Sunday, September 12, 2010

Mwandishi Raymon Owaman wa RFA na Stav TV augua gafla!

Mwandishi huyo pichani juu aliugua gafla nyumbani kwake maeneