishi kulikuwa na agenda ya siri isiyotakiwa kujulishwa jamii,ambayo inahitaji taarifa nani anafanya nini na wapi ,na anamkakati wa kuwafanyia nini watanzania.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Hivyo kumwachia “mhuni” rungu ya kubagua waandishi katika<span style="mso-spacerun: yes"> </span>kampeini za Kikwete ni hatari <st1:city st="on"><st1:place st="on">sana</st1:place></st1:City>.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Aidha waandishi wanaoandamana na wagombea waanchu ushabiki,kuvaa sare za vyama kwani hivyo ni kinyume na maadili ya taaluma.<o:p></o:p></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Kwa kuacha hulka hizo<span style="mso-spacerun: yes"> </span>watatenda kazi zao wakiwa huru,bila kuvalishwa nguo za chama ,na hayo ndiyo matarajio ya jamii kwa kipindi hiki ambacho<br />wanahitaji uchambuzi wa kina wa sera ,ilani na mikakati ya vyama vyote na wala si ushabiki.<i><o:p></o:p></i></span></span></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><i><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;">Mwandishi anapatikana kwa simu no 0787239480.</span></span></i></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><i><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;"></span></span></i> </p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 4.25pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><i><span style="FONT-SIZE: 9.5pt"><span style="font-family:Times New Roman;"><strong>Makala hii imetolewa kwenye gazeti Malengo Yetu Toleo la leo septemba 7,2010<o:p></o:p></strong></span></span></i></p><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><o:p><span style="font-family:Times New Roman;"> </span></o:p></p>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-11178251568046896242010-09-07T01:55:00.000-07:002010-09-07T02:05:50.473-07:00Mapungufu kwa wagombea wote haya hapa !<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgMp2K97rFGf32wb7bB9sH-1lwZ_JRi12antpabsWtyjACLtJqkgbUD7W-tDKpcQjSE3h7P_gIt68srjcHLjcv-iSN2TP9T5bHATMLwde-reKg0bCMIFClrMphFZg3luW-n8b_PHvvTgXhB/s1600/01+lusahunga.jpg"><img style="TEXT-ALIGN: center; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 171px; DISPLAY: block; HEIGHT: 200px; CURSOR: hand" id="BLOGGER_PHOTO_ID_5514094545702762018" border="0" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgMp2K97rFGf32wb7bB9sH-1lwZ_JRi12antpabsWtyjACLtJqkgbUD7W-tDKpcQjSE3h7P_gIt68srjcHLjcv-iSN2TP9T5bHATMLwde-reKg0bCMIFClrMphFZg3luW-n8b_PHvvTgXhB/s200/01+lusahunga.jpg" /></a> <img style="TEXT-ALIGN: center; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 200px; DISPLAY: block; HEIGHT: 106px; CURSOR: hand" id="BLOGGER_PHOTO_ID_5514094277819204370" border="0" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgpn4XXfa4eIHFCNgc4fxZkIA830zF_0XE_zc0My5XiLk_aX2wZXeu_Qla1wHwuPASNTKAvPzCLCQ_b7o9cADAThOdrW6UwXBsEtHoLLt2FYnQsYnSP3FmFmzI46LOi8ZY2I1HxU03r60AX/s200/left_pic2+chadema.jpg" /><img style="TEXT-ALIGN: center; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 200px; DISPLAY: block; HEIGHT: 177px; CURSOR: hand" id="BLOGGER_PHOTO_ID_5514094087842235650" border="0" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi4iEt25AIZdCMryE59AdWccfBM9sHMpfNZ7VmSKwAUEUqRhZ9E1VjMwfZP7XlZ-18fEiXa4C8hH1Su_Zsx69ecFWz-JpW7m7H2PDzHF8nFy8FjT4KVBcmgANIivjvPpb2PzlndfCFa4gfO/s200/lipduni+4.jpg" /> <div><div><div><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-size:9;"><span style="font-family:Times New Roman;"></span></span></p><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Na Mwandishi Wetu.<?xml:namespace prefix = o ns = "urn:schemas-microsoft-com:office:office" /><o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Harakati za kampeni zikiwa zimepamba moto kwa wagombea wa nafasi za Urais,Ubunge na Udiwani tayari kumejitokeza mapungufu makubwa ambayo iwapo hayatarekebishwa yanaweza kuathiri mantiki nzima ya mchakato wa uchaguzi Mkuu.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Aidha imebainika kuwa hakuna chombo chochote kinachoratibu kampeini za wagombea kubaini kama wanayoyafanya kwenye kampeini zao ni sawa au wafanye marekebisho.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Uchunguzi wa gazeti hili tangu kuanza rasmi kwa kampeini hizo August 20 mwaka huu umebaini kuwa wagombea wa nafasi za udiwani na ubunge wanafanya kampeini ambazo hazitoi nafasi kwa wapiga kura kuwapima.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Hivyo hivyo wagombea nafasi za Urais wakiwemo<span style="mso-spacerun: yes"> </span>Mutamwega Mutahywa(TLP),Hashimu Rungwe (NCCR-Mageuzi),Ibrahimu Lipumba,Willbroad Slaa(CHADEMA) na Jakaya Kikwete(CCM) ambao tayari wamezindua kampeini zao nao wamekumbwa na ‘ugonjwa huo’.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Kwa mjibu wa Uchunguzi huo ni kuwa kati ya wagombea hao hakuna hata mmoja anayetoa fursa za kuulizwa maswali au kuwataka wasikilizaji kupata ufafanuzi wa jambo lolote.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Imebanika kuwa wagombea wote wamekuwa wakihutubia tu na baada ya mkutano kuondoka huku wakiacha maswali mengi kwa wapiga kura ambao hukosa fursa ya kujua hasa mgombea alichosema .Na wanaotaka kupata ufafanuzi<span style="mso-spacerun: yes"> </span>wa jambo lililosemwa huachwa njia panda<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Mathalan,mgombea anasema kuwa iwapo atachaguliwa atahakikisha nchi inaondokana na umaskini kwa muda wa siku 100 lakini hatoi nafasi kwa wananchi kuuliza jambo juu ya hoja zake hizo.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Wapiga kura waliohojiwa walisema kuwa hawaoni haja ya kwenda kwenye mikutano ya kampeini kwani inakuwa kama wanapata hotuba zilizorekodiwa kupitia kwenye redio au Television.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Uchunguzi umebaini kuwa hata katika ratiba zao hakuna kipengele cha maswali bali kuna muda wa wagombea kuongea na wananchi na siyo kueleza sera zao.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">“Wote hawataki tuwaulize maswali<span style="mso-spacerun: yes"> </span>na wanatoi ahadi ambazo hata hazitekelezeki na wengine walishindwa kutekeleza kwa kipindi cha nyuma lakini kwa kuwa hawatoa fursa ya maswali wanatulisha sera zao tu na kuondoka”Alisema Bw Theresphory Maiko mkazi wa Rwamishenye Bukoba mjini.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Akihojiwa na gazeti hili Mwanasheria wa kituo cha Sheria na Haki za binadamu(LHRC) cha Jijini Dar Es Salaam Pasience Mlowe ni kuwa hayo ni mapungufu makubwa kikatiba.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Mlowe anasema kuwa iwapo wananchi hawapati fursa hivyo ni vigumu kuwapima wagombea kwani<span style="mso-spacerun: yes"> </span>na kwamba hii inaweza kuathiri mchakato wa kampeini kwao wengine wanaweza kudhani ndiyo utaratibu kumbe siyo.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">“Ni haki ya wananchi kikatiba,wananchi kuhoji mgombea juu ya jambo lolote alilosema kwenye mkutano au kupata ufafanuzi wa jambo hilo na kinyume chake ni makosa hivyo ni wajibu wa wananchi kudai haki hiyo” Alisema.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Kwa upande wake Rais wa Shirika la People Organization Transparency<span style="mso-spacerun: yes"> </span>Agency(POTA) Idrisa Masalu<span style="mso-spacerun: yes"> </span>ni kuwa hotuba zinazotolewa katika mikutano ya hadhara ni lazima wananchi wapate fursa ya kuuliza maswali.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">“Hii ni hasara kwa wagombea na wapiga kura kwani bila maswali,mgombea atapataje uhakika kama wapiga kura wameelewa na mpiga kura atajuaje kama anachosema mgombea ni sahihi”Alisema Masalu na kuongeza<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">“Sera siyo biblia,ni lazima mgombea aulizwe na ukiona anayekataa kufanya hivyo ujue hajiamini na anaogopa kuumbuka na kwa lugha nyepesi anapiga propanganda tu aelezi sera”.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Mbali na kasoro za kutokubali kuulizwa maswali pia imeibuka tabia ya baadhi ya wagombea kutoa ahadi zisizo tekelezeka na baadhi yao kufanya kampeini za matusi badala ya kueleza sera zao.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Mathalan,katika mikutano ya kampeini za CHADEMA,CUF na CCM ambazo zimefanyika katika uwanja wa mafumbo(CHADEMA),uwanja wa Uhuru(CUF na CCM) wagombea wamebanika kujadili mienendo ya wagombea wa vyama vingine tofauti na kueleza sera zao.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Wagombea hao wanatumia dakika 28 kati ya 30 walizopewa<span style="mso-spacerun: yes"> </span>kutukana,kueleza sifa mbaya za wagombea wa vyama vingine,kutoa taarifa zisizo na udhibitisho juu ya wenzao,uzuri wa chama chao na dakika mbili au tatu ndizo wanazotumia kueleza sera na nini watawafanyia wananchi iwapo watachaguliwa.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Aidha imegundulika pia kwenye ajenda za kujadili kwenye mikutano hiyo ya vyama zimo ajenda za kujadili wagombea wa vyama tofauti na vyao<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Baadhi ya wanachama<span style="mso-spacerun: yes"> </span>wa vyama vya siasa vya CHADEMA,CUF na CCM walihojiwa juu ya kasoro hizo katika kampeini wengi walionekana kutojua faida wala madhara yake huku wengine wakionekana kuwa nas jazba kwa kudai kuwa muuliza swali ametumwa na wapinzani wao.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Hakuna kiongozi yoyote wa Vyama hivyo ngazi ya mkoa aliyekuwa tayari kutoa ufafanuzi juu ya kasoro hizo kwa madai wao wanajua mbinu za kutumia wakati wa kampeini.<o:p></o:p></span></p><br /><br /><br /><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 11.35pt; MARGIN: 3.95pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Aidha Jeshi la polisi nchini limenoa askari wake na kuwapatia mavazi na vifaa vipya kama wanavyoonekana pichani mbele mahususi kwa ajili ya kudhibiti vurugu wakati wa mchakato wa uchaguzi kwa nchi nzima<o:p></o:p></span></p><br /><strong>Hii ndiyo habari kubwa kwa gazeti Malengo Yetu Toleo la leo Septemba 7,2010<br /></strong><br /><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><o:p><span style="font-family:Times New Roman;"></span></o:p></p></div></div></div>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-67953411652978468232010-08-26T00:51:00.000-07:002010-08-26T00:56:04.427-07:00Waandishi Kagera waanza ucgunguzi kwenye kata 30Kufuatia waandishi wa Habari mkoani kagera,kupata fedha kutoka TMF sasa wameanza rasmi uchunguzi kutafuta chanzo cha wananchi katika wilaya ya Bukoba kutojiandikisha kwa wingi kupiga kura na hata wachache wanaojiandikisha kutojitokeza kwa wingi kupiga kura<br /><br />Uongozi KPC unawatakia kazi njemaKagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-16846876990907931392010-08-16T04:40:00.000-07:002010-08-16T04:43:15.309-07:00Tahariri ya Gazeti Malengo Yetu Toleo No 14<p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="COLOR: black; FONT-SIZE: 40pt">Kauli hizi za wanasiasa wanawake hazifai !</span></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="COLOR: black; FONT-SIZE: 40pt"></span><?xml:namespace prefix = o ns = "urn:schemas-microsoft-com:office:office" /><o:p></o:p></span></b> </p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;">Wakati tunaunga mkono harakati za kutafuta usawa wa kijinsia zinazofanywa na Mh. Rais Jakaya Mrisho Kikwete, wanaharakati, wanawake wenyewe pamoja na sisi wanaume, katu hatuungi mkono fikra zinazopandikizwa sasa kuwa wanawake ni lazima kuwachagua wanawake wenzao.<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Katika awamu hii ya uongozi wa nchi unaokaribia kumaliza muda wake ukiahidi kuwa lengo <?xml:namespace prefix = st1 ns = "urn:schemas-microsoft-com:office:smarttags" /><st1:place st="on"><st1:placetype st="on">lake</st1:PlaceType> <st1:placename st="on">kuhusu</st1:PlaceName></st1:place> wanawake ni kuwa wawe asilimia hamsini kwenye vyombo vya maamuzi zinaenezwa fikra potofu zinazoashiria kuchochea hisia za ubaguzi na mapambano ya wanawake dhidi ya wanaume.<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Kuwa wanawake wako upande wao halikadhalika wanaume upande wao hali inayoashiria kujenga matabaka katika nchi yetu.<span style="mso-spacerun: yes"> </span>Hali hii haiwezi kupewa nafasi na kuachiliwa iendelee kwa kuwa itakuwa inapotosha dhana nzima ya kuwawezesha wanawake na badala yake kuifedhehesha jamii nzima.<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu wapiga kura waelimishwe kumchagua kiongozi mwadilifu, anayeelewa<span style="mso-spacerun: yes"> </span>matatizo yao, mwenye maono na ambaye ni sehemu ya jamii (‘anayekula na kuishi nao’kwa kila hali), lakini si kupiga debe achaguliwe fulani kwa sababu ya jinsi yake , kabila lake<span style="mso-spacerun: yes"> </span>au dini yake.<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Kwa hiyo tuwahamasishe wananchi wawachague viongozi bora na si kwa tofauti zao za kidini, kikabila wala kimaumbile. Hivyo yeyote atakayehamasisha watu kuwachagua wagombea kwa sababu ni wanawake na tofauti na yule anayepandikiza ubaguzi wa kidini au kikabila.<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Kauli kama hizi ni maarufu <st1:city st="on"><st1:place st="on">sana</st1:place></st1:City> katika kampeini ambazo tumeshuhudia hivi karibuni na hasa wakati wa kura za maoni za kuwatafuta wagombea wa vyama vya siasa. Mara utasikia, zinazotolewa kauli kwamba wanawake ni wenye huruma (kinyume chake wanaume ni wakatili ) wanawake wana upendo (wanaume wamejaa chuki ), wanawake ni waaminifu (wanaume si waaminifu)n.k.<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Ni mtazamo wetu kuwa kama ilivyo kwa baadhi ya wanaume, hata katika kundi la wanawake kuna wasio na upendo, wasio waaminifu, wakatili na hata majambazi. Ndiyo maana tunawasihi watanzania tumchague kiongozi kwa kuangalia uwezo na zifa alizonazo mgombea kama kiongozi bora bila kutanguliza jinsi, kuwapa nafasi wanawake kuchukuliwa kuwa ni vita au uadui kati ya wanawake na wanaume.<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Kama wanawake wote wataungana kuwaunga mkono wanawake wenzao tu,mwanaume gani atapita?. <o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Baadhi ya viongozi wa ngazi za juu wanawake walishawahi kutoa kauli za kuchefua hivi karibuni mfano, mmoja wapo ni kiongozi mmoja wa wanawake aliyekaririwa katika chombo kimoja cha habari akisema ‘’Rafiki wa mwanamke ni mwanamke’’.<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Baada ya siku chache kiongozi mmoja mwanamke akiwa kwenye ziara mkoani Arusha alikaririwa akiwataka wanawake kuwa na umoja na kupendana ili waweze kuwashinda wanaume katika uchaguzi mkuu.<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Haitoshi mwingine akiwa wilayani Arumeru alikaririwa na vyombo vya habari akisema, ‘’Wanawake ni jeshi kubwa wakishirikiana wanaweza kuwania na kugombea nafasi mbalimbali na kuwashinda wanaume’’.<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Hofu yetu sisi <i style="mso-bidi-font-style: normal">Malengo Yetu</i> ni kuwa kutokana na uwingi wa wanawake tutakuwa na bunge la wanawake, endapo kauli <st1:place st="on">kama</st1:place> hizo za viongozi maarufu na wenye ushawishi katika jamii zitaachwa kuendelea kutolewa. Kwa hali <st1:place st="on">kama</st1:place> hiyo lengo la 50 kwa 50 halitawezekana.<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Hata hivyo hatari nyingine inayoonekana ni kuwa sasa kuna kundi moja katika jamii ambalo limejipanga kuanzisha mapambano. Sasa hofu yetu inajengeka katika ukweli kuwa ni athari gani zinazoweza kujitokeza endapo kundi linaloshambuliwa katika jamii wakati wa mapambano hayo litaamua kujihami?<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Pengine sio rahisi kupata jibu. Sisi Malengo Yetu tunaamini kuwa mchakato kufikia malengo ya asilimia 50 kwa 50 za wanawake na wanaume katika nafasi za maamuzi hatuhitaji kutumia lugha za kuchochea mapambano bali kutumia uhamasishaji. Wengine katika lugha sanifu zaidi wanasema tunahitaji kutumia uzengeaji na uchechemuzi( lobbying and advocacy).<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Katika matumizi mabaya ya Demokrasia ipo mifano ya maamuzi ya ovyo yaliyofikiwa na kuwa na athari mbaya kwa jamii kutokana na kutumia kigezo cha wengi wape. Kwamba hata <st1:place st="on">kama</st1:place> wale wachache walikuwa na mawazo ya kufikiwa kwa maamuzi ya busara basi kwa kigezo cha upigaji kura wengi wenye maamuzi ya ovyo wakapata kura nyingi na uamuzi wao kuwa ndio utakaotumika kwa kigezo cha Demokrasia.<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;">Katika maana yake halisi Demokrasia ni kama mkondo wa maji mbayo hutiririka siku zote kutoka kileleni hadi bondeni, maji hayawezi yenyewe kupanda kilele cha mlima hadi nguvu fulani itumike.<o:p></o:p></span></b></p><p style="TEXT-ALIGN: justify; TEXT-INDENT: 5.65pt; MARGIN: 5.65pt 0in 0pt; mso-layout-grid-align: none" class="MsoNormal"><b><span style="font-family:Times New Roman;"><span style="mso-spacerun: yes"> </span>Kwa hiyo demokrasia ya wanawake kushika nafasi za uamuzi<span style="mso-spacerun: yes"> </span>kwa asilimia 50 kwa 50 inabidi itumike kwa busara katika uchaguzi ujao. Isije kuwa kulazimisha maji kupanda kilele cha mlima. Lengo la uchaguzi si wanawake kuwashinda wanaume bali ni kushindanisha hoja, fikira,mitazamo,maono<span style="mso-spacerun: yes"> </span>na uwezo wa kuwa kiongozi bora wa wanaume, wanawake na watoto.<o:p></o:p></span></b></p><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><span style="FONT-SIZE: 14pt"><o:p><span style="font-family:Times New Roman;"> </span></o:p></span></p>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-11582891031595401022010-07-21T06:59:00.000-07:002010-08-03T00:10:01.718-07:00Kagera Press Club yapata milioni 40 kutoka TMF !<div><div></div><div><br /><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Na Mwandishi Wetu.</span><br /></p><br /><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Chama cha Waandishi mkoa wa Kagera(KPC) kimepata jumla ya shilingi milioni 40 kutoka mfuko wa kusaidia vyombo vya habari na waandishi wa habari nchini Tanzania(TMF) .