Thursday, December 31, 2009

Kwa Heri 2009,Karibu 2010

Leo mungu akipenda tutaumaliza mwaka 2009 na kuingia mwaka mpya wa 2010 saa chacha kutoka sasa.

Hata hivyo kiutendaji mwaka 2009 ulikuwa wa mafanikio makubwa kwani wadau wa tasnia ya Habari nchini walishuhudia Kagera Press Club ikianzisha gazeti la kiswahili mapema mwezi wa pili baada ya mchakato wa takribani miaka mitano.

Mategemo ya Kagera Press Club,wadau ni kwamba mwaka 2010 ambao ni wa uchaguzi kwa Tanzania ni mwaka mgumu sana kwa upande wa waandishi wa habari kwani ni mwaka ambao baadhi yao madili ya uandishi wa habari uwekwa kando katika kutekeleza majukumu yao.

Tunachukua fursa hii kuwatahadharisha wanachama wa Kagera Press Club kuwa makini katika kutekeleza kazi zao kwa mwaka mzima tnaotarajia kuangia wa 2010.

Tusitegemee wanataaluma wengine kutujengea taaluma yetu,MJENGA NCHI NDIYE MBOBOA NCHI kazi kwenu.

Tunawatakia kazi njema.

Imetolewa na
Mwenyekiti wa Kagera Press Club

No comments:

Post a Comment