Sunday, December 20, 2009

Mwanachama wa Kagera Press Club ashinda Tuzo za Mwandishi Bora 2009

Bw Phinias Bashaya(pichani) ni mmoja wa washindi wa tuzo za mwandishi bora wa mwaka zilizoandaliwa na baraza la habari la Tanzania(MCT) na wadau wengine wa habari nchini.

Bashaya ambaye ni mwandishi wa gazeti la Habarileo alishinda tuzo hiyo kwa upande wa jinsia kufuatia makala ya uchunguzi iliyohusu wakazi wa visiwani vilivyoko katika ziwa victoria upande wa mkoa wa kagera kufuatia kupata ruzuku kutoka mfuko wa kusaidia vyombo vya habari(tmf).

kufuatia ushindi huo bashaya amekabidhiwa tuzo,cheti na computer ndogo katika sherehe zilizozofanyika desemba 19,2009 jijini dar na alikabidhiwa tuzo na Rais wa UTPC Bw Ken Simbaya.
TUTACHAPISHA HAPA MAKALA ILIYOSHINDA TUZO HIYO SIKU CHACHE ZIJAZO.

Kujua kile kilicjojiri na wenghine walioshinda
gonga hapa

Uongozi wa Kagera Press Club na wanachama wengine wanatoa pongezi kwa mwanachama mwenzao kupata tuzo hiyo na wengine wanaombwa kuiga mfano wake.

No comments:

Post a Comment