</span><br /></p><br /><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Fedha hizo zitatumiwa na wanachama wa KPC kufanya uchunguzi na kuripoti kwenye vyombo wanavyowakilisha kuhusuaiana na masuala ya uchaguzi katika majimbo ya uchaguzi ya Bukoba mjini na Bukoba vijiini.</span><br /></p><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Waandishi hao watawezeshwa kufika katika maeneo ya vijiji,kata na kuchunguza sababu zinazosababisha wananchi kutijipokeza kwa wingi kujiandisha kwenye daftari la wapiga kura na<span style="mso-spacerun: yes"> </span>kupiga kura katika<span style="mso-spacerun: yes"> </span>majimbo hayo.</span><br /><br /></p><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Viongozi wa KPC ambao ni Mwenyekiti wa Bw Gilbert Makwabe na Katibu Bw Mathias Byabato walisaini mkataba<span style="mso-spacerun: yes"> </span>kwa ajili ya kupokea fedha hizo kwenye Ofisi za Tanzania Media Fund(TMF) Jijini Dar Es Salaam Julai 21,2010 kwa niaba ya wanachama wa KPC.</span></p><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><?xml:namespace prefix = o ns = "urn:schemas-microsoft-com:office:office" /><o:p><span style="font-family:Times New Roman;"></span></o:p></p><br /><br /><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Akiongea kabla ya kusaini mkataba huo Meneja wa TMF Bw Ernest Sungura aliwapongeza wanachama wa KPC kwa kufanikiwa kupata fedha hizo na <span style="mso-spacerun: yes"></span>kuwa<span style="mso-spacerun: yes"> </span>KPC imepewa fedha baada ya andiko lao kukidhi vigezo na kwamba awali watapewa asilimia 82 ya fedha hizo na asilimia 18 watapewa baada ya kukamilisha mradi huo.</span></p><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><o:p><span style="font-family:Times New Roman;"></span></o:p></p><br /><br /><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Akiongea kwa niaba ya KPC Mwenyekiti wake Bw Makwabe aliishukuru TMF kwa kutoa fedha<span style="mso-spacerun: yes"> </span>hizo na kuhaidi kufanya kazi kulingana na makubaliano yaliyopo kwenye andiko lenyewe na mkataba.</span><br /></p><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><o:p><span style="font-family:Times New Roman;"></span></o:p></p><br /><br /><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><span style="font-family:Times New Roman;">Kwa mjibu wa andiko <?xml:namespace prefix = st1 ns = "urn:schemas-microsoft-com:office:smarttags" /><st1:place st="on"><st1:city st="on">hilo</st1:city></st1:place> wanachama hao watalazimika kufanya kazi kwa muda wa miezi sita<span style="mso-spacerun: yes"> </span>kuanzia Agust 2010<span style="mso-spacerun: yes"> </span>hadi Januari 2011.<img style="TEXT-ALIGN: center; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 200px; DISPLAY: block; HEIGHT: 88px; CURSOR: hand" id="BLOGGER_PHOTO_ID_5501077081907505554" border="0" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj-PUMINWo9MIaY7kTzcGuA5vrpXujVSnTl1WUwlTs2vwg9k8F0uXT9SR49kFXPnIvBop9fDojHsPfnT0jwq5ZgOPjZqAelxWIJ9dQVed1JsiX3I15VOrlJhMjtzAlILA9tESFwNgYxxcU-/s200/DSC01345+mpya.JPG" /></span></p><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><o:p><span style="font-family:Times New Roman;"></span></o:p></p><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><o:p><span style="font-family:Times New Roman;"></span></o:p></p><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><o:p></o:p></p><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><o:p><span style="font-family:Times New Roman;"></span></o:p></p><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"> </p><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><b style="mso-bidi-font-weight: normal"><span style="font-family:Times New Roman;">Pichani:Katibu wa Kagera Press Club Bw Mathias Byabato (Kulia) akisaini mkataba wa kupokea shilingi milioni arobaini kutoka TMF ,Katikati ni Meneja wa TMF Bw Ernest Sungura na kushoto ni Afisa wa TMF anayehusika na masuala ya ruzuku za mashirika Bw <span class="fontdarkgray1"><span style="color:#222222;">Derek Murusuri</span></span><span class="cgselectable"> </span><o:p></o:p></span></b></p><br /><br /><p style="MARGIN: 0in 0in 0pt" class="MsoNormal"><o:p><span style="font-family:Times New Roman;"></span></o:p></p></div></div>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-43106867754579534652010-03-23T06:13:00.000-07:002010-03-23T06:19:13.400-07:00Mzungu anayecharaza wananchi viboko mbaroni<a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgD0arEdpjmVxpI79Whx4pal5DwZ1qM4ZdOqZemS1M1_CWo4_vV1V7u6s3BHXUg-04hXjvhke4h3uzh6Irhn5z_U4y9XiXn9wSoCvRH5TPVH-g9ybB18NFDTwZiTD46aSr73ip7xjjgW2Fg/s1600-h/DSC00003.JPG"><img style="margin: 0px auto 10px; display: block; text-align: center; cursor: pointer; width: 153px; height: 200px;" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgD0arEdpjmVxpI79Whx4pal5DwZ1qM4ZdOqZemS1M1_CWo4_vV1V7u6s3BHXUg-04hXjvhke4h3uzh6Irhn5z_U4y9XiXn9wSoCvRH5TPVH-g9ybB18NFDTwZiTD46aSr73ip7xjjgW2Fg/s200/DSC00003.JPG" alt="" id="BLOGGER_PHOTO_ID_5451818023456991058" border="0" /></a><br />Gazeti Malengo Yetu toleo la leo limeripoti kuwa yule mzungu ambasye taarifa zake ziliwekwa katika blog hii kuwa amekatwa na vyombo vya dola na kuwa juhudui za kukamatwa kwa raia huyo wa kifgeni zimefanywa na gazeti hilo.<br /><br />vizuri sanaKagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com1tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-4475338731069290662010-02-16T05:09:00.000-08:002010-02-16T05:13:32.003-08:00Gazeti Malengo Yetu litakuwa mitaani kuanzia februari 23 mwaka huuWapenzi wa gazeti Malengo Yetu linalotolewa na Chama cha waandishi wa Habari Mkoani Kagera(KPC) litaanza kuonekana terna mitaani kuanzia februari 23 mwaka huu siku ya jumanne likiwa na marekebisho makubwa.<br /><br />Gazeti hilo lilikuwa katika marekebisho yaliyotuchukua siku kadhaa bila kuonekana mitaani<br /><br />Tuongeni mkono kwa kununua gazeti hilo ukiwa Kagera,Mara,Shinyanga,Mwanza na Kigoma<br /><br />Imetolewa na<br />Uongozi<br />KPCKagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-49087507740196941892010-02-01T02:30:00.000-08:002010-02-01T02:32:27.207-08:00Mwandishi wa Habari Mkongwe afariki Dunia<strong><span style="font-size:180%;">PRESS RELEASE</span></strong><br /><br /><span style="font-size:130%;">TANGAZO LA KIFO CHA MWANACHAMA WA KPC<br /></span><br />Uongozi wa chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Kagera (KPC) unasikitika kutangaza kifo cha mwanachama wake na mmoja wa waanzilishi wa chama hicho Bw.Dominick Rweyemamu.<br /><br />Bw. Rweyemamu amefariki usiku wa kuamkia leo februari 1,2010 katika hospital ya Ndolage Muleba, alipokuwa akipatiwa matibabu,<br /><br />Bw. Rweyemamu aliwahi kuwa mtumishi wa serikali katika Idara ya Habari Maelezo, na baada ya kustaafu alishirikiana na waandishi wenzao mwaka 1998 wakianzisha chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Kagera.<br /><br />KPC,waandishi wa Habari wote mkoa wa Kagera wamepokea kwa masikitiko taarifa za kifo hicho na inaomba ndugu,jamaa ,familia yake kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu.<br /><br />Mungu alitoa, Mungu ametwaa jina lake liabudiwe, AMINA.<br /><br /><br /><br />Imetolewa na<br />M. Byabato<br />Katibu Mtendaji<br />Kagera Press ClubKagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-58869508710531612682010-01-29T07:27:00.000-08:002010-01-29T07:36:31.057-08:00Mkutano mkuu wa KPC ni Februari 12,2010 !Wanachama wote wa Kagera Press Club mnatangaziwa kuwa mkutano mkuu wa mwaka uliokuwa ufanyike novemba 2009 sasa utafanyika februari 12,2010 kwenye ofisi za KPC.<br /><br />Maelezo zaidi yatawekwa kwenye blog hii,kutumiwa barua na kupigiwa simu.<br /><br />kwa waliooko bukoba mjini mnaweza kusoma tangazo la mkutano huo kwenye ubao wa matangazo wa KPC.<br /><br />Imetolewa na<br /> G.Makwabe<br /> Mwenyekiti KPCKagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-50042886957241411832010-01-27T04:00:00.000-08:002010-01-27T04:45:51.680-08:00Ukweli kuhusu 'Mzungu' anayecharaza wananchi viboko Kagera !<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjb5psRYtwi3lpD0fDTy698HsWipZpeCGS0HxINzkdAdiEK2jLHcixb0og5lhkUluKZNmNJaTCoYr02H5WFkbRPzwkkHBELRQP7334l7KFnv6sNxoaNh3-DNCAZIxC3DKlAa-mLXnXmW3aW/s1600-h/DSC04955.JPG"><img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5431399414221091298" style="DISPLAY: block; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 200px; CURSOR: hand; HEIGHT: 150px; TEXT-ALIGN: center" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjb5psRYtwi3lpD0fDTy698HsWipZpeCGS0HxINzkdAdiEK2jLHcixb0og5lhkUluKZNmNJaTCoYr02H5WFkbRPzwkkHBELRQP7334l7KFnv6sNxoaNh3-DNCAZIxC3DKlAa-mLXnXmW3aW/s200/DSC04955.JPG" border="0" /></a> Baadhi ya waandishi wakifanya mahojiano na wakazi wa kijiji cha Ijumbi wanaoishi kwa mashka.<br /><div><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjOJSkUSTISc7vmP9npzKYPJCBj7VnhDZXFhtUeMg5xSSOaRFvw5670C8pHzR4DXyCoxSiYxAI6bKIoSX6JsGx5WjvGY7BQrq0sJ1pXeSdf78Qb7Xs3cDZuNxlAMYk4FT4JDb9vBE5tt7C_/s1600-h/DSC04947.JPG"><img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5431398660928068130" style="FLOAT: right; MARGIN: 0px 0px 10px 10px; WIDTH: 150px; CURSOR: hand; HEIGHT: 200px" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjOJSkUSTISc7vmP9npzKYPJCBj7VnhDZXFhtUeMg5xSSOaRFvw5670C8pHzR4DXyCoxSiYxAI6bKIoSX6JsGx5WjvGY7BQrq0sJ1pXeSdf78Qb7Xs3cDZuNxlAMYk4FT4JDb9vBE5tt7C_/s200/DSC04947.JPG" border="0" /></a><br /><br /><div><br /><br /><br /><div><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj267x70A81_PiWTLNZF7BX5QR9ba-sxIIZl3iowUBpTIAK0Ugk5spQ6mpLawVtUtQu-akqMmqhv7ADEJY_LsAWjkB4gxKSxuz3xt9FeGd6q6rNNj7HyahlQvHoP1FCMhinasBR8JC4XU00/s1600-h/DSC04982.JPG"><img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5431394381630318082" style="DISPLAY: block; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 200px; CURSOR: hand; HEIGHT: 150px; TEXT-ALIGN: center" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj267x70A81_PiWTLNZF7BX5QR9ba-sxIIZl3iowUBpTIAK0Ugk5spQ6mpLawVtUtQu-akqMmqhv7ADEJY_LsAWjkB4gxKSxuz3xt9FeGd6q6rNNj7HyahlQvHoP1FCMhinasBR8JC4XU00/s200/DSC04982.JPG" border="0" /></a> Licha ya kucheka lakini wanacharazwa bakora,wengine ni wazee sana<br /></div><br /><div><br /><div>Taarifa za kuwepo raia mmoja wa kigeni anayenyanyasa wananchi zimekuwa zikiripotiwa na vyombo kadhaa vya habari lakini kagera press club iliwatuma waandishi 7 wa vyombo kadhaa kuchunguza chanzo cha mgogoro huo.</div><br /><div></div><br /><div>kilichobainika ni hiki hapa.<br /><br /></div><br /><div><strong>Na Mwandishi wa Blogspot</strong><br /><br /><span style="color:#3333ff;">KATIKA hali isiyo ya kawaida wananchi wapatao 100 wa kitongoji cha Bujenjeke kijiji cha Ruhija kata ya Ijumbi wamekuwa waakilazimika kuhamisha makazi yao porini kukwepa kipigo kutoka wanamgambo wakishirikiana na askari polisi wanaodaiwa kununuliwa na raia wa kigeni.<br /><br />JESHI la polisi mkoani Kagera limejikuta likiwa katika lindi la mgogo mkubwa kwa kile kinachodaiwa kuwa kumkingia kifua raia wa kigeni anayedaiwa kuwanyanayasa wananchi na kuwalazimu kukimbia nyumba zao na kulala vichakani zaidi ya mwezi mmoja sasa.<br /><br />Hayo yamebainika jana baada ya kundi la waandishi wa habari wa mkoani Kagera kulazimika kufanya ziara ya siku moja ya kwenda kuchunguza malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wananchi ya kudai kunyanyaswa na Mzungu ambaye ni anadaiwa kuwa ni raia wa nchini Uingereza.<br /><br />Wakizungumza na waandishi wa habari wakazi wa kijijini hapo, walidai kuwa kwa kipindi kirefu wamekuwa wakilala na kushinda porini, kukwepa kupigwa na askari polisi wanaodaiwa kuwa katika ofisi ya Kamanda wa polisi Mkoani Kagera na wanamgambo wanaokodishwa kutoka maeneo yaasiojulikana kutokana na mavazi wanayovaa aina ya kininja.<br /><br />Katika uchunguzi uliofanywa na kundi hilo la wandishi wa habari kutoka chama cha waandishi mkoa wa Kagera(Kagera Press Club) uliweza kubaini kutokuwepo kwa dhana ya utekelezaji wa kilimo kwanza kutokana na kutokuwepo hata shamba jipya linaloonesha kulimwa hivi karibuni zaidi ya zamani kukanda, huku wananchi wakidai kuwa wanashindwa kujishughulisha na kazi za kilimo kutokana na vitisho, vipigo na kuswekwa rumande kwa kubambikiziwa kesi.<br /><br />Mmoja wa wakazi hao aliyejitambulisha kwa jina la Bahabti Mussa (32) alisema chanzo cha migogoro hiyo ni baaada ya mzungu huyo raia wa Uoingereza, Robert Maintland kwenda kijijini hapo, mwaka 2003 ambapo alifika na kuweka kuanza kuweka vigingi bila kuishirikisha jamii iliokuwa ikiishi hapo, na baadaye kuondoka na kurudi Uingereza.<br /><br />Alisema mwaka 2008 Maintland alirejea tena nchini na baada ya siku tano kupita badhi ya wananchi walienda kumsalimia kama jirani yao, ambapo katika hali isiyo ya kawaida aliwataka waondoke katika eneo hilo.<br /><br />Hata hivyo, Musa alisema kuwa walilazimika kumhoji wakiondoka wakiondoka atawalipa, ambapo aliwajibu kuwa angewalipa kuanzia sh. 100,000 hadi 350,000 na kumwambia Mussa kuwa kwa kuwa yeye ni msemaji sana angweweza kumlipa sh. 500,000 kitu ambacho wanchi hao hawakuweza kuafikiana naye, ambapo aliwaambia kuwa asiyeafikiana naye atakipata cha 'moto'.<br /><br />Naye Elenestina Eleneus (74) alisema yeye kutokana na kutokuwa na nguvu anapata shida kwa kipindi kwa vurugu na vitisho vinavyofanywa askari hivyo amekuwa akishinda vichakani ili kunusuru uhai wake.<br /><br />Alisema tangu uhai wake hajawahi kushuhudia hali hiyo hapa nchini hasa katika kitongoji hicho.<br />Alisema kwa sasa hata vifaa vyajke vya kupikia vimsombwa na askari hao na kwenda navyo kusikojulikana na hivyo kulazimika kulia kwenye majani ya migomba.<br /><br />Jenipha Romwad (29) alidai Novemba 2, 2008 saa 2 asubuhi alipata kipigo kikali kutoka kwa askari akiongozwa na mwanagambo mmoja aliyemtambua kwa jina moja la James huku mzungu akivurumisha risasi kadhaa hewani ya kuwatishia ulifanya mimba yake miezi minane kutoka na kufariki, pamoja na maumivu hayo alisondekwa rumande siku mbili katika kituo cha Muleba kwa madai kuwa ni wavamizi wa ardhi ya Mzungu.<br /><br />"Nikiwa na mtoto wa mwingine, nilipigwa teke la kiunoni na tumboni na huyo askari hadi kusababisha mimba yangu ya miezi minane kutoka, cha kushanga pamoja na ugonjwa wangu wala polisi pale Muleba hawakunijali hata kunipa huduma na hata sijui kichanga alikozikwa wala hata jinsi yake"alisema.<br /><br />Mzee Kasenene (80) anayedaiwa kuwa alikuwa mpishi wa mmiliki wa shamba hilo aliyejulikana kwa jina la Peter Pantelakis alisema kwamba wamekuwa wakiishi kwa matesho makubwa kutoka na uwepo wa raia huyo wa kigeni.<br /><br />Kwa upande wa Mzungu Robert Maintland ambaye hakuwepo katika eneo hilo akizungumza na waandishi wa habari kwa njia ya simu, alisema kuwa ardhi yake na hakuna hata raia wa Tanzania anayeishi pale kwani wote ni Warundi waliokuwa vibarua wa babu yake.<br /><br />"Hakuna hata mtu wa Mtanzania nayeishi katika eneo lile, wote ni Warundi, ambao wanatabia mbaya za kubaka kuua,wakata miti ovyo"alisema.<br /><br />Hata hivyo, Maintlanda alidai watu hao wanatumwa na Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini Wilson Masuilingi kuendeela kusihi karika ardhi yake ili aendelee kupata wapiga kura wengi.<br /><br />Kuhusu kuwavamia na kuwapiga wananchi kulazimika kuhama makazi yao kwa kushirikiana na askari na wanamgambo anaowakodi kutoka katika maeneo yasojulikana, alikataa na kusema kuwa yeye hajui na wala hajui kufanya hivyo na kwamba hayo ni majungu anayopikiwa juu yake ya kumpaka matope.<br /><br />Halikadhalika kuhusu kuwazuia wananchi kuchukua aina yoyote ya mazao kutoka kwenye msitu unaowanguka, mazao kuvuna mazao waliolima na hata kulima na kutumia maji ya Kurumiyo yalioko katika kitongoji hicho kwa matumizi ya nyumbani alidai kuwa hakuwahi na kwamba yote hayajui.<br /><br />Mbunge wa Jimbo la Kusini, Masilingi akuzunguzia sakata hilo, alikiri kupokea taarifa za malalamiko ya manyanyaso waofanyiwa wananchi hao na huyo raia wa Kigeni na kufanya mikutano wa hadhara katika kitongoji hicho akiwa na Mkuu wa wilaya ya Muleba, Angelina Mabula ambapo waliagiza raia huyo wa kigeni akamatwe na kuchukuliwa hatua, lakini anashangaa hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kwake.<br /><br />Alisema wananchi walitakiwa kubaki katika kitongoji chao na kuendelea na shughuli zao kama wananchi wa kawaida.<br /><br />Alisema katika suala nzima ya Kitingoji hicho kutaka taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa kuingilia kati na kuchunguza mgogoro wake ambao umegubikwa na harufu za rushwa.<br /><br />Alisema mzungu huyo anataka kumiliki kitongoji kizima wakazi wakazi hao waliwepo katika eneo hilo miaka mingi, na kwamba katika eneo hilo kuna mgogo wa wanafamilia baina ya mzungu na ndugu zake, mgogoro ambao wananchi hawahusiki kabisa.<br /><br />Kuhusu ujenzi wa vigingi alisema kuwa unatokana na maafisa wa ardhi kula rushwa, kwani ujenzi huo haujahusisha wakazi wa eneo lile, kwa nini ijengwe vigingi wakati serikali.<br /><br />Naye Kamanda wa polisi Mkoa Kagera Bw Henery salewi alipotakiwa na waandfishi wa habari kuelezea juu ya mgogoro huo unaodaiwa kuwa polisi wake ndiyo wamekuwa wakitumiwa na mzungu huyo kwenda katika kitongoji kuwatishia wananchi na kuwapora mali zao huku wenginew akiwapiga hadi kuharibiwa kwa mimba zao , alikataa kuonana hata kuzungumza na waandishi wa habari na kuwataka waandishi hao wamuulize mkuu wa mkoa ambaye hakuweza kupatikana mara moja.<br /><br />"Ninashughuli nyeti, kama mtakataka kushuhudia njooni kwa Mkuu wa Mkoa, au nendeni mkaongee naye atawapa jibu"alisema licha ya waandishi wa habari kufika ofisini kwake jana saa 4. asubuhi na kuwajibu kupitia msaidizi wake kuwa tumpigie simu saa nane mchana ili aaweze kutuambia yuko wapi tuweze kuzungumza naye.<br /><br />Eneo linalogombaniwa na mzungu na wananchi hao mwanzoni kabla ya uhuru lilikuwa na ukubwa wa hekari 900 na baadaye hekari zaidi ya 200 ziligawiwa kwa wananchi na kubaki hekari 741.34 ambapo ardhi hiyo ilipimwa mwaka Septemba 15, mwaka 1927 na kugawawia wananchi mwaka 1961. </span><br /></div><div>vyombo vingine vilivyochapisha habari za raia huyo ni <a href="http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=12447">tanzania daima </a>na <a href="http://www.chten.tv/">Channel ten tv</a></div></div></div></div>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-44122793141783304372010-01-22T08:12:00.000-08:002010-01-22T08:17:40.321-08:00Ni kweli Uchumi wa wanahabari Nchini Tanzania u mikononi mwa wahariri<div class="text1">Na Gordon Kalulunga<p>TASNIA ya habari ni taaluma kama zilivyo taaluma nyingine ingawa tofauti yake moja kubwa ni kwamba iko karibu zaidi na wananchi. </p><p>Vyombo vya habari vimekuwa vikiibua mijadala mingi kupitia makala mbalimbali. Si wote wangependa mijadala hiyo kuibuliwa kwa kuwa inawagusa. </p><p>Lakini pamoja na vyombo vya habari kuwa na nguvu hiyo, waandishi wamekuwa wakikabiliwa na matatizo mbalimbali. </p><p>Kuna matukio mengi yanayowakumba waandishi nchini na duniani kwa ujumla na hivyo wengi kuogopa kufanyiwa unyama kama walivyowahi kutendewa wenzao. </p><p>Hapa nataka kuweka wazi kuwa kuna waandishi wa habari wengi ambao wamekufa hapa nchini na vifo vyao havielezeki kutokana na ama kuuliwa kikatili au kuuliwa kibaiolojia. Lakini pia baadhi kulundikwa kwenye mahabusu za polisi kwa visingizio vya sheria. </p><p>Hali ya namna hii inawatia hofu waandishi wengi hasa yanapotokea matukio ya kutisha ya namna hii kama lile lililotokea mkoa wa Mbeya ambako mwandishi John Lubungo amekufa na kifo chake kimeacha maswali mengi yasiyo na majibu kwa wanahabari wenyewe na wadau wengine wa habari hapa nchini. </p><p>John Lubungo alikuwa Mtangazaji wa ITV; alifariki akiwa na umri wa miaka 34 siku ya Ijumaa ya Januari 25, 2008 majira ya saa 5.00 usiku akiwa anaendesha gari dogo akitokea mjini Mbeya akielekea Tunduma, wilayani Mbozi, mkoa wa Mbeya yalikoweko makazi yake. </p><p>Nikimnukuu aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Mbozi, Halima Kihemba, aliyesema kwa masikitiko: “Lubungo alikuwa mtu wa karibu sana na serikali na alipigania sana maendeleo ya mji wa Tunduma, wilaya ya Mbozi na mkoa kwa ujumla; na hapa nimetumwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile, kuweka shada la maua kama ishara ya pole kwa familia na ndugu wengine.” </p><p>Naye aliyekuwa kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya, wakati huo, Suleiman Kova, ambaye ni mdau mkubwa wa wanahabari nchini, alisema alisikitishwa sana na kifo cha John Lubungo ambapo alimtaja John Lubungo kuwa mmoja wa waandishi ambao walikuwa wakiutetea na kuutangaza mkoa wa Mbeya na Tanzania kwa ujumla. </p><p>Kwa upande wake aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoani hapa kwa kipindi hicho, Christopher Nyenyembe, alisema kuwa kifo cha mwanahabari huyo kilitokea ghafla na kilileta mshtuko mkubwa kwa taaluma ya wanahabari na wadau wote waliokuwa wakishirikiana vyema na marehemu katika uhai wake. </p><p>Si hayo tu bali hata ofisi aliyokuwa akiitumikia wakati wa uhai wake ilitoa masikitiko makubwa sana kwa kumpoteza kati ya makamanda wake wa kampuni lakini cha ajabu licha ya kusikitika kote huko likaibuka sula moja nyeti kuwa mwandishi huyo hakuwa na mkataba na kampuni hiyo! </p><p>Jambo hilo halikuwashangaza waandishi wengi bali lilisikitisha sana kutokana na kumjua vema marehemu Lubungo wakati wa uhai wake hasa uchapaji kazi wake wa muda mrefu katika chombo chake. </p><p>Sina nia ya kumwelezea binafsi ndugu yetu huyo aliyetangulia mbele ya haki lakini nia ya makala hii ni kuweka bayana mateso wayapatayo waandishi wa habari hapa nchini hasa waandishi wa mikoani. </p><p>Moja ya kero kubwa kwa waandishi hao hasa wa mikoani ni malipo kidogo wanayoyapata kutoka kwenye vyombo vyao vya habari wanavyovifanyia kazi na kutopewa mikataba kama sheria za kazi za nchi zinavyoelekeza. </p><p>Suala hilo limezua kansa ya manug’uniko kwa waandishi wa habari kutokana na kutoweza kutafutiwa ufumbuzi wala mjadala wa kitaifa jambo ambalo linatafsiriwa na baadhi yao kuwa ni kuvunja haki za binadamu na kiraia. </p><p>Mmoja wa waandishi ambao wamelaani vikali suala la mapunjo ya malipo kwa waandishi wa habari hapa nchini ni Mkurugenzi wa Chuo cha Uandishi wa Habari (MIJO) kilichoko mkoani Mbeya, Jonas Mwasumbi. </p><p>Katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima kuhusu suluhisho la malalamiko ya muda mrefu ya waandishi wa habari juu ya malipo madogo wanayoyapata kutoka kwenye vyombo vyao wanavyofanyia kazi, alisema kuwa umefika wakati wahariri wa vyombo vya habari kubadilika kifikra na kimtazamo na waandishi wenyewe kujiendeleza zaidi kitaaluma. </p><p>Mwasumbi ambaye ni mwandishi mwandamizi wa magazeti ya Serikali hapa nchini na kiongozi wa muda mrefu wa MISA na taasisi nyeti za habari alisema kuwa tatizo hilo ni kubwa na linatokana na waandishi wenyewe na baadhi ya wahariri wao. </p><p>“Malalamiko hayo yanatokana na elimu ndogo waliyonayo baadhi ya waandishi ambayo haimwezeshi mwandishi kupata ajira na baadhi hawafahamu haki zao za msingi juu ya ajira.” </p><p>“Pamoja na hilo tatizo, lingine liko kwa wahariri ambao hawana utu wala dini na kuendelea kuwanyonya waandhishi wao hasa wa mikoani huku wakiendelea kutumia kwenye magazeti yao habari za waandishi hao ambao hawawalipi ipasavyo jambo ambalo ni dhambi mbaya sana,” alisema Mwasumbi. </p><p>Mkurugenzi huyo aliendelea kueleza kwamba wahariri wa vyombo mbalimbali hapa nchini wanapaswa kubadilika na kuheshimu haki za binadamu; vilevile kwa upande wa waandishi wa habari wanapaswa kuongeza viwango vyao vya elimu ili kupambana na utandawazi na soko la ajira kwa ujumla hasa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. </p><p>Kwa mtazamo wangu na kutokana na malalamiko ya waandishi wa habari hapa nchini ni muhimu ikaibuliwa hoja na mjadala stahiki juu ya mustakabali wa waandishi wa habari Tanzania ili kutambua dhana nzima ya utawala bora kwa viongozi wetu waliokabidhiwa dhamana na kuwawezesha waandishi wa nchi hii kukabiliana na hali mbaya ya kiuchumi inayowakabili. </p><p>Pamoja na kuibua hoja ya maslahi ya waandishi wa habari hapa nchini, pia mjadala ulenge kutambua na kuthamini kivitendo si kinadhalia thamani ya waandishi wa habari katika taifa hili ili kujua mustakabali wa waandishi wa habari wa Tanzania. </p><p>Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.</p><p><br /></p><p>Imetolewa kwenye gazeti la Tanzania Daima Toleo la januari 19,2010</p><p>unaweza kuisoma kwa kuki <a href="http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=12281">click hapa</a> </p><p>kazi njema.<br /></p></div>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-70374816961727736722010-01-14T07:27:00.000-08:002010-01-14T07:32:14.473-08:00Grants for investigative reporters to attend Global Investigative Journalism Conference 2010 at Geneva, Switzerland.Jamani tunaendelea kuwaltea link ambazo mnaweza kunufaika<br /><br />ebu jisomee mwenyewe kwa <a href="http://www.gijc2010.ch/en/grants">kugonga hapa</a><br />Imetolewa na Uongozi<br />Kagera Press ClubKagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-31551584135737849852010-01-14T07:23:00.000-08:002010-01-14T07:27:21.788-08:00Wanaotaka kujitosa kwenye tuzo za CNNNdugu<br />Napenda kuwajulisha kwamba wale wote wanataka kushiriki katika tuzo za CNN muda unakaribia kwisha.<br /><br />wenye kazi zao na maelezo zaidi ebu <a href="http://www.cnn.com/africanawards">fungua hapa</a><br /><br />au soma maelezo haya hapa chini(not edited)<br /><br />2010 CNN MultiChoice African Journalist Awards>> CNN International and MultiChoice recently launched the CNN> MultiChoice African Journalist 2010 Awards.>> The winners will be announced at a gala ceremony to be held in> Kampala, Uganda in May 2010.>> John-Allan Namu, from Kenya, was awarded the top prize at the CNN> MultiChoice African Journalist 2009 Awards ceremony. Namu, reporter> for Kenya Television Network, won for his stories "In the shadow of> the Mungiki" and "Inside Story: Scars and Sufurias," which were chosen> from among 1665 entries from 38 nations across the African continent.>> Over the past fifteen years, the competition has grown in size and> status. In 2009, it attracted entries from 38 African countries and a> Highlights Programme of the ceremony, held in Durban, South Africa,> was broadcast in 44 African countries, on the Africa Channel in the> US, OBE TV and Southern Africa Direct in the UK and RTP Africa.>> Awards categories:>> - Arts & Culture Award> - Digital Journalism Award> - Economics & Business Award> - Environment Award> - Free Press Africa Award> - The HIV/AIDS Reporting Award> - Mohamed Amin Photographic Award> - MSD Health & Medical Award> - Print General News Award> - Radio General News Award> - Sport Award> - Television Features Award> - Television News Bulletin Award> - Tourism Award> - Francophone General News Awards> - Portuguese Language General News Award> - From these category winners, the judges choose the overall winner -> the CNN MultiChoice African Journalist 2010.>> Finalists in the 2010 competition will participate in a four day> finalists' programme that will include a media forum and networking> opportunities with senior journalists, editors, business leaders and> media owners from across the continent, culminating in a gala awards> ceremony in May, 2010.>> All finalists receive a cash prize and each category winner also> receives a laptop and printer. The CNN MultiChoice African Journalist> 2010 will receive an additional cash prize and a trip to the CNN> Center in Atlanta.>> The competition is open to African nationals who are professional> journalists including freelancers across print, television, internet,> photographic and radio.>> Full details on how to enter can be found by logging on at> <a href="http://www.cnn.com/africanawards" target="_blank">www.cnn.com/africanawards</a>.>> The closing date for entries is 28 January 2010. There will not be any> extensions of this closing date, and entries received after this date> may be disqualified.>> The judging will take place in March 2010.>> All entries should be broadcast or published during January 2009 -> December 2009.Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-73309222645072370562010-01-07T03:50:00.000-08:002010-01-07T04:15:29.959-08:00Waandishi tuweni makini kipindi cha lawama kwetu kimekwisha anza !<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg5VrdBj_sRum1CuKkhqpuWaN0yxf1-rMC5tmeTpTDPnqs1IpkQOQfXU6vD0kmqt617nNEc8lc5XZwzQ3JiGecorEfUGpbFt0AliWnFNh14GsYk43hlJQo-K1pQUKZBl2KwPcYUFD8X_Em4/s1600-h/CCM+BUKOBA+MJINI.jpg"><img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5423966628613172306" style="DISPLAY: block; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 126px; CURSOR: hand; HEIGHT: 200px; TEXT-ALIGN: center" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg5VrdBj_sRum1CuKkhqpuWaN0yxf1-rMC5tmeTpTDPnqs1IpkQOQfXU6vD0kmqt617nNEc8lc5XZwzQ3JiGecorEfUGpbFt0AliWnFNh14GsYk43hlJQo-K1pQUKZBl2KwPcYUFD8X_Em4/s200/CCM+BUKOBA+MJINI.jpg" border="0" /></a><br /><div></div><br /><div><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhaVXj74cor2-0KypuOuzvlJgb0HCJHqyThBl_y857xRgIYHErkHVhI83t3huZbNasoBhk5FACmDqu-3unesKfS7pzP-w85umLXoEuM5RG79aSo4bcL_nxgsRHaJ2tZN-DACJaxG8PlPVFY/s1600-h/CCM+BUKOBA+MJINI.jpg"></a><span style="color:#3366ff;"><span style="font-size:180%;">Wa</span></span><span style="font-size:180%;color:#3366ff;"><span style="color:#3366ff;">pendwa</span> wanachama wa Kagera Press Club wanaofuatilia taarifa kama hizi kupitia blog hii na hasa waliko nje ya Manispaa ya Bukoba tunawaomba na kuwatahadharisha sana kuwa makini katika shuguli zao za kila siku za kuhabarisha jamii hasa katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.<br /><br />mfano tazama taarifa kama hii hapo juu iliyotolewa na CCM Bukoba mjini,ni taarifa nzuri lakini yenye kuitaji uangalizi mkubwa wakati wa kuandika stori kutoka kwenye taarifa hiyo kwa kutazama taratibu za kupata wagombea wa vyama,mapenzi ya watu nk.<br /><br />Tumeweka taarifa hii si kwa lengo la kuibeza bali kuwalewesha kwamba kupitia taarifa hii waandishi wanaweza kulisha wananchi umbea,au kutumika kama kasuku tu.<br /><br />Hata hivyo tunachukua nafasi hii kuwapongeza redio Kasibante Fm ya mjini bukoba kwa jinsi ilivyotanagaza habari hiyo (ya jana saa 3:00 usiku) kutoka kwenye taarifa hii na kuwaomba waandishi wengine ambao ni wanachama wa Kagera Press Club kuiga mfano wa uhariri uliofanywa na wahariri wa redio hiyo.<br /><br />Tofauti na hapo waandishi tutaendelea kuwa 'makasuku' tu na kutumiwa na vyama badala ya kuchambua hoja kuhusu yale wanayotueleza na mwisho wake ni kupotosha jamii ambayo inakosa umakini katika kuchagua viongozi wanaowafaa na wenye kuwaletea tija.<br /><br />Imetolewa na Uongozi<br />Kagera Press Club<br />Januari 7,2009</span></div>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-15622823266058663912010-01-05T03:06:00.000-08:002010-01-05T03:22:07.261-08:00'Dili' la mafunzo huko Geneva Uswizi kuhusu Habari za Uchunguzi<span style="font-size:180%;">Wapenzi Wanachama wa Kagera Press Club na wadu wengine wa habari,</span><br /><span style="font-size:180%;"></span><br /><span style="font-size:180%;">Kama unataka kujiongeza ujuzi wa namna ya kuandika habari za uchunguzi unaweza kuomba kuhudhuria mafunzo yatakayofanyika Geneva Uswizi hapo April mwaka huu.</span><br /><span style="font-size:180%;"></span><br /><span style="font-size:180%;">Kama una nia </span><a href="http://www.blogger.com/www.gijc2010.ch/en/grants"><span style="font-size:180%;">soma hapa</span></a> <span style="font-size:180%;">kujua namna ya kuomba kuhudhuria kwa kufadhiliwa</span><br /><span style="font-size:180%;"></span><br /><span style="font-size:180%;">kazi kwenu</span><br /><span style="font-size:180%;"></span><br /><span style="font-size:180%;">Imetolewa na uongozi </span><br /><span style="font-size:180%;">Kagera Press Club</span>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-62427880920677956472009-12-31T06:35:00.000-08:002009-12-31T06:44:52.094-08:00Kwa Heri 2009,Karibu 2010Leo mungu akipenda tutaumaliza mwaka 2009 na kuingia mwaka mpya wa 2010 saa chacha kutoka sasa.<br /><br />Hata hivyo kiutendaji mwaka 2009 ulikuwa wa mafanikio makubwa kwani wadau wa tasnia ya Habari nchini walishuhudia Kagera Press Club ikianzisha gazeti la kiswahili mapema mwezi wa pili baada ya mchakato wa takribani miaka mitano.<br /><br />Mategemo ya Kagera Press Club,wadau ni kwamba mwaka 2010 ambao ni wa uchaguzi kwa Tanzania ni mwaka mgumu sana kwa upande wa waandishi wa habari kwani ni mwaka ambao baadhi yao madili ya uandishi wa habari uwekwa kando katika kutekeleza majukumu yao.<br /><br />Tunachukua fursa hii kuwatahadharisha wanachama wa Kagera Press Club kuwa makini katika kutekeleza kazi zao kwa mwaka mzima tnaotarajia kuangia wa 2010.<br /><br />Tusitegemee wanataaluma wengine kutujengea taaluma yetu,MJENGA NCHI NDIYE MBOBOA NCHI kazi kwenu.<br /><br />Tunawatakia kazi njema.<br /><br />Imetolewa na<br />Mwenyekiti wa Kagera Press ClubKagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-48769340741528239072009-12-20T23:37:00.000-08:002009-12-20T23:51:48.629-08:00Mwanachama wa Kagera Press Club ashinda Tuzo za Mwandishi Bora 2009<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh1FgsyBmJCxflGR0GXTfhGMNQhcQYMxzhtEUAcGN2F7xJInF5rXYCthnQdyAU4VqgrSNYGH8541k4R8zaDhjYdrySvdwuPyLhIAHllO9iP8EzbTWi1UivD2kKgiccZTtOSUhN9BgJSnuzx/s1600-h/bashaya.png"><img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5417590539478161586" style="DISPLAY: block; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 230px; CURSOR: hand; HEIGHT: 165px; TEXT-ALIGN: center" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh1FgsyBmJCxflGR0GXTfhGMNQhcQYMxzhtEUAcGN2F7xJInF5rXYCthnQdyAU4VqgrSNYGH8541k4R8zaDhjYdrySvdwuPyLhIAHllO9iP8EzbTWi1UivD2kKgiccZTtOSUhN9BgJSnuzx/s320/bashaya.png" border="0" /></a> <span style="color:#9999ff;">Bw Phinias Bashaya(pichani) ni mmoja wa washindi wa tuzo za mwandishi bora wa mwaka zilizoandaliwa na baraza la habari la Tanzania(MCT) na wadau wengine wa habari nchini.<br /><br />Bashaya ambaye ni mwandishi wa gazeti la Habarileo alishinda tuzo hiyo kwa upande wa jinsia kufuatia makala ya uchunguzi iliyohusu wakazi wa visiwani vilivyoko katika ziwa victoria upande wa mkoa wa kagera kufuatia kupata ruzuku kutoka mfuko wa kusaidia vyombo vya habari(tmf).<br /><br />kufuatia ushindi huo bashaya amekabidhiwa tuzo,cheti na computer ndogo katika sherehe zilizozofanyika desemba 19,2009 jijini dar na alikabidhiwa tuzo na Rais wa UTPC Bw Ken Simbaya.<br />TUTACHAPISHA HAPA MAKALA ILIYOSHINDA TUZO HIYO SIKU CHACHE ZIJAZO.<br /><br />Kujua kile kilicjojiri na wenghine walioshinda </span><a href="http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=4925"><span style="color:#9999ff;">gonga hapa</span></a><span style="color:#9999ff;"><br /><br />Uongozi wa Kagera Press Club na wanachama wengine wanatoa pongezi kwa mwanachama mwenzao kupata tuzo hiyo na wengine wanaombwa kuiga mfano wake.</span>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-39095314447055141632009-12-17T05:47:00.000-08:002009-12-17T05:50:25.831-08:00Mwandishi unaweza kutoa story yako kupitia video cheki hiiWapendwa waandishi nimetumiwa video na mtandao wa IJNT ambapo waandishi kuele marekani wanaweza kutumia picha za video kueleza ukweli wa jambo kupitia video.<br /><br />ebu <a href="http://www.youtube.com/IJNetVideo">gonga hapa</a>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-24489150938301058532009-12-17T05:20:00.000-08:002009-12-17T05:31:21.295-08:00Tuzo za Mwandishi Bora Tanzania 2009 Kagera Press Club itaambulia chochote ?<span style="color: rgb(51, 102, 255);">Wapendwa wanachma wa Kagaera Press Club pamoja na wadau wengine wanaosoma blog hii ni kuwa ile siku iliyosubiriwa sana na wadau wa habari ya kutanagzwa kwa waandishi bora wa mwaka 2009 iliyoandaliwa na </span><a style="color: rgb(51, 102, 255);" href="www.mct.or.tz">baraza la Habari Tanzania</a><span style="color: rgb(51, 102, 255);">(MCT) pamoja na vyama vingine vya waandishi na mfuko wa Tanzania Media Fund(TMF) itafanyika desemba 19,2009 katika jiji la Dar Es salaam.</span><br /><br /><span style="color: rgb(51, 102, 255);">kikubwa ni washiriki wa tuzo hizo kutoka Kagera Press Club waliowasilisha kazi zao za uchunguzi ni watano,mwanamke mmoja.</span><br /><br /><span style="color: rgb(51, 102, 255);">ngoja tusubiri kama watashinda tuzo husika.</span><br /><br /><span style="color: rgb(51, 102, 255);">tutawajulisha matokeo kupitia blog hii.</span>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-84676731783505520382009-12-17T03:39:00.000-08:002009-12-17T03:42:24.934-08:00Matokeo ya Uchunguzi wa KPC juu ya matumizi Mabaya ya Fedha Bukoba VijijiniMwaka 2008 Kagera Press Club ilifanya uchunguzi juu ya matumizi mabaya ya fedha kwa Halamshauri ya Bukoba vijijini na kubanisha mambo kadhaa.<br /><br />tumelazimika kuiweka hapa baada ya kuombwa na wadau wetu kufanya hivyo ebu <a href="file:///C:/Documents%20and%20Settings/t3455477/My%20Documents/PET%20BUKOBA.htm">gonga hapa </a>kujua kiliacobanishwa.Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-29293136438055156772009-12-17T03:32:00.000-08:002009-12-17T03:37:24.528-08:00Matokeo ya Uchunguzi wa KPC juu ya matumizi Mabaya ya Fedha Bukoba Vijijini<div class="Section1"> <p class="MsoNormal" style="text-align: center;" align="center"><b style=""><span style="background: lime none repeat scroll 0% 0%; font-size: 22pt; font-family: "Bell MT"; -moz-background-clip: -moz-initial; -moz-background-origin: -moz-initial; -moz-background-inline-policy: -moz-initial;"><o:p> </o:p></span></b></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: center;" align="center"><b style=""><span style="background: lime none repeat scroll 0% 0%; font-size: 22pt; font-family: "Bell MT"; -moz-background-clip: -moz-initial; -moz-background-origin: -moz-initial; -moz-background-inline-policy: -moz-initial;"><!--[if gte vml 1]><v:shapetype id="_x0000_t75" coordsize="21600,21600" spt="75" preferrelative="t" path="m@4@5l@4@11@9@11@9@5xe" filled="f" stroked="f"> <v:stroke joinstyle="miter"> <v:formulas> <v:f eqn="if lineDrawn pixelLineWidth 0"> <v:f eqn="sum @0 1 0"> <v:f eqn="sum 0 0 @1"> <v:f eqn="prod @2 1 2"> <v:f eqn="prod @3 21600 pixelWidth"> <v:f eqn="prod @3 21600 pixelHeight"> <v:f eqn="sum @0 0 1"> <v:f eqn="prod @6 1 2"> <v:f eqn="prod @7 21600 pixelWidth"> <v:f eqn="sum @8 21600 0"> <v:f eqn="prod @7 21600 pixelHeight"> <v:f eqn="sum @10 21600 0"> </v:formulas> <v:path extrusionok="f" gradientshapeok="t" connecttype="rect"> <o:lock ext="edit" aspectratio="t"> </v:shapetype><v:shape id="_x0000_i1025" type="#_x0000_t75" style="'width:53.25pt;" bordertopcolor="black" borderleftcolor="black" borderbottomcolor="black" borderrightcolor="black" filled="t" stroked="t" strokeweight=".5pt"> <v:fill color2="black"> <v:imagedata src="PET%20BUKOBA_files/image002.jpg" title=""> <w:bordertop type="single" width="4" space="3"> <w:borderleft type="single" width="4" space="7"> <w:borderbottom type="single" width="4" space="3"> <w:borderright type="single" width="4" space="7"> </v:shape><![endif]--><!--[if !vml]--><img src="file:///C:/Documents%20and%20Settings/t3455477/My%20Documents/PET%20BUKOBA_files/image003.jpg" shapes="_x0000_i1025" width="93" height="73" /><!--[endif]--></span></b><b style=""><span style="font-family: "Bell MT";"><o:p></o:p></span></b></p> <table class="MsoNormalTable" style="margin-left: -31.15pt; border-collapse: collapse;" border="0" cellpadding="0" cellspacing="0"> <tbody><tr style="height: 32.6pt;"> <td style="border-style: double none; border-color: black -moz-use-text-color; border-width: 1pt medium; padding: 0in 5.4pt; width: 495pt; height: 32.6pt;" valign="top" width="660"> <p class="MsoNormal" style=""><b style=""><span style="font-family: "Bell MT";">Bohari Kuu ya Mkoa, Jamhuri Road, P.O.Box 1899 Bukoba, Kagera, Tanzania. Tel/Fax<span style=""> </span>028 2220183,Mob 0754527358 , Email: </span></b><a href="mailto:presskagera@yahoo.com"><span style="font-family: "Bell MT";">presskagera@yahoo.com</span></a><b><span style="font-size: 16pt;"><o:p></o:p></span></b></p> </td> </tr> </tbody></table> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><o:p> </o:p></p> <p class="MsoTitle" style=""><span style="font-size: 20pt;">ZOEZI LA UFUATILIAJI WA FEDHA ZINAZOTOLEWA KWA AJILI YA MAENDELEO YA ELIMU YA MSINGI KATIKA WILAYA YA BUKOBA VIJIJINI<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style=""><span style="font-size: 20pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style=""><span style="font-size: 20pt;"><!--[if gte vml 1]><v:shape id="_x0000_i1026" type="#_x0000_t75" style="'width:431.25pt;height:254.25pt'" filled="t"> <v:fill color2="black"> <v:imagedata src="PET%20BUKOBA_files/image004.jpg" title=""> </v:shape><![endif]--><!--[if !vml]--><img src="file:///C:/Documents%20and%20Settings/t3455477/My%20Documents/PET%20BUKOBA_files/image005.jpg" shapes="_x0000_i1026" border="0" width="575" height="339" /><!--[endif]--><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 20pt;">Hii ni nyumba alimopanga Mwalimu Alfred Jeremiah wa Shule ya Msingi Karama kutokana na kukosa nyumba ya kuishi shuleni hapo baada ya ujenzi wa nyumba ya mwalimu chini ya mpango wa MMEM kukwama kwa sababu za ubadhilifu wa fedha.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 20pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 20pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 20pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;">YALIYOMO<span style=""> </span><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;">Utangulizi........................................................................................................ uk. 3<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;">Lengo Kuu......................................................................................................uk. 4<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;">Lengo Mahususi...........................................................................................uk. 4-5<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Madhumuni ya PETS<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Mantiki ya Zoezi<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;">Njia za Uchunguzi........................................................................................uk.5-6<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;">Matokeo ya jumla.........................................................................................uk.6-7<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Vyumba vya Madarasa/ Vifaa<span style=""> </span><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;" lang="FR">Kamati za Shule<span style=""> </span><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;" lang="FR"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;" lang="FR">Matokeo Mahsusi ya zoezi la PETS…………………………………………uk.7-15<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;" lang="FR"><span style=""> </span></span><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;" lang="FR">Udadhilifu wa fedha<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;" lang="FR"><span style=""> </span>Madaraka ya Kamati za Shule</span><span style="font-size: 12pt;" lang="FR"><span style=""> </span><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;" lang="FR"><span style=""> </span><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;">Changamoto……………………………………………………………………...uk.15-20<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;">Mapendekezo……………………………………………………………………..uk.19-22<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;">Hitimisho…………………………………………………………………………..uk 23-24<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 14pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 1.5in; text-align: left;" align="left"><u><span style="font-size: 12pt;">VIAMBATANISHO<o:p></o:p></span></u></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><span style=""> </span></span><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Mwongozo wa Uimarishaji wa Kamati za Shule za Msingi katika Mpango shirikishi, Usimamizi wa fedha na vifaa. Moduli ya pili</span><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><span style=""> </span>I<span style=""> </span><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Nakala za madodoso yaliyotumika <span style=""> </span>II<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Barua mbalimbali kutoka halmashauri zinazoelekeza matumizi ya fedha<span style=""> </span>III<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;" lang="FR">Nakala ya habari za Magazeti<span style=""> </span>IV<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;" lang="FR"><span style=""> </span><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;" lang="FR"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="" lang="FR"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="" lang="FR"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="" lang="FR"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="" lang="FR"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="" lang="FR"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: left;" align="left"><span style="" lang="FR">Utangulizi<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;" lang="FR">Taarifa hii inahusu zoezi la ufuatiliaji wa Matumizi ya fedha za Umma (PETS- Public Expenditure Tracking System) zilizopokelewa kwa ajili miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu<span style=""> </span>katika shule zilizoko wilaya ya Bukoba vijijini chini ya Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM). Zoezi hili pia lilihusu ufuatiliaji wa matumizi ya fedha kwa ajili ya kusaidia maendeleo ya wanafunzi kitaaluma zinazotolewa kupitia utaratibu wa «Capitation Grant »<span style=""> </span>kwa uwiano wa wanafunzi wa shule husika.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;" lang="FR"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;" lang="FR">Zoezi hili lilifanyika kutokana na kuwepo kwa tashwishi za matumizi mabaya ya fedha kwa ajili ya miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba zilizotolewa chini ya Mpango Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM).<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;" lang="FR">Kutokana na taarifa hizo, Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoani Kagera, kwa ufadhili wa Shrilika la Maendeleo la Uholanzi(SNV), kilimteaua Bw <span style="color: blue;">Joas Kaijage</span> ambaye ni Mwandishi wa Habari za Uchunguzi na mwanachama wa (KPC), kufanya uchunguzi wa kina kubaini ukweli wa<span style=""> </span>tashwishi hizo.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;" lang="FR">Zoezi hili lilifanyika kuanzia June 15 hadi Novemba 1, 2008 na kuhusisha shule 20 za Msingi ambazo ziko kwenye vijiji na tarafa kama inavyooneshwa kwenye jedwali hapa chini. Utafiti huu umefanywa na Bw Joas Kaijage kama mtafiti Mkuu pamoja na watafiti wasaidizi wawili.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><!--[if gte vml 1]><v:shapetype id="_x0000_t202" coordsize="21600,21600" spt="202" path="m,l,21600r21600,l21600,xe"> <v:stroke joinstyle="miter"> <v:path gradientshapeok="t" connecttype="rect"> </v:shapetype><v:shape id="_x0000_s2050" type="#_x0000_t202" style="'position:absolute;" stroked="f"> <v:fill opacity="0" color2="black"> <v:textbox inset="0,0,0,0"> <![if !mso]> <table cellpadding="0" cellspacing="0" width="100%"> <tr> <td><![endif]> <div> <table class="MsoNormalTable" border="0" cellspacing="0" cellpadding="0" style="'margin-left:5.4pt;border-collapse:collapse;mso-padding-alt:0in"> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">SHULE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KIJIJI<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KATA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">TARAFA<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">NTOMA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">BUTAHYAIBEGA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KANYANGEREKO<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR'">KYAMUTWARA<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">NYARUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">BULINDA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KANYANGEREKO<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KYAMUTWARA<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">MAIGA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">BUTAIRUKA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">MARUKU<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KYAMUTWARA<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KATOMA A<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">LUKINDO<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KATOMA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KYAMUTWARA<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KATOMA B<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KASHENGE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KATOMA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KYAMUTWARA<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR'">RUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUKOMA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUKOMA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KARAMA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">NSHESHE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">NSHESHE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">NSHESHE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">NYAKAJU<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUBALE<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">MWEMAGE A<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KIBONA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">IBWERA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR'">KATERERO<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">MWEMAGE B<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KOBONA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">IBWERA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KATERERO<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KANAZI<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KANAZI<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KATERERO<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KATERERO<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KATERERO<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KANAZI<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KATERERO<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KATERERO<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KARONGE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KARONGE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">IBWERA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KATERERO<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KAISHAZA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KIBALE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">BUHENDANGABO<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">BUGABO<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUSHAKA B<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">RUSHAKA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">BUHENDANGABO<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">BUGABO<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KALEMA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">BUSHAGALA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">BUHENDANGABO<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">BUGABO<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">NYAKATO<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">IGOMBE<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">NYAKATO<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">BUGABO<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> <tr style="'mso-yfti-lastrow:yes;height:.25in'"> <td width="108" valign="top" style="'width:81.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KAAGYA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="156" valign="top" style="'width:117.0pt;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">MUSHOZI<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="144" valign="top" style="'width:1.5in;border-top:none;border-left:"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">KAAGYA<o:p></o:p></span></p> </td> <td width="145" valign="top" style="'width:109.0pt;border:solid"> <p class="MsoTitle" style="'text-align:justify;layout-grid-mode:char'"><span lang="FR" style="'font-size:12.0pt;mso-ansi-language:FR;font-weight:normal;">BUGABO<o:p></o:p></span></p> </td> </tr> </table> <p class="MsoNormal"><o:p> </o:p></p> </div> <![if !mso]></td> </tr> </table> <![endif]></v:textbox> <w:wrap type="square" side="largest"> </v:shape><![endif]--><!--[if !vml]--><img src="file:///C:/Documents%20and%20Settings/t3455477/My%20Documents/PET%20BUKOBA_files/image006.gif" alt="Text Box: SHULE KIJIJI KATA TARAFA NTOMA BUTAHYAIBEGA KANYANGEREKO KYAMUTWARA NYARUBALE BULINDA KANYANGEREKO KYAMUTWARA MAIGA BUTAIRUKA MARUKU KYAMUTWARA KATOMA A LUKINDO KATOMA KYAMUTWARA KATOMA B KASHENGE KATOMA KYAMUTWARA RUBALE RUBALE RUBALE RUBALE RUKOMA RUKOMA RUBALE RUBALE KARAMA NSHESHE RUBALE RUBALE NSHESHE NSHESHE RUBALE RUBALE NYAKAJU RUBALE RUBALE RUBALE MWEMAGE A KIBONA IBWERA KATERERO MWEMAGE B KOBONA IBWERA KATERERO KANAZI KANAZI KATERERO KATERERO KATERERO KANAZI KATERERO KATERERO KARONGE KARONGE IBWERA KATERERO KAISHAZA KIBALE BUHENDANGABO BUGABO RUSHAKA B RUSHAKA BUHENDANGABO BUGABO KALEMA BUSHAGALA BUHENDANGABO BUGABO NYAKATO IGOMBE NYAKATO BUGABO KAAGYA MUSHOZI KAAGYA BUGABO" shapes="_x0000_s2050" align="left" width="559" height="509" hspace="12" /><!--[endif]--><span style="font-family: "Arial Narrow";"><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><b style=""><span style="font-family: "Arial Narrow";">Lengo Kuu<o:p></o:p></span></b></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";">Kuimarisha utawala bora (uwazi, uwajibikaji miongoni mwa watendaji kwa jamii, ushirikishaji wa wananchi katika kupanga, kutekeleza na kutathmini miradi ya maendeleo katika shule za msingi<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><span style=""> </span><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">Lengo mahususi <o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Zoezi hili la (PETS) lililenga kuishirikisha jamii katika mchakato wa kufuatilia mtiririko wa fedha za umma tangu zinapotolewa toka Serikali Kuu, kupitia ngazi<span style=""> </span>za kati, yaani Halmashauri<span style=""> </span>na Kata, hadi ngazi<span style=""> </span>ya chini<span style=""> </span>kwenye<span style=""> </span>Kijiji<span style=""> </span>ambako<span style=""> </span>matumizi<span style=""> </span>ya mwisho<span style=""> </span>hufanyika<span style=""> </span>katika<span style=""> </span>kutekeleza<span style=""> </span>miradi<span style=""> </span>mbalimbali kama vile kujenga vyumba vya<span style=""> </span>madarasa , zahanati, kisima cha maji,<span style=""> </span>vifaa vya darasani kama vitabu, chaki na kadhalika. Lengo<span style=""> </span>la PETS ni kuboresha<span style=""> </span>na kuongeza ushirikishwaji wa jamii katika utekelezaji<span style=""> </span>wa mipango<span style=""> </span>tarajiwa na pia kufanya ufuatiliaji ili kuhakiki iwapo utekelezaji ulifanyika kwa<span style=""> </span>uwazi na ufanisi.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kufanyika kwa zoezi hili la PETS kuna uhusiano mkubwa na MKUKUTA (Mkakati wa Kupunguza Umaskini na Kukuza Uchumi Tanzania). Katika kutekeleza nguzo tatu za Mkukuta yaani Ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini wa kipato nguzo ambayo inaunganishwa na nguzo nyingine mbili za Kuimarisha ubora wa maisha na ustawi wa jamii na Utawala bora na uwajibikaji. Ni dhairi kuwa ushirikishwaji wa jamii kama mdau mmojawapo unasisitizwa katika kupanga, kutekeleza,kufuatilia<span style=""> </span>na kutathmini<span style=""> </span>shughuli<span style=""> </span>mbalimbali za jamii ha hasa maendeleo ya Elimu ya Msingi. Ushiriki wa jamii katika mchakato huu pia ni muhimu kwa kuwa ni tafsiri mpango wa serikali wa kupeleka madaraka kwa umma kwa kukasimu mamlaka (D-by-D) ambapo mamlaka katika ngazi zote za Halmashauri ya Wilaya, Kata na vijiji yanaongezwa. Kwa hiyo pamoja na jamii kupitia kamati za Shule kushirikishwa katika mchakato wa kuainisha mahitaji na kuandaa mipango ya maendeleo katika shule zilizoko kwenye vijiji vyao, jamii inapaswa kupewa mlishonyuma na kufanya tathmini ili kujua kama kazi iliyofanyika inalingana na kiasi cha fedha kilichotumika( VALUE FOR MONEY). <o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kwa mujibu wa Kifungu cha 3.1.1 cha mwongozo wa mujukumu ya Kamati za Shule </span><i style=""><span style="font-size: 12pt;">module ya pili</span></i><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"> kilichochapishwa na Wizara ya Elimu kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa inasisitizwa kuwa ili kusogeza madaraka karibu zaidi na wananchi mamlaka za ununuzi wa vifaa na mali kwa ajili ya shule umo mikononi mwa Kamati za shule na Halmashauri za vijiji na Kamati za Mitaa. Kwa mujibu wa mwongozo huo, Halmashauri za wilaya, Miji, Manispaa na Majiji watakuwa na jukumu la kutoa ushauri, utaalam, usimamizi na kushirikiana na Kamati za shule katika kutafuta vifaa na si vinginevyo.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Hatua hii inahitaji ushirikiano wa wadau mbalimbali na<span style=""> </span>kuishirikisha jamii pana zaidi<span style=""> </span>katika<span style=""> </span>kufikia azma ya<span style=""> </span>kuongeza<span style=""> </span>kiwango cha uwazi na uwajibikaji kwa upande mmoja na<span style=""> </span>kuongeza<span style=""> </span>ufanisi<span style=""> </span>katika<span style=""> </span>utoaji huduma<span style=""> </span>zinazolengwa kwa upande mwingine.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.5in;"><span style="font-family: "Arial Narrow";">Matokeo ya utafiti huu yanakusudiwa kuboresha na kuongeza ushirikishwaji wa wananchi/jamii katika<span style=""> </span>kwa kwa kubainisha mianya ya ubadhilifu ili kuthibiti matumizi mabaya ya fedha za umma zinazotolewa kwa ajili ya maendeleo ya elimu ya msingi.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><b style=""><span style="font-family: "Arial Narrow";"><span style=""> </span></span></b><b style=""><span style="font-family: "Arial Narrow";" lang="FR">Hii itawezesha<o:p></o:p></span></b></p> <p class="MsoNormal" style="margin-left: 1in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol;"><span style="">¨<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-family: "Arial Narrow";">Kusaidia kubaini ni wapi pakacha linavuja na kwa kiwango gani ili mianya hiyo izibwe.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="margin-left: 1in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol;"><span style="">¨<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-family: "Arial Narrow";">Kuimarisha utawala bora (uwazi, uwajibikaji miongoni mwa watendaji kwa jamii, ushirikishaji wa wananchi katika kupanga, kutekeleza na kutathmini miradi ya maendeleo katika shule za msingi<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="margin-left: 1in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol;"><span style="">¨<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-family: "Arial Narrow";">Kutoa fursa kwa wadau kulinganisha iwapo kiasi cha fedha zilizotolewa zimetumika kama ilivyopangwa na kwa ufanisi wa kuridhisha.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="margin-left: 1in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol;"><span style="">¨<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-family: "Arial Narrow";">Kuhakiki iwapo matumizi ya fedha yanaonyesha au yanatoa picha ya thamani halisi ya fedha zilizotumika katika utekelezaji wa mradi husika.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="margin-left: 1in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol;"><span style="">¨<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-family: "Arial Narrow";">Ni mfumo wa kuiwezesha jamii kutambua mapungufu katika utendaji na kutoa mrejesho kwa watendaji kuhusu nini kifanyiwe maboresho katika maeneo yaliyobainishwa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">Njia za Uchunguzi (research methodology)<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Mchunguzi alitumia njia mbalimbali za kupata taarifa kulingana na maudhui ya shughuli yenyewe ambazo zilihusisha kuongea na wadau wa sekta ya Elimu kama walimu wa shule za Msingi, wajumbe wa Kamati za Shule, Maafisa wa Halmashauri ya wilaya ya Bukoba Vijijini, Wananchi wa kawaida, Wajumbe wa Kamati za TASAF na Wazabuni wakiwamo Watoaji wa Huduma mbalimbali zinazohusiana na Maendeleo ya Elimu ya msingi.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Njia zilizotumika kupata taarifa mbalimbali kwa sehemu kubwa zilihusisha mahojiano ya ana kwa ana na watoa taarifa (respondents) kwa kuwa ndio njia iliyoonyesha ufanisi zaidi katika kupata taarifa za kutosha. Hata hivyo njia nyingine kama kutomia madodoso maalum zilizotumika lakini kwa utaratibu wa mchunguzi kuuliza maswali ambayo yalikuwa kwenye madodoso hayo moja kwa moja na sio utaratibu uliozoeleka wa kusambaza madodoso kwa walengwa na kuwapa nafasi ya kujaza majibu kwa wakati wao.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Njia hii ya pili iliepukwa kwa vile ilionekana haitoi nafasi kwa mtafiti kuuliza maswali ya nyongeza kwa upande mmoja lakini inatoa mwanya kwa mtu aliyeulizwa kutoa majibu kwa nia ya kukwepa kutoa majibu yanayoweza kumuwajibisha.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Njia nyingine zilizotumika ni pamoja na kutembelea maeneo ya utafiti ili kujionea hali halisi </span><span style="font-size: 12pt;">(phsical observation)</span><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"> ikiwa ni pamoja na kutizama nyaraka mbalimbali </span><span style="font-size: 12pt;">(documentary review)</span><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"> kuthibitisha taarifa zilizotolewa wakati wa mahojiano. Jumla ya watu 144 walihusika katika kutoa taarifa zilizofanikisha utafiti huu.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Hata hivyo baadhi ya watu waliohojiwa walikubali kuhojiwa wakiwakatika maeneo ya wazi wakati wengine walipendelea kutoa taarifa kwa mtafiti faraghani.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><span style=""> </span></span><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Taarifa zilizokusanywa, ndio msingi wa kuandaa taarifa hii kwa kuonyesha matokeo ya utafiti, mapendekezo na changamoto zilizojitokeza wakati wa kufanya zoezi hili. Kufuatia matokeo yaliyopatikana wakati wa uchunguzi huu wa PETS, kuna haja ya kufanya shughuli ya aina hiyo katika maeneo mengine wilayani humo na mkoa wa Kagera kwa ujumla ili kuhusisha shule nyingi zaidi na kupata maoni ya wadau mbalimbali.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">Matokeo ya Jumla</span><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">:<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Uchunguzi umeonyesha kuwa jamii iko tayari kuchangia nguvu kazi katika maendeleo ya shule zao isipokuwa ukosefu wa uwazi katika kuwapatia taarifa mbalimbali jinsi michango yao inavyotumika unavunja ari ya wananchi kuchangia miradi husika.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Imebainika kuwa shule nyingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Vijiji inakabiliwa na upungufu mkubwa wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu pamoja na vifaa mbalimbali vya kufundishia kama vitabu. Mathalan, katika shule ya Maiga ambayo ina idadi ya wanafunzi 615(Darasa la Kwanza hadi la Saba) ukiongeza wanafunzi 50 wa darasa la awali, jumla ya wanafunzi katika shule hiyo ni 665. Kwa idadi hiyo shule hiyo ilitakiwa kuwa na vyumba 14 vya madarasa badala ya 9 vilivyopo.<span style=""> </span>Upungufu huo wa vyumba vya madarasa unaifanya shule hiyo kuwa na wastani wa wanafunzi 73 wanaosomea katika chumba kimoja cha darasa hali inayoatrhiri ufundishaji. Idadi hiyo ya wanafunzi katika chumba kimoja cha darasa ni zaidi ya idadi inayotakiwa ya wanafunzi 45 kwa mujibu wa sera ya wizara.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Ukosefu huo wa vyumba vya madarasa pia unazikabili shule nyingine za msingi ambazo ni pamoja na shule ya Mwemage A ambayo imelazimika kutumia jengo lililokuwa linatumika kama bwalo ili kupata vyumba viwili vya madarasa katika hali ya kukabiliana na upungufu huo. Shule hiyo ina vyumba vitano tu vya madarasa vinavyotumiwa na wanafunzi 315 na hivyo chumba kimoja kutumika kwa wanafunzi zaidi ya 60.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Mfano mwingine wa upungufu wa vyumba vya madarasa ni katika shule ya Kanazi yenye wanafunzi 642 lakini ina vyumba sana tu vya madarasa idadi inayofanya wanafunzi zaidi ya 90 kusongamana katika chumba kimoja.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Halikadhalika upungufu wa nyumba za walimu umejitokeza katika shule ya Mwemage A yenye upungufu wa nyumba sita za walimu na Karonge Shule ya Msingi inayopungukiwa nyumba 2.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.25in; text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><span style=""> </span><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.25in; text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Wakati ni shule mbili tu za Mwemage B na Karonge miongoni mwa shule zilizotembelewa ndizo hazikuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa, ni karibu shule zote zilikuwa zinakabiliwa na upungufu mkubwa wa vitabu wa kati ya kitabu kimoja kutumika kwa wanafunzi wawili hadi 9. Shule hizo ni kama Maiga ambapo katika baadhi ya masomo kitabu kimoja hutumika kwa wanafunzi 9 hadi 40 badala ya sera ya angalau kitabu kimoja kutumiwa na wanafunzi wawili.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kwa mujibu wa matokeo ya ujumla ya utafiti huu, Shule ya Maiga pia ina upungufu mkubwa wa vyoo ambapo zaidi ya wanafunzi hutumia tundu moja la choo badala ya wanafunzi 20 hadi 25 kwa tundu moja kulingana na sera ya Taifa. Shule hiyo inatakiwa kuwa na matundu 24 ya vyoo badala ya 12 ya sasa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Ilibainika kuwa wajumbe wa Kamati za Shule hawatekelezi mujukumu yao ipasavyo si tu kutokana na baadhi yao kuwa na ufahamu duni wa mujukumu yao bali pia kutokuwa na njia za kipato ambapo baadhi yao hudiriki hushirikiana na watendaji wasiokuwa waadilifu kuhujumu maendeleo ya shule.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Ilibainika kuwa baadhi ya Watendaji wa Halmashauri wanatoa maagizo yanayodhoofisha mamlaka ya Kamati za Shule katika kusimamia matumizi ya fedha na vifaa katika shule za msingi.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Ilibainika kuwa walimu wakuu wa Shule za Msingi hawawashirikishi walimu wa kawaida katika kuainisha mahitaji ya shule kabla ya kukutana na wajumbe wa kamati ya shule kupanga matumizi ya fedha za </span><i style=""><span style="font-size: 12pt;">capitation grant.<o:p></o:p></span></i></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Imebainika kuwa kutokana na ubadhilifu wa fedha baadhi ya shule zimekwama au zimetekeleza kwa kusuasua ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu chini ya Mpango wa Mendeleo ya Elimu ya Msingi </span><i style=""><span style="font-size: 12pt;">MMEM.<o:p></o:p></span></i></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Imebainika kuwa fedha inayotolewa kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu hazitoshelezi na matokeo yake shule hulazimika kujenga majengo yaliyochini ya viwango.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Imebainika kuwa shule nyingi hazikaguliwi kwa wakati, hali inayotoa mwanya kwa walimu kutotekeleza mujukumu yao ikiwa ni pamoja na kusimamia matumizi ya fedha za umma na vifaa vya shule.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 8pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Ilibainika kuwa shule nyingi zinatumia vitabu vya kumbukumbu za kihasibu baada ya matumizi ya fedha kwenye shughuli husika lakini kutokana na kukosa mafunzo ya kutosha matumizi ya vitabu hivyo huonekana kama mzigo mkubwa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">MATOKEO MAHSUSI<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><i style=""><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></i></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Imebainika kuwa shule mbili za Karama na Nsheshe ambazo ziko katika kijiji cha Nsheshe, Kata na tarafa ya Rubale zimeshindwa kukamilisha ujenzi wa nyumba za walimu na vyumba vya madarasa kutokana na fedha iliyokuwa imetolewa kwa kazi hiyo kutumika vibaya.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Wakati shule ya msingi Karama ilikuwa imepanga kukamilisha ujenzi wa chumba kimoja cha darasa na nyumba moja ya mwalimu, Nsheshe ilikuwa imepanga kujenga nyumba moja ya mwalimu. Shule zote hizo ziko zaidi ya kilometa 80 kutoka makao makuu ya Halmashauri ya wilaya ya Bukoba vijijini. Taarifa zinasema kuwa kutokana na umbali huo shule hizo hazitembelewi mara kwa mara na viongozi wa halmashauri na hasa wakaguzi. Mwaka 2005 shule ya Karama ilipatiwa jumla ya shilingi ml 6.7 huku ml 3.1 zikiwa ni kwa ajili ya ujenzi wa chumba cha Darasa na shilingi ml 3.6 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba moja ya mwalimu kazi ambayo haijakamilika miaka mitatu sasa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kukamilika kwa kazi hiyo ambayo pia ilitegemea mchango wa Nguvu za wananchi kungeifanya shule hiyo kuwa na upungufu wa chumba kimoja cha darasa kwa kuwa na jumla ya vyumba sita badala ya vitano vya sasa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Halikadhalika ni walimu wawili tu wanaoishi katika nyumba ya walimu shuleni hapo na wengine 3 huishi zaidi ya kilometa 8 mbali na shule hiyo. Hali hiyo huchangia walimu kushindwa kutekeleza mujukumu yao ya kufundisha na kuathiri maendeleo ya taaluma shuleni hapo kutokana na kuchelewa kufika shuleni. Hali ya mahudhurio ya walimu wanaoishi mbali na eneo la shule huwa mbaya zaidi wakati wa majira ya mvua ambapo maeneo mengi ya njia zinazoelekea shuleni kutoka eneo la Nsheshe hujaa maji.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kukwama kwa ujenzi wa shule hiyo kulitokana na shule hiyo kupoteza zaidi ya shilingi mil 3 ambazo zilikuwa zimepangwa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya ujenzi. Taarifa zilizopo zinaonyesha kuwa mwalimu huyo aliandika hundi ya malipo na kuikabidhi kwa kampuni moja ya Basinda Construction Company, ambayo haijatoa vifaa vilivyolipiwa hadi leo.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><!--[if gte vml 1]><v:shape id="_x0000_i1027" type="#_x0000_t75" style="'width:431.25pt;height:324pt'" filled="t"> <v:fill color2="black"> <v:imagedata src="PET%20BUKOBA_files/image007.jpg" title=""> </v:shape><![endif]--><!--[if !vml]--><img src="file:///C:/Documents%20and%20Settings/t3455477/My%20Documents/PET%20BUKOBA_files/image008.jpg" shapes="_x0000_i1027" border="0" width="575" height="432" /><!--[endif]--></span><span style="font-size: 12pt;"><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">Hiki ni chumba cha darasa katika shule ya msingi Karama ambacho ujenzi wake ulikwama baada ya fedha za MMEM zilizokuwa zimetolewa kutumiwa vibaya na hivyo kutopatikana kwa vifaa kama mabati, misumari na mbao ili kukamalisha shughuli hiyo.Baadhi ya watoto wa shule hiyo wanasomea chini ya mwembe baada ya kukosa mahali pa kusomea.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Hadi ujenzi wa nyumba ya mwalimu unakwama ulikuwa umefikia hatua ya linta wakati ule wa chumba cha darasa ulikuwa umefikia hatua ya kuezeka. Ni baada ya shinikizo kutoka kwa Kamati ya shule kwa uongozi wa halmashauri ya Wilaya, ndipo, mhusika mkuu( aliyekuwa mwalimu Mkuu wa shule hiyo) alipogharimia vifaa mbalimbali kwa fedha yake na kulifikisha jengo hilo hadi hatua ya kuezekwa na zaidi ya miaka 2 sasa hakuna kinachofanyika.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kutokana na kutelekezwa, vichaka vimeota ndani ya jengo hilo ambalo sambamba na chumba kimoja cha darasa kisichokamilika kutokana na matumizi mabaya ya fedha vinaonekana kama magofu katikati ya majengo mengine yaliyo katika eneo hilo.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Wakati ujenzi wa nyumba ya mwalimu ulikwama katika hatua ya hanamu, tayari chumba cha darasa kilishawekewa papi lakini mabati na misumali ndivyo havikupatikana baada ya ubadhilifu huo unajitokeza.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Matokeo yake tayari mbao zilizowekwa juu ya chumba cha darasa kwa ajili ya shughuli za kuezeka zimeanza kupinda sambamba na zile zilizotayarishwa kwa ajili ya nyumba ya walimu. Katika hali hiyo itabidi zinunuliwe mbao nnyingine na zifungwe upya endapo fedha ya mabati itapatikana na shughuli ya kuezeka majengo hayo kufanyika.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Nalo jengo la nyumba ya walimu katika shule ya Msingi Nsheshe lilikwama wakati limefikia hatua ya kuezekwa. <o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><!--[if gte vml 1]><v:shape id="_x0000_i1028" type="#_x0000_t75" style="'width:431.25pt;height:268.5pt'" filled="t"> <v:fill color2="black"> <v:imagedata src="PET%20BUKOBA_files/image009.jpg" title=""> </v:shape><![endif]--><!--[if !vml]--><img src="file:///C:/Documents%20and%20Settings/t3455477/My%20Documents/PET%20BUKOBA_files/image010.jpg" shapes="_x0000_i1028" border="0" width="575" height="358" /><!--[endif]--></span><span style="font-size: 12pt;"><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">Picha hii hapo juu inaonesha nyumba ya walimu katika shule ya msingi Nsheshe ambayo ujenzi wake ulikwama kutokana na ubadhilifu wa fedha.Kama nyumba hiyo ingekamilika ingeondoa tatizo la walimu kuishi mbali na shule na hivyo kuchelewa kufika shuleni hivyo kuathiri ufundishaji.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Taarifa zilizopatikana zinadai maafisa fulani wa halmashauri waliwaagiza walimu wakuu wa shule hizo waandike hundi za malipo kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya ujenzi katika duka lililomilikiwa na Lugaiyamu Basinda ambaye hakutoa vifaa baada ya kupokea malipo hayo. Ingawa hakuna maandishi yanayoonyesha madai ya walimu hao kuelekezwa hivyo kukiukwa kwa taratibu za manunuzi kunajenga mazingira yanayoonyesha maafisa wa Halmashauri kuhusika na upotevu huo.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kulingana na miongozo iliyopo, masuala yanayohusiana na manunuzi ya vifaa vya shule hujadiliwa na Kamati za Shule husika baada ya kuainisha mahitaji. Baada ya hatua hiyo, mtunza stoo hutembeza karatasi maalum ya kulinganisha bei (quotation) kwa wenye maduka ya vifaa vinavyohitajika.<span style=""> </span>Baada ya hapo ndipo kamati hukubaliana juu ya mtu atakayetoa vifaa hivyo kwa kuangalia mwenye bei nafuu na kisha mwalimu huandika hundi ya malipo baada ya kupokea vifaa hivyo.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Hata hivyo, Mhandisi wa Halmashauri ambaye anatakiwa aione orodha ya vifaa vilivyonunuliwa na kudhibitisha kama vimepelekwa eneo husika hakufanya hivyo kabla ya kuidhinishwa kwa malipo ya vifaa. Katika hili maafisa wa halmashauri wanaohusika na utaratibu wa kuidhinisha malipo pamoja na mwalimu mkuu wa shule zinazodai kutapeliwa vifaa vya ujenzi wanawajibika kwa hasara iliyosababishwa kwa kuwa hawakutekeleza wajibu wao kama taratibu zinavyopaswa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><!--[if gte vml 1]><v:shape id="_x0000_i1029" type="#_x0000_t75" style="'width:431.25pt;height:273pt'" filled="t"> <v:fill color2="black"> <v:imagedata src="PET%20BUKOBA_files/image011.jpg" title=""> </v:shape><![endif]--><!--[if !vml]--><img src="file:///C:/Documents%20and%20Settings/t3455477/My%20Documents/PET%20BUKOBA_files/image012.jpg" shapes="_x0000_i1029" border="0" width="575" height="364" /><!--[endif]--></span><span style="font-size: 12pt;"><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">Viwango hafifu vya majengo ya shule nyingi za msingi katika wilaya ya Bukoba vijijini vinaweza kufanya majengo hayo kuanza kuharibika baada ya muda mfupi kama inavyoonesha kwenye chumba hiki katika shule ya msingi Karama ambacho madirisha yake tayari yameanza kuharibika.Pamoja na picha hiyo ni mbao ambazo zimeanza kupinda baada ya kukaa zaidi ya miaka miwili bila kutumiwa katika ujenzi wa jengo lililokwama.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><span style=""> </span>Wajumbe wa Kamati ya Shule ya Karama wanadai ni hadi waliposhindwa kuona maendeleo ya ujenzi wa shule ndipo walipoandamana hadi ofisi ya serikali ya kijiji ili kupata maelezo na ndipo Mwalimu Mkuu alipotoa taarifa ya kutapeliwa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Hata hivyo baadhi ya nyaraka mbalimbali na taarifa zilizopatikana wakati wa zoezi hili, zinaonyesha Viongozi wa Idara ya Elimu wamekuwa wakitoa maagizo mbalimbali ambayo yanadhoofisha </span><span style="font-size: 12pt;">uwezo </span><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">na </span><span style="font-size: 12pt;">uhuru</span><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"> wa Kamati za Shule katika kutekeleza mujukumu yake. Upo ushahidi wa madai kuwa Walimu wa shule zilizotapeliwa vifaa vya ujenzi waliagizwa kununua vifaa katika Duka la Basinda na kuagizwa kuidhinisha malipo hata kabla ya kupokea vifaa kama taratibu zinavyoagiza.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Malalamiko hayo ya walimu waliotapeliwa kuwa walilazimishwa ama kuelekezwa kununua vifaa vya ujenzi kutoka kwa mfanyabiashara huyo hayana ushahidi wa maandishi. Hata hivyo kutokana na idadi kubwa ya shule zilizonunua vifaa kutoka kwa mfanyabiashara huyo hata zile ambazo hazikutapeliwa, upo ushahidi wa kimazingira kuwa shule hizo hazikununua vifaa huko kwa bahati mbaya (coincidence) bali kwa kuelekezwa. Hii inatokana na ukweli kuwa jambo hili lilijitokeza katika ununuzi wa vifaa vya ujenzi na sio katika ununuzi wa vifaa vingine vya shule kama vifaa vya kufundishia ikiwamo vitabu ambapo aghalabu shule zimenunua vifaa hivyo kutoka kwa wafanyabiashara tofautitofauti.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Hata hivyo upo ushahidi kimaandishi kuwa wakati fulani viongozi wa Idara ya Elimu katika Halmashauri hiyo wamewahi kutoa maagizo ambayo yanaashiria kukandamiza mamlaka ya kamati za shule na hata kusababisha matumizi mabaya ya fedha za umma.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Mnamo tarehe 13, Mei 2008, Afisa Elimu wa halmashauri ya Wilaya ya Bukoba aliawaandikia walimu wakuu wote wa shule za msingi wilayani humo akiwaagiza kutumia sehemu ya fedha inayotolewa kwa utaratibu wa </span><i style=""><span style="font-size: 12pt;">Capitation Grant </span></i><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">kinyume na mwongozo wa matumizi ya fedha hizo.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Barua hiyo yenye kichwa cha habari: KUGHARIMIA SCANNING YA TSM9 ZA WANAFUNZI WA DARASA LA VII na Kumb Na. BDC/E/E.5/3/VOL.6/69, inawaagiza walimu wakuu kutumia fungu la mtihani kwenye fedha ya capitation kulipia gharama za kuscan fomu zenye picha za wanafunzi wa darasa la saba kwa ajili ya mtihani wa kitaifa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Hata hivyo, barua hiyo pia inawaelekeza shughuli hiyo ifanywe na kampuni ya Benny Bazaar kwamba ni mwenye gharama nafuu dhidi ya wengine, hata bila kuainisha ni utaratibu gani umefuatwa kulinganisha bei kwa mujibu.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Sehemu ya barua hiyo inasomeka “……………</span><i style=""><span style="font-size: 12pt;">kwa kuwa shughuli hii ni nyeti, inaagizwa zoezi hili lifanywe na Kampuni moja.<span style=""> </span>Kwa kuwa Benny Bazaar ina bei nafuu dhidi ya kampuni nyingine ndiye ahusike.<o:p></o:p></span></i></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Barua hiyo iliyosainiwa na </span><span style="font-size: 12pt;">H. Batinoluho</span><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">, inaendelea kuagiza……<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><i style=""><span style="font-size: 12pt;">………………….taratibu zote za malipo zifuatwe na mzabuni awe amelipwa kabla ya Mei 31, 2008.<o:p></o:p></span></i></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><i style=""><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></i></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><i style=""><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></i></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Maagizo haya ni kinyume na mwongozo wa matumizi ya fedha za umma zinazopelekwa katika shule za msingi kwa ajili ya shughuli mbalimbali za maendeleo ya elimu kwa kuwa yanawapokonya wajumbe wa kamati za shule uhuru wa kuainisha mahitaji yao na kupendekeza huduma inayotakiwa kutolewa na mtu mwenye huduma yenye ubora na gharama nafuu.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Taarifa inaonesha kuwa maagizo ya aina hiyo yamekuwa yakitolewa kwa kipindi cha miaka miwili hivi iliyopita na walimu wa shule nyingi za msingi wamelazimika kuchukua fedha kutoka mafungu mengine ya Captation grant baada ya kuwa na fedha pungufu kwenye fungu la mtihani. Halikadhalika kutokana na mwongozo wa matumizi ya fedha kwenye miradi ya maendeleo ya elimu ya msingi kupitia utaratibu wa capitation, fungu la mtihani ambalo ni aslimia 10% ni kwa ajili ya shughuli zote za mitihani katika shule husika.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kutokana na kutumia fedha hizo kwa shinikizo kutoka Halmashauri karibia shule zote zimelazimika kutoa fedha katika maeneo mengine kama ukarabati, utawala na kadhalika na hivyo shughuli katika maeneo husika kukwama ikiwa ni pamoja na baadhi ya shule kushindwa kugharimia mitihani kwa madarasa yaliyobaki jambo linaloathiri maendeleo ya mtihani kwa kiwango kikubwa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Mathalan wakati agizo hilo linatolewa, Shule ya Msingi Mwemage A ilikuwa na shilingi 12,874.40/= katika fungu la mitihani na kwa vile fedha hiyo ilihitajika ilipwe ndio watoto waweze kufanya mitihani, shule hiyo ililazimika kuchukua kiasi cha shilingi 82,676/= kwenye fungu la ukarabati ili kugharimia scanning ya picha kwa ajili ya watahiniwa 49 wa darasa la saba kwa gharama ya shilingi 1950/= kwa kila fomu ya TSM9 yenye picha.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Shule hiyo ambayo kabla ya kumilikiwa na Serikali mwaka 1970, ilianzishwa na Kanisa la Kikatoliki mwaka 1960 na inahitaji ukarabati mkubwa ikiwa ni pamoja na kuezeka upya majengo yake.<span style=""> </span>Kwa sasa majengo ya shule hiyo yameezekwa kwa mabati aina ya asbestos ambayo yameharibika vibaya na wanafunzi hunyeshewa darasani wakati wa mvua.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">Ukichukua takwimu za watahiniwa 8548 waliofanya mtihani wa Darasa la saba mwaka huu katika wilaya ya Bukoba vijijini kwa kuzidisha na gharama ya kuscan fomu ya TSM9 moja ni sawa na 16,668,600= ambazo kampuni ya Benny Bazaar imelipwa bila hata utaratibu wa kushindanisha au kutangaza zabuni kwa mujibu wa taratibu. Taarifa zinaonyesha kuwa utaratibu wa kuwashurutisha walimu wakuu kugharimia scanning umekuwa ukifanyika kwa miaka mitatu Halmashauri hiyo ilipoanza kuscan form za TSM9 baada ya utaratibu wa zamani ambapo picha zilikuwa zinabandikwa kwenye form kuwa na matatizo ya watahiniwa kupoteza picha zao baada ya kubanduka kwenye form. Kwa hali hii wastani wa milioni 50,005,800= za capitation grant zinaweza kuwa zimetumika katika kipindi cha miaka mitatu tangu utaratibu huo wa kuzishurutisha kamati za shule ulipoanza.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Barua hiyo haikuwa ya kwanza kuandikwa kwa walimu wakuu ili kuwapatia maelezo ya namna ya kutumia fedha za shule au kuwachagulia mtu, Kampuni ya kuwasambazia bidhaa wanazozihitaji katika miradi mbalimbali ya maendeleo ya shule. <o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Barua ya Decemba 22, 2004 iliyosainiwa kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Bukoba vijijini inaitambulisha kwa walimu wakuu wote wa wilaya hiyo kuwa Kampuni ya Alpex imeruhusiwa kuendesha shughuli za uuzaji vitabu na vifaa vingine vya kielimu katika halmashauri hiyo. Kwa mujibu wa mwongozo wa usimamizi wa fedha na vifaa vya shule Kamati za Shule ndizo zenye mamlaka ya kupendekeza/kuchagua mzabuni wa kuwapatia huduma wanayohitaji baada ya kufuata taratibu zote za manunuzi na sio Viongozi wa Halmashauri kuelekeza au kupendekeza mtu au kampuni inayostahili kutoa huduma hiyo.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kimantiki sio jambo la ajabu kwa uongozi wa halmashauri hiyo kufanya utambulisho wa Kampuni zinazohitaji kupata soko la kuuza bidhaa mbalimbali kwa shule za msingi. Jambo la kushangaza kuhusu utaratibu huu ni pale ambapo utambulisho wa aina hiyo hufanywa kwa kambuni fulani pekee na wakati mwingine viongozi wa halmashauri ya wilaya kudaiwa kuwaelekeza au kuwashurutisha walimu wakuu kufanya bishara na Kampuni fulani na kuwazuia wasinunue bidhaa kutoka kwa maduka fulani ambayo kamati za Shule ziumeamua zenyewe kwa kufuata mwongozo wa matumizi ya fedha za maendeleo ya elimu ya Msingi.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Walimu waliohojiwa wanakiri kuwa pamoja na kuwa matumizi hayo ni kinyume na utaratibu uliopo, yapo maneno katika barua yenye agizo hilo ambayo yanawafanya walimu wasiwe na pingamizi lolote kutekeleza maamuzi hayo ya wakuu wao wa kazi. Mfano barua hiyo inatoa nakara kwa waratibu elimu wa kila kata kuwaagiza wahakikishe agizo hilo linatekelezwa, hali inayofanya kuchagua kuheshimu matakwa ya wakubwa wao wa kazi na kudharau muongozo wa matumizi ya fedha za shule.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Inaagizwa katika </span><i style=""><span style="font-size: 12pt;">moduli ya pili </span></i><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">ya mwongozo wa uimarishaji wa uwezo wa wajumbe wa Kamati za Shule za Msingi juu ya Mpango shirikishi, usimamizi wa fedha na vifaa Kifungu cha 3.1.2 ( Taratibu za Kumpata Mzabuni kwa Ununuzi wa Vifaa/Bidhaa/ Huduma ukurasa wa 43 kuwa:<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><i style=""><span style="font-size: 12pt;">“Utaratibu wa ununuzi wa vifaa vya shule unaokubalika na Serikali ni ule wa kutumia mzabuni. Mzabuni ni mtu binafsi, kikundi cha watu, au kampuni ambayo imeandikishwa kisheria kuuza bidhaa au vifaa na awe ameingia mkataba baina yake na shule. Muuzaji huyo awe na namba ya utambulisho kama mlipa kodi. Uchaguzi wa mzabuni wa shule utafanywa na Kamati ya Shule baada ya kuchambua sifa za vifaa na huduma inayotakiwa kutoka kwa wazabuni mbalimbali.”<o:p></o:p></span></i></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><i style=""><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></i></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Katika hili utafiti huu umebaini kuwa kama ungefanyika utaratibu wa kuwashindanisha wazabuni mbalimbali, gharama za kuscan za watahiniwa wa mtihani wa Darasa la Saba TCM9 katika ya maduka kama Church Bookshop, New Bukoba Cyber Centre, na Morden Secretarial Services zote za mjini Bukoba, gharama za kuscan form moja zingekuwa kati ya shilingi 500 hadi 1000 badala ya 1950 alizolipwa Benny Bazaar.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><!--[if gte vml 1]><v:shape id="_x0000_i1030" type="#_x0000_t75" style="'width:431.25pt;height:324pt'" filled="t"> <v:fill color2="black"> <v:imagedata src="PET%20BUKOBA_files/image013.jpg" title=""> </v:shape><![endif]--><!--[if !vml]--><img src="file:///C:/Documents%20and%20Settings/t3455477/My%20Documents/PET%20BUKOBA_files/image014.jpg" shapes="_x0000_i1030" border="0" width="575" height="432" /><!--[endif]--></span><span style="font-size: 12pt;"><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">Hili ndilo jengo la nyumba ya walimu katika shule ya Msingi Karama ambalo lilikwama kwa sababu ya matumizi mabaya ya fedha za MMEM<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Agizo lingine ni lile lililokuwa linawaelekeza walimu hao kutumia fedha za Captation kugharimia mafunzo ya walimu ambao walitakiwa kwenda kuhudhuria mafunzo kuhusiana na maboresho ya mtaala.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Hali hii inawafanya walimu na wajumbe wa kamati za shule Kwa ujumla kuamini kuwa katika halmashauri kuna mawakala wa watu wanaopendekezwa kupewa kazi ya kutoa huduma mbalimbali ikiwamo ununuzi wa vifaa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kutokana na hitilafu hii walimu wa shule zilizopoteza fedha wakati wa ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu wamedai kuwa wamekuwa wakielekezwa maduka ya kununua vifaa mbalimbali vya shule na hundi za walimu wanaokaidi maagizo hayo hucheleweshwa kuidhinishwa ama kukataliwa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kuna taarifa kuwa hivi karibuni baadhi ya walimu wameelekezwa kufanya manunuzi ya vitabu kwenye Kampuni binafsi iliyoko mjini Bukoba, tofauti na Kampuni ya MBESA BOOKS DISTRIBUTORS LTD kwa madai kuwa gharama za vitabu za Kampuni hiyo ni za juu. Baadhi ya shule hizo ni Kamuli, Butainamwa, Nsheshe na Kobunshwi ambazo zinadaiwa malimbikizo ya gharama za ununuzi wa vitabu kutoka Kampuni ya Mbesa. Kampuni hii ilipata umaarufu wakati wa mradi wa kusambaza Tusome Vitabu wa CARE, mradi uliofanikiwa sana katika maeneo mengi ya wilaya hiyo na Shule nyingi zinatumia huduma zake. <o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Mbali na shule za Nsheshe na Karama zilzizofuja fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa pamoja na nyumba za walimu kama ilivyoelezwa hapo juu, taarifa zilizopatikana wakati wa uchunguzi huu, zinataja baadhi ya shule nyingine za Buzi (tarafa ya Bugabo),Nyakabulala(Rubale),Butulage(Rubale) na Umoja(Rubale).<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Baadhi ya shule, mfano Shule ya Msingi Katerero zilipoteza fedha za ununuzi wa mbao ambapo kampuni ilipewa zabuni ya kuwapatia mbao za Pine, lakini badala yake zikatolewa Griveria ambazo sasa zimebunguliwa mbali na wahusika kuhalalisha malipo kwa bidhaa hiyo.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><span style=""> </span>Shule hizo zinadaiwa kupoteza fedha kwa kampuni ya vifaa vya ujenzi ambayo ilipokea malipo lakini ikashindwa kutoa vifaa hali iliyosababisha majengo yaliyotarajiwa kujengwa kwa fedha hiyo kukwama au kuendelea kwa kusuasua baada ya walimu waliohusika kushinikizwa kutoa fedha yao kuyakamilisha.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">VIWANGO VYA MAJENGO/VIFAA (Value for Money)<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Taarifa nyingi zilizopatikana wakati wa uchunguzi huu zinaonesha kuwa majengo mengi iwe ni vyumba vya madarasa au nyumba za walimu yako chini ya viwango. Hii inatokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na udhibiti mdogo wa vifaa vinavyonunuliwa kwa ajili ya majengo hayo na utaalam duni unaotumika katika ujenzi ambao ni pamoja kutumia vipimo hafifu hasa wakati wa uchanganyaji wa saruji ili kukamilisha jengo husika kwa fedha kidogo iliyotengwa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Mathalan, fedha inayotolewa kwa ajili ya ujenzi wa<span style=""> </span>chumba kimoja cha darasa kupitia mpango wa Maendeleo ya elimu ya Msingi(MMEM) ni shilingi ml 3.1, wakati ikiwa jengo kama hilo lingekuwa linajengwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii(TASAF), zaidi za shilingi milioni kumi zingehitajika.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Shilingi milioni 3.1 kwa ujenzi wa chumba kimoja cha darasa na shilingi milioni 3.6 kwa nyumba ya mwalimu ni viwango ambavyo vimekuwapo tangu mwaka 2001 wakati miradi ya MMEM ilipoanza lakini bei ya bidhaa mbalimbali za ujenzi imekuwa ikipanda kila kukicha.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Lakini la kushangaza ni taarifa za baadhi ya wajumbe wa Kamati za Shule kuhusika na wizi wa vifaa vya ujenzi. Hii inatokana na wengi wa wajumbe wa Kamati za Shule kuwa na kipato duni au kutokuwa na kipato kabisa lakini wanapewa kazi ya kusimamia Utendaji wa watu wanaolipwa ujira kama mafundi Ujenzi na Walimu wakuu wakati wa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ya shule.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><!--[if gte vml 1]><v:shape id="_x0000_i1031" type="#_x0000_t75" style="'width:431.25pt;height:324pt'" filled="t"> <v:fill color2="black"> <v:imagedata src="PET%20BUKOBA_files/image015.jpg" title=""> </v:shape><![endif]--><!--[if !vml]--><img src="file:///C:/Documents%20and%20Settings/t3455477/My%20Documents/PET%20BUKOBA_files/image016.jpg" shapes="_x0000_i1031" border="0" width="575" height="432" /><!--[endif]--></span><span style="font-size: 12pt;"><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">Huu ni Msingi wa jengo la chumba cha Darasa katika shule ya Msingi Karama ambalo pia halikukamilia kwa madai ya ubadhilifu.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Baadhi ya Wajumbe wa Kamati waliohojiwa, walikiri ama kuona au kushiriki katika wizi wa saruji kwa kushirikiana na mafundi ili kupata fedha za kujikimu. Wajumbe wa Kamati za shule katika maeneo yaliyotembelewa ni watu wanaojiajiri (wenye kipato duni), na hukabidhiwa jukumu la kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo wakati hawana namna yoyote ya kujikimu. Wakati wa ujenzi wa vyumba vya madarasa wajumbe wa kamati hupangiwa zamu kwa muda wa wiki mojamoja ili kuhakikisha udhibiti wa vifaa. <o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kuna Taarifa kuwa kutokana na Wajumbe wa Kamati za Shule ama kukosa umakini katika kutekeleza mujukumu yao au kwa kupatiwa fedha kidogo ya kujikimu hula njama na baadhi ya walimu wakuu wa shule kughushi sahihi za mihutasari ya vikao vya kamati ili kufanya manunuzi hewa hasa kwa kutumia fedha ya Capitation ambayo hutolewa kwa ajili ya maendeleo ya shule kwa uwiano wa idadi ya wanafunzi wa shule husika.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">CHANGAMOTO<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Zipo changamoto nyingi ambazo zinatoa mwanya wa matumizi mabaya ya fedha au kukwamisha maendeleo ya elimu ya msingi kwa ujumla katika wilaya ya Bukoba vijijini kama ifuatavyo:<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Changamoto ya kwanza ni la Kimfumo zaidi ambapo Utendaji Kazi wa walimu wakuu wa shule nyingi za msingi ambao kimsingi wanawajibika kwa Kamati za Shule katika mambo ya kiuendeshaji, hujikuta wakilazimika kuwajibika zaidi kwa wakuu wao wa kazi(Afisa Elimu, au baadhi ya maafisa waandamizi wa Idara hiyo) hata katika kutimiza maagizo ambayo yanakinzana na Maagizo ya Kamati za Shule. Walimu hufanya hivyo kwa kuhofia kupoteza ajira zao au kupata adhabu kutokana na kukaidi maagizo ya wakuu wao wa kazi na kuheshimu matakwa ya Kamati za Shule.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Shule nyingi za msingi ambazo ziko umbali wa zaidi ya kilometa 80 kutoka makao makuu ya Halmashauri ya wilaya ya Bukoba Vijijini kama Nsheshe na Karama kutembelewa mara chache sana katika kipindi kirefu na wakaguzi wa Halmashauri hiyo. Hali hiyo inaathiri utendaji wa walimu wa shule hizo kama ilivyodhihirika kwa shule hizo ambazo huchukua kipindi cha takriban miaka mitatu hadi mitano kutembelewa na maafisa wa idara hiyo.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Taarifa zilizopatikana zinaeleza kuwa hata wakati wa ujenzi wa majengo yaliyokwama katika shule ya msingi Karama, Mhandisi wa Halmashauri hakuwahi kufika kukagua hatua mbalimbali za ujenzi kama taratiubu zinavyotakiwa hadi wakaguzi wa ndani walipofika baada ya ujenzi kukwama.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Hata hivyo si kila tatizo linalotokea katika usimamizi mbovu wa matumizi ya fedha au miradi mbalimbali ya maendeleo ya shule za msingi zilizotembelewa unatokana na utendaji mbovu wa maafisa wa halmashauri au wajumbe wa Kamati za shule. <o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Halmashauri ya wilaya ya Bukoba inakabiliwa na tatizo kubwa la upungufu wa fedha za kuendesha shughuli za ukaguzi wa mara kwa mara hasa katika miradi inayofanyika kwenye maeneo yaliyoko mbali na makao makuu ya halmashauri hiyo. Baadhi ya maafisa wa idara ya ukaguzi waliohojiwa walisema kuwa shughuli za ukaguzi wa shule hazijafanyika kwa kipindi cha miezi mitatu sasa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Tatizo jingine ni kwamba walimu wanaosimamia maazimio ya Kamati za Shule pamoja na Wajumbe wa Kamati hizo wenyewe hawana elimu ya kutosha kuhusu majukumu yao. Kabla ya kuanza kwa mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi, wajumbe wa Kamati hizo walipewa mafunzo lakini yalikuwa ya muda mfupi kiasi kwamba wamekuwa wakishindwa kutekeleza majukumu yao kama mwongozo unavyoelekeza.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Karibia aslimia 90 ya wajumbe wa Kamati za Shule waliohojiwa wakati wa utafiti huu, walipendelea usimamizi wa shughuli za Kamati za Shule zibakie mikononi mwa wajumbe wasiokuwa walimu na walimu waendelee na majukumu yao ya kufundisha wakati ni chini ya aslimia 10 walioona vyema walimu waendelee kutekeleza majukumu ya kamati hizo kama ilivyo sasa. Hii inatokana na taarifa zilizopatikana kwa kutumia madodoso.Katika swali namba 9 (a) na (b) wajumbe wa Kamati za Shule walitakiwa kutoa maoni ikiwa ni vyema walimu ambao majukumu yao ya kimsingi ni kufundisha waendelee kuwamo katika Kamati za Shule ili hali muda wao wa kuwa darasani unapungua kwa sababu ya shulghuli za Kamati. Swali hili ambalo pia lilikuwa linatoa nafasi ya kupendekeza nini kifanyike ili kufidia vipindi vinavyopotea kutokana na walimu kuwa katika shughuli za Kamati, ni miongoni mwa maswali yaliyolenga kupata maoni kama wajumbe wa Kamati za Shule wanaotokana na jamii wanashiriki kikamilifu katika kudhibiti na kusimamia matumizi ya fedha za umma badala ya kazi hiyo kuachiwa walimu kama ilivyobainika.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Baadhi ya wajumbe wa Kamati za Shule wasiokuwa walimu walionekana kutokuwa na taarifa muhimu za maendeleo ya miradi mbalimbali inayotekelezwa katika shule zao na kusisitiza kila wakati kuwa mwenye taarifa fulani, mfano idadi ya mifuko ya saruji iliyotumika katika ujenzi wa jengo fulani ni Mwalimu Mkuu au Mtunza stoo. Hali hii ilijitokeza wakati wajumbe wa kamati za Ujenzi ndio waliuokuwa wanapaswa kusimamia vifaa vya ujenzi wakati miradi husika inaendelea.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Wajumbe waliohojiwa walipendelekeza wapewe mafunzo zaidi ya usimamizi wa Uendeshaji wa shughuli za Kamati. <o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Pia imebainika kuwa fedha inayotolewa kwa miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa haitoshelezi mahitaji na badala yake miradi hiyo hutekelezwa chini ya viwango au kususua na hasa kutokana na kwamba ari ya wananchi kuchangia maendeleo yake ni ndogo kutokana na kwamba mara nyingi miradi hiyo hupangwa kutoka juu na sio chini.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Watu waliohojiwa walishauri kuwa badala ya kutenga shilingi 3.1 za ujenzi wa chumba cha darasa na shilingi ml 3.6 za nyumba ya mwalimu ambazo hazitoshi kufanya kazi hiyo, ingekuwa vema zaidi fedha hiyo ikatumika kukarabati vyumba vilivyoko katika hali mbaya au kujenga mojawapo ya majengo hayo badala ya kujenga majengo yote na kushindwa kuyakamilisha kwa wakati mmoja kutokana na uhaba wa fedha.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.25in; text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Hata hivyo ilibainika kuwa miradi yote ya ujenzi iliyotekelezwa chini ya TASAF au World Vision ilikamilika kwa viwango na kwa muda uliopangwa si kutokana na usimamizi wake tu bali na kwamba huibuliwa na wananchi nap engine kupigiwa kura kutokana na umuhimu wa mradi husika na hivyo ari ya wananchi kuchangia maendeleo yake huwa ni ya kiwango kikubwa. Kwa hiyo katika maeneo mengi yaliyotembelewa na hata wiyala ya Bukoba vijijini kwa ujumla imeonekana kuwa wananchi wa maeneo hayo wana ari ndogo ya kuchangia miradi hiyo kwa kuwa wanaona kwa mfano si kipaumbele kujenga chumba kipya cha darasa au nyumba ya mwalimu wakati wanafunzi hawana madawati ya kutosha na nakadhalika. <o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.25in; text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><!--[if gte vml 1]><v:shape id="_x0000_i1032" type="#_x0000_t75" style="'width:431.25pt;height:324pt'" filled="t"> <v:fill color2="black"> <v:imagedata src="PET%20BUKOBA_files/image017.jpg" title=""> </v:shape><![endif]--><!--[if !vml]--><img src="file:///C:/Documents%20and%20Settings/t3455477/My%20Documents/PET%20BUKOBA_files/image018.jpg" shapes="_x0000_i1032" border="0" width="575" height="432" /><!--[endif]--></span><span style="font-size: 18pt;"><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 18pt;"><span style=""> </span></span><span style="font-size: 12pt;">Hii ni picha ya choo inayotumiwa na familia inayoishi katika nyumba ambamo Mwalimu Alfred Jeremiah anapanga.Kama wananchi wangeshirikishwa katika kuamua miradi ipi ipewe kipaumbele katika maendeleo ya elimu ya msingi basi ingepanga kutekeleza miradi kwa lengo la kuwaondolea walimu adha kama inayompata mwalimu huyu.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.25in; text-align: justify;"><span style="font-size: 18pt;"><span style=""> </span><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><span style=""> </span><!--[if gte vml 1]><v:shape id="_x0000_i1033" type="#_x0000_t75" style="'width:431.25pt;height:324pt'" filled="t"> <v:fill color2="black"> <v:imagedata src="PET%20BUKOBA_files/image019.jpg" title=""> </v:shape><![endif]--><!--[if !vml]--><img src="file:///C:/Documents%20and%20Settings/t3455477/My%20Documents/PET%20BUKOBA_files/image020.jpg" shapes="_x0000_i1033" border="0" width="575" height="432" /><!--[endif]--></span><span style="font-size: 12pt;"><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><span style=""> </span>MALIWATO (bafu)<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">Hii nayo ni picha ya Bafu inayotumiwa na familia inayoishi katika nyumba ambamo Mwalimu Alfred Jeremiah anapanga.Kama wananchi wangeshirikishwa katika kuamua miradi ipi ipewe kipaumbele katika maendeleo ya elimu ya msingi basi ingepanga kutekeleza miradi kwa lengo la kuwaondolea walimu adha kama inayompata mwalimu huyu.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kutokana na hali iliyoelezwa hapo juu baadhi ya shule kwa mfano, zinapangiwa kujenga nyumba za walimu wakati nyumba zilizoko hazina walimu wanaoishi humo. Baadhi ya shule hizo ni kama Nyakato ambako kuna nyumba moja isiyokuwa na walimu wanaoishi. Kwa mfano zipo taarifa kuwa moja kati ya nyumba 2 za walimu katika shule ya Msingi shule Kitunga iliyoko Kata ya Butelankuzi inakaliwa na Mwalimu wa Sekondari na nyingine Afisa Mtendaji wa Kijiji baada ya kukaa bila walimu wanaoishi shuleni hapo. Jambo hili la walimu kutopendelea kuishi katika nyumba za walimu zilizojengwa maeneo ya shule ni moja ya sababu ya wananchi wengi wilaya ya Bukoba vijijini kuwa na ari ndogo ya kuchangia ujenzi wa nyumba hizo ambazo matokeo yake hazitumiki.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Halikadhalika ilibainika kuwa kwa kuwa miradi ya ujenzi inayotekelezwa kwenye shule husika huchukuliwa na baadhi ya wanasiasa kama sera na kipimo cha kujinadi wakati wa kuomba kura kwenye uchaguzi unaofuata, hakuna kiongozi yeyote anayeweza kukubali mapendekezo ya kutumia fedha za ujenzi wa chumba cha darasa au nyumba ya mwalimu kwa kazi tofauti hata kama kwa kufanya hivyo kuna lenga matumizi yenye tija.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Baadhi ya watu walio na uhusiano na miradi iliyokuwa ikitekelezwa chini ya mpango wa World Vision wanasema kuwa hata malipo kwa watu wanaotoa vifaa vya ujenzi kwa ajili ya miradi yake hutakiwa kutoa vifaa vilivyoagizwa kwa kuandikiwa LPO na malipo hufanyika baada ya vifaa kufikishwa kwa mnunuzi tofauti na ilivyojitokeza kwenye shule zilizotapeliwa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Hata hivyo wanashangaa kwa kuwa Shule za Msingi ni taasisi za Serikali na haiwezekani mfanyabiashara yeyote akatapeli vifaa vya shule halafu asichukuliwe hatua za kisheria!<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Miradi yote ya World Vison iliyotekelezwa katika shule za Mwemage B, Maiga, Kaishaza B na Kalema ni mfano wa kuigwa na miradi mingine katika kusukuma maendeleo ya shule.Hii inajidhihirisha hata katika mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa chini ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF ambayo ilikamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Karibia asilimia 90 ya shule za msingi katika maeneo yaliyotembewa zimekuwa na kiwango kikubwa cha wanafunzi wanaofaulu kwenda shule za sekondari. Hata hivyo hali hiyo haimaanishi kuongezeka kwa kiwango cha elimu.<span style=""> </span>Hii inatokana na ukweli kuwa idadi kubwa ya wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza hushinda kwa alama za chini na kusajiliwa katika shule za sekondari za kata ambazo nyingi zake hazina vifaa vya kufundishia sambamba na walimu.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Maeneo mengi ya vijijini hayana maduka ya kuuza vifaa vinavyotakiwa na hata wakiwa navyo wengi wao hawawezi kutoa nyaraka mbalimbali zinazohitajika kisheria kwa ajili ya kumbukumbu za kihasibu.<span style=""> </span>Mathalani kuna wafanyabiashara wawili tu wanaouza vifaa vya ujenzi katika kata ya Rubale zilipo shule za Karama na Nsheshe. Ni maduka haya tu ambayo yanaweza kutumika kutoa vifaa vya ujenzi na kutoa stakabadhi muhimu zinazohitajika endapo shule hizo zingeamua kuchukua vifaa vya ujenzi katika eneo hilo badala ya kulazimika kununua vifaa Mjini Bukoba kutokana na maduka mengi ya vijiji kutokuwa na bidhaa za kutosha au kutokuwa na nyaraka muhimu ikiwamo stakabadhi zinazohitajika kwa ajili taratibu za kihasibu.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">MAPENDEKEZO:<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Baada ya changamoto zilizoainishwa, taarifa zilizopatikana zinaashiria mapendekezo yafuatayo:<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kuna haja ya kuwa na mafunzo zaidi kwa wajumbe wa Kamati za Shule ili kufanikisha utekelezaji wa Majukumu yao ambayo ni pamoja na usimamizi thabiti wa fedha zinazotolewa kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo ya elimu ya Msingi.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kuna haja ya kutenga fedha zaidi kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu badala ya viwango vya zamani vya shilingi 3.1ml na ml 3.6 ili kuhakikisha majengo yanakamilika katika muda uliopangwa na kwa viwango vya kuridhisha. Viwango hivyo vilipangwa tangu mwaka 2000 wakati wa kuanza kwa utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) kabla bei za bidhaa mbalimbali kupanda kama ilivyo sasa. Miradi inayoibuliwa chini ya Mpango wa TASAF au kutekelezwa na mashirika mengine kama World Vision mathalan hupangiwa fedha ya kutosha kwa kuwa makadirio ya bajeti hufanyika kwa kuzingatia mazingira na bei za wakati husika. <o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kuna haja ya kupambanua majukumu ya Kamati za Shule na yale ya Halmashauri kiutendaji katika kufanya maamuzi ya namna ya kutumia fedha za maendeleo ya Elimu ya Msingi ili kuepuka matumizi yasiyoendana na mwongozo wa Usimamizi wa Fedha na Vifaa vya Shule.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Uongozi wa Halmashauri unapaswa kuchunguza tuhuma za upotevu wa vifaa vya ujenzi wa madarasa na nyumba za walimu katika shule za Karama, Nsheshe na nyinginezo na kuchukua hatua ikiwa ni pamoja na kuepuka matumizi mabaya ya fedha za Umma.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Ni Muhimu walimu wakuu wa shule za Msingi pamoja na viongozi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa wanafuata miongozo katika kutumia fedha zinazotolewa kwa ajili ya maendeleo ya Elimu ya Msingi.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kuna haja ya kufanya upya tathimini ya mahitaji ya vyumba vya madarasa na nyumba za walimu katika shule mbalimbali za msingi kwenye wilaya ya Bukoba Vijijini ili kubaini ni wapi pa kupewa kipaumbele tofauti na hali ya sasa ambapo mgawanyo wa fedha kwa ajili ya shughuli hiyo hufanyika kwa matakwa ya kisiasa. Kutokana na mgawanyo wa fedha kwa ajili ya miradi ya elimu kufanyika kwa matakwa ya kisiasa, shule kama Mwemage A iliyokuwa chini ya uangalizi wa Kanisa la Kikatoliki kabla ya kumilikiwa na serikali haijawahi kupata fedha za ujenzi tangu kuanza kwa MMEM mwaka 2000 wakati wanafunzi wa shule hiyo wanatumia jengo lililokuwa linatumika kama bwalo la chakula kama darasa. Kuna taarifa kuwa tathimini ya hali ya vyumba vya madarasa na nyumba za walimu iliyofanywa na DANIDA kabla ya kuanza kwa utelekezaji wa MMEM haikubainisha mahitaji halisi ya majengo yao.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.25in; text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><span style=""> </span><!--[if gte vml 1]><v:shape id="_x0000_i1034" type="#_x0000_t75" style="'width:431.25pt;height:324pt'" filled="t"> <v:fill color2="black"> <v:imagedata src="PET%20BUKOBA_files/image021.jpg" title=""> </v:shape><![endif]--><!--[if !vml]--><img src="file:///C:/Documents%20and%20Settings/t3455477/My%20Documents/PET%20BUKOBA_files/image022.jpg" shapes="_x0000_i1034" border="0" width="575" height="432" /><!--[endif]--></span><span style="font-size: 12pt;"><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.25in; text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">Hili ni jiko katika shule ya Msingi Maiga lakini tofauti na miradi ya TASAF,miradi mingi ya ujenzi katika shule za msingi hutekelezwa kwa shinikizo la wanasiasa na siyo maamuzi ya wananchi wenyewe.Kama wangeshirikishwa wananchi wanaosishi karibu na shule ya Msingi Maiga pengine wangeamua kujenga jiko hili linalotumiwa na walimu kama kipaumbele chao.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.25in; text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Ni vyema uwepo mpango utakaohakikisha kuwa walimu ambao majukumu yao ya kimsingi ni kufundisha wanapewa nafasi ya kutimiza wajibu wao huo kwa kuwapa uwezo zaidi Wajumbe wa Kamati za Shule kuhusika badala ya majukumu yote kuachiwa walimu kama ilivyo sasa. Wakati wa utafiti huu ilibainika kuwa Wajumbe wengi wa Kamati za Shule wanaotokana na jamii hawahusiki kikamilifu katika kutekeleza majukumu yao na hivyo walimu kulemewa na mzigo au walimu wasiokuwa waaminifu kuchukua nafasi hiyo kufuja fedha na raslimali za umma bila ya wanajamii kuwa na taarifa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.25in; text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kupitia vyanzo vyake mbalimbali vya Mapato, kuna haja ya halmashauri na serikali za vijiji viweke mpango wa kugharimia chakula, viburudisho kwa wajumbe wa Kamati za Shule wanapokuwa wanatekeleza shughuli zinazohusiana na Kamati hizo ili kuondoa uwezekano wa kushawishiwa na walimu( wanaolipwa mshahara) kukiuka ama kufanya maazimio yanayolenga kufanya ubadhilifu wa fedha za umma.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.25in; text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Kuna haja ya Halmashauri ya Wilaya kufanya tathimini ya MMEM na hasa ili kubaini kiwango cha ubadhilifu unaodaiwa kufanywa katika ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu na kuwachukulia hatua za kisheria wahusika.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.25in; text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Ni vema halmashauri ya wilaya ya Bukoba iimarishe kitengo cha ukaguzi wa shule ili kuwawezesha wataalam wa idara na hiyo na Mhandisi wa Halmashauri kufanya ufuatiliaji wa karibu wa shule za msingi hususan kwa shule ambazo ziko mbali na makao makuu yake badala ya hali ya sasa ambapo baadhi ya shule huchukua kati ya miaka 3 hadi 5 kabla ya kutembelewa na maafisa hao.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.25in; text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><span style=""> </span>Kutokana na hasara iliyosababisha baadhi ya shule za msingi kutapeliwa vifaa vya ujenzi na mfanyabiashara anayedaiwa kuwa na mahusiano na baadhi ya viongozi wa Halmashauri hiyo, kuna haja ya uongozi wa juu kufanya uchunguzi wa kina juu ya madai hayo na kuwachukulia hatua wahusika.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="margin-left: 0.5in; text-align: justify; text-indent: -0.25in;"><!--[if !supportLists]--><span style="font-size: 12pt; font-family: Symbol; font-weight: normal;"><span style="">·<span style="font-family: "Times New Roman"; font-style: normal; font-variant: normal; font-weight: normal; font-size: 7pt; line-height: normal; font-size-adjust: none; font-stretch: normal;"> </span></span></span><!--[endif]--><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;">Ni vema miradi ya ujenzi mashuleni iwe inaibuliwa na mikutano ya vijiji husika ili vipaumbele viainishwe na jamii husika na kuifanya iwe na ari ya kuchangia maendeleo yake badala ya ilivyo sasa ambapo miradi mingi huibuliwa kwa misingi ya kisiasa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt; font-weight: normal;"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoTitle" style="text-align: justify;"><span style="font-size: 12pt;">HITIMISHO<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><b style=""><span style="font-family: "Arial Narrow";"><o:p> </o:p></span></b></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";"><span style=""> </span>Matokeo ya zoezi la PETS lilifanyika katika tarafa aza Rubale, Kyamtwara, Katerero na Bugabo ni mrejesho<span style=""> </span>kutoka kwa jamii jinsi wanavyoiona hali halisi ya matumizi ya fedha za umma katika sekta ya elimu katika maeneo yao. Matokeo haya<span style=""> </span>yanalenga kuwasaidia wadau<span style=""> </span>mbalimbali, kutafakari<span style=""> </span>namna<span style=""> </span>ya kuyatumia<span style=""> </span>katika kurekebisha upungufu unaotajwa na wapokeaji huduma ili kuziboresha na kutoa huduma<span style=""> </span>kwa<span style=""> </span>ufanisi zaidi. Vile vile matokeo ya zoezi hili yanakusudia kusaidia katika kuhakiki iwapo thamani ya fedha (value for money) inazingatiwa katika kuboresha utoaji wa huduma za jamii. Kwa mfano, uchunguzi unaangalia zaidi ya ujenzi wa chumba cha darasa na kusimamisha jengo kwamba vifaa vilivyotumika ni bora, thamani yake inalingana na malipo aliyopewa mkandarasi, jengo ni imara, halina nyufa, vipimo ni sahihi kadiri ya viwango vilivyoelekezwa? Mfano wa lengo hili la kubaini viwango vya bidha inayotumika katika ujenzi wa vyumba vya madarasa shuleni umejidhihirisha katika Shule ya Katerero ambapo mbao zilizotumika kwa ajili ya kuezeka chumba cha darasa chini ya MMEM ni tofauti za zile ambazo shule ilikuwa imekubaliana na mkandarasi na matokeo yake zinawahi kuoza kwa kubunguliwa. Kama ni utengenezaji wa madawati ya wanafunzi, je vipimo ni sahihi kadiri ya viwango vinavyokubalika, aina ya ubao uliotumika ni ule unaotajwa katika mkataba, uimara unaridhisha, idadi ya dawati ni sahihi na kuna utaratibu wa kupokea vifaa kama dawati zinapowasilishwa na mkandarasi ili ikibidi zikaguliwe kwa kulinganisha na masharti ya mkataba? Hii ni baadhi ya mifano tu jinsi ya kuhakiki ili kubaini iwapo ipo mianya ya pakacha kuvuja, linavujia wapi na wahusika ni akina nani.<span style=""> </span><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";"><span style=""> </span>Mtazamo wa wananchi<span style=""> </span>kuhusu zoezi la PETS<span style=""> </span>ni wa kuliunga mkono na kwamba limewafumbua<span style=""> </span>macho kuhusu haki yao<span style=""> </span>ya kupata<span style=""> </span>habari<span style=""> </span>ili<span style=""> </span>wazitumie<span style=""> </span>katika kufuatilia matumizi<span style=""> </span>ya fedha<span style=""> </span>za umma. Hata hivyo,<span style=""> </span>angalisho<span style=""> </span>lilitolewa<span style=""> </span>kuwa viongozi<span style=""> </span>na watendaji<span style=""> </span>kata nao<span style=""> </span>wabadilike<span style=""> </span>kwa kuwajibika kwa wananchi . Ilidokezwa kuwa<span style=""> </span>upeo mdogo<span style=""> </span>wa viongozi walio<span style=""> </span>wengi ngazi<span style=""> </span>ya kijiji<span style=""> </span>unachangia kwa kiasi kikubwa<span style=""> </span>kusababisha<span style=""> </span>upungufu unaojitokeza katika utendaji. <o:p></o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";">Wananchi kukubali kutoa taarifa zilizotengeneza ripoti hii ni ishara tosha kuwa wanathamini mchango wa wake katika kuboresha hali zao za maisha kupitia sekta husika.Wengine waliochangia mafanikio ni SNV ambao walimwezesha Kujenga Uwezo wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa Kagera (KPC) kuendesha zoezi hili. Kupitia taarifa hii tunapenda kuwashukuru wote<span style=""> </span>kwa michango<span style=""> </span>yao kwa namna<span style=""> </span>mbalimbali<span style=""> </span>hadi<span style=""> </span>kukamilisha<span style=""> </span>zoezi lenyewe.<span style=""> </span><o:p></o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";"><o:p> </o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style="font-family: "Arial Narrow";">Zoezi hili limehusisha shule 20 tu katika wilaya ya Bukoba vijijini ambayo ina shule 144. Tunaomba wadau mbalimbali waendelee kutoa ushirikiano wa dhati kwani zoezi la PETS ni endelevu. ASASI<span style=""> </span>na watu binafsi waliopewa mafunzo wasaidie<span style=""> </span>kuelimisha jamii<span style=""> </span>namna ya<span style=""> </span>kuendelea<span style=""> </span>kufanya<span style=""> </span>ufuatiliaji wa matumizi ya fedha za umma siyo<span style=""> </span>tu katika sekta<span style=""> </span>za elimu<span style=""> </span>bali<span style=""> </span>pia<span style=""> </span>katika<span style=""> </span>sekta<span style=""> </span>nyingine kadiri<span style=""> </span>zitakavyopendekezwa na jamii husika ili MKUKUTA na<span style=""> </span>malengo ya millennia viweze kufikiwa.<o:p></o:p></span></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style=""> </span>Mwisho wa kazi ya Uchunguzi</p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><o:p> </o:p></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><o:p> </o:p></p> <p class="MsoNormal" style="text-align: justify;"><span style=""> </span><b style=""><u><span style="font-size: 20pt; color: fuchsia;"><br /></span></u></b></p><br /></div>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-53540613423925116412009-11-06T03:58:00.000-08:002009-11-06T04:24:22.121-08:00Wanachma Tabora Press Club walipotembelea Kagera Press Club katika Picha<div><br /><br /><div><img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5400959770409988722" style="DISPLAY: block; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 214px; CURSOR: hand; HEIGHT: 320px; TEXT-ALIGN: center" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhpYMiQoCvRgOSzMexnAlMrW6U5vdHDtUmTUiyBEs-Iw41j5ZPjlDu7fQF708f1-xksw5CIbRxHYdV-q8LOrrWiGMgpDEHA8iFOkQpqpOGhxMBNgFJ8f2Tv-yrmL5yxSl-q9BaAVGMHrMUN/s320/ziara+tbora+pichani+029.jpg" border="0" /> Hapo juu ni jengo la Kiwanda cha Kukoboa kahawa cha Tanica kilichopo Mjini Bukoba ambapo wana Tabora walitembelea.</div><br /><div></div><br /><div></div><br /><div><img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5400961438902993730" style="DISPLAY: block; MARGIN: 0px auto 10px; WIDTH: 320px; CURSOR: hand; HEIGHT: 171px; TEXT-ALIGN: center" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiwD1kwNOIC4DziKcNvQbyUe024tDXFVNYkSkxbXZvrNFRT4m-rrXZVNqNwHxEesUcjPCvfOzkBHbZTz2i7m12xNn6GywoCcCwWfd7kKjnssl1ImIUcPvWKqofyMLABOVGL5x69qLq8sLdd/s320/ziara+tbora+pichani+tanica+3.jpg" border="0" /></div><br /><div>Hapa ni baadhi ya wanachma wa Tabora Press Club wakipata maele<a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjBI-2eq8QysKW3vNfktLrdOcBiKo5s6KlZ7dDunyz3O26gpYwe9co0f8_z7o90nT9znCInTA_5zLB45x5NbpKr12QKfkjEuWXqj3MH0q955tClneWJy1-kxtODQiciOoIb4xMj-iAgVxbH/s1600-h/ziara+tbora+pichani+wakipewa+zawadi+tanica.jpg"><img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5400964891374084690" style="FLOAT: right; MARGIN: 0px 0px 10px 10px; WIDTH: 320px; CURSOR: hand; HEIGHT: 214px" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjBI-2eq8QysKW3vNfktLrdOcBiKo5s6KlZ7dDunyz3O26gpYwe9co0f8_z7o90nT9znCInTA_5zLB45x5NbpKr12QKfkjEuWXqj3MH0q955tClneWJy1-kxtODQiciOoIb4xMj-iAgVxbH/s320/ziara+tbora+pichani+wakipewa+zawadi+tanica.jpg" border="0" /></a>zo kutoka Kwa uongozi wa </div><div>Tanica namna kahawa inavyoandaliwa.</div><div> </div><div>Kamera,Ninasa sauti vilitumikla kuweka kumbukumbu sawa kama inavyoonekana.</div><div> </div><div> </div><div> </div><div> </div><div> </div><div> </div><div> </div><div> </div><div> </div><br /><div></div><br /><div><br /><br /></div><br /><div></div></div>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0tag:blogger.com,1999:blog-8561979294144901567.post-1296464936570946592009-11-06T03:46:00.000-08:002009-12-31T06:47:48.895-08:00ZIARA YA WANACHAMA WA TABORA PRESS CLUB KWENYE PRESS CLUB YA KAGERA<br /><br />Katika mradi wa Balaza la Habari Tanzania (Media Council of Tanzania - (MCT) na Jumuhiya ya Vyama vya Waandishi wa Habari Tanzania (Union Of Tanzania Press Clubs), Tabora Press Club ilipata fursa ya kuitembelea Kagera Press Club iliyoko Mkoa wa Kagera. Katika Ziara hiyo pia waliambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Jumuiya hiyo Bw. Abubakar Kasan.<br /><br />Ziara hiyo ilikuwa ya siku tano iliyolenga kubadilisha uzoefu kwa kila Klabu iliwahusisha wanachama watano kutoka Tabora Presss Club ambao ni Juma Kapipi,Salma Abdul,Chuma Shomari,Swaumu Juma na Murugwa Thomas.<br /><br />Katika nasaha zake kwa wana Tabora Press na wanachama wa Kagera Press Club ,Mkurugenziwa UTPC aliviasa Vilabu vya Waandishi wa habari nchini kuwa makini katika kupanga mipango yake ya maendeleo. Amesema inabidi kuwepo ubunifu makini ikiwa lengo ni kuboresha kipato cha Wanachama wake na kukuza uchumi kwenye vilabu vyao.<br /><br />Akitoa ushauri huo Bw. Karsan alisema "hakikisheni kabla ya kupitisha mradi/miradi kwanza angalieni mapato na matumizi, tengenezani mpango endelevu wa biashara na kuhakiki kwa makini sana je, mpango huo utaleta tija na ni endelevu"<br /><br />alisema bila kufanya hivyo vilabu vitajikuta vinakuwa mufilisi au kuleta migogoro kwenye vilabu vyao na kwamba hali hiyo inaweza kuwa chanzo cha kusambaratisha umoja ambao tayari umekwisha kuwepo.<br /><br />Alifafanua kwamba Jumuiya ya Vyama vya Waandishi wa Habari (UTPC) uhai wake ni uhai wa Press Clubs nchini na kwamba hivi sasa Pemba Press Club ndiyo inayoongoza kwa sasa kwa maendeleo kuliko press club nyingine nchini.<br /><br />Karsan alito ushauri huo baada ya taarifa ya KPC iliyotolewa kwa wageni hao kufafanua kuwa miradi iliyokuwa tayari ikiiendesha na club hiyo kuwa ni pamoja na Gazeti la kila wiki liitwalo "Malengo yetu" ambalo lengo kuu ni kuhabarisha jamii ya maeneo ya kanda ya ziwa wanaishi maeneo ya vijijini ambako habari nyingi haziandikiwi au magazeti ya kitaifa kufika kwa sababu mbalimbali.<br /><br />"Pamoja na miradi mingine ambayo Kagera Press Club inakusudia kuendesha ni kuwa na Chama cha kuweka na kukopa (SACCOS) na tayari Chama hicho cha waandishi wa Habari kipo kwenye mchakato kwa kushirikiana na Wanajamii na Wadau mbali mbali wakiwemo UTPC,Shirika la Maendeleo laNetherland SNV kuanzisha Radio ya Kijamii (Community Radio) iitwayo "Omumwani Fm" jina hilo lilitokana na Wanajamii kwenye kikao cha pamoja kilichofanyika mjini Bukoba<br /><br />Kwenye ziara hiyo ya Waandishi wa Habari kutoka Tabora (Tabora Press Club) walipata fursa ya kutembelea maeneo mbali mbali katika Wilaya ya Missenyi mpakani mwa Tanzania na Uganda na kujionea Soko kuu la Kimataifa la kuuzia mazao mbali mbali hasa ndizi zitokazo katika Mkoa wa Kagera. Soko hilo ni kiungo muhimu kwa matumizi ya Nchi zinazo jumuisha Afrika Mashariki na Kati.<br /><br />Pia katika ziara hiyo walitembelea Viwanda mbali mbali, Kiwanda cha kuchapia Gazeti na Vitabu (Rumuli Printing Press) kilichoko Bunena, Kiwanda cha kukoboa Kahawa BUKOP LTD na kuonyeshwa kahawa zinavyokobolewa na walifurahia baada ya kuona kahawa zinavyokobolewa na kupata nafasi ya kukitembelea Kiwanda cha kusindika Kahawa (TANICA) na kuonyeshwa jinsi Kahawa inavyosindikwa mpaka inawekwa kwenye kopo ikiwa tayari kupelekwa kwenye masoko.<br /><br />Fursa hiyo walitembelea kwenye kijiji cha Maonesho mbali mbali ya kale kinacho simamiwa na kituo cha utalii cha Kiroyera ambacho hushughulikia Utalii katika mkoa huu na Kitaifa na kujionea vivutio vilivyopo kwenye sehemu mbali mbali zilizoko Mkoani Kagera, ikiwa baadhi Nyumba za zamani za Msonge, vifaa vitumikavyo kushikia Senene,<br /><br />(Senene ni kilaji maalum na kuheshimika sana katika nyanja mbali mbali katika tamaduni za Kihaya), vibuyu vya kuwekea pombe ya kienyeji (Rubisi) na kuona picha maalum zinazo onyesha ndege ambazo hazipatikani kwenye sehemu yoyote nchini, nyoka na vipepeo. Haya ni baadhi tu kwa vile kijiji hicho kina mambo mengi muhimu yamanufaa kwa kujione.<br /><br />Waandishi hao kutoka Tabora Press Club, walivinjali kwenye ufukwe wa Ziwa Victoria, ziwa linalo unganisha Tanzania, Uganda na Kenya na kujionea mandhari ya Ziwa hilo na viunga vya Ziwa hilo ikiwa ni pamoja na Kituo cha Nyamkazi ambako sehemu muhimu ya kufikishia samaki kutoka ziwani na kupimwa tayari kupelekwa Viwandani. Matembezi hayo pia walikiona kwa macho yao Kisiwa kiitwacho "MUSIRA" na kuitembelea Shule ya kisasa iliyoko Kata ya Ijuganyondo ya Kemebos.<br /><br />Ziara hiyo iliwachukua siku tano na mwisho Waandishi hao walihitimisha ziara yao kwa kubadilishana mawazo na uzoefu na wenyeji wao kwenye viwanja vya "Bukoba Club" iliyoko kwenye Manispaa ya Bukoba.<br /><br />Tunawashukuru sana wote waliofanikisha ziara hiyo ikiwemo wale wopte waliokubali wageni wetu kutembelea ofisi maeneo yao. <div></div><div></div><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiDbBCr2oZhTHmtvPr2tDlaSNPPtjq0hclPwUw1oyEQ1uJLTdE2ziOBTOINwGSGsOFD19XgMmVBoJt5TtlJCw_Dsb5fV1BcvHjgLuGyqDBoISMcPHxZ_NmW9xDNPHNmYg9kDNaeIjCD3inR/s1600-h/muhimu+picha.jpg"><img id="BLOGGER_PHOTO_ID_5400956600684842578" style="FLOAT: left; MARGIN: 0px 10px 10px 0px; WIDTH: 320px; CURSOR: hand; HEIGHT: 183px" alt="" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiDbBCr2oZhTHmtvPr2tDlaSNPPtjq0hclPwUw1oyEQ1uJLTdE2ziOBTOINwGSGsOFD19XgMmVBoJt5TtlJCw_Dsb5fV1BcvHjgLuGyqDBoISMcPHxZ_NmW9xDNPHNmYg9kDNaeIjCD3inR/s320/muhimu+picha.jpg" border="0" /></a><br /><div></div><div></div><div></div><div></div><div></div><div></div><div></div><div></div><div></div><div></div><div>Hapa Mkurugenzi Mtendaji wa UTPC akiteta jambo na baadhi ya viongozi wa KPC.Yupo Method Kalikila,Gilbert Makwabe na Pontian Kaiza</div><div></div><div></div><div></div><div></div><div></div><div></div><div></div><div></div><div></div><div></div><div> </div><div> </div><div> </div><div> </div><div> </div><div> </div><div> </div><div><em><span style="font-family:georgia;">Unaweza kusoma historia ya Kagera Press Club kwa</span></em> <a href="http://www.kagerapressclub.blogspot.com/">kubonyeza hapa</a></div>Kagera Press Clubhttp://www.blogger.com/profile/09188769524386003168noreply@blogger.com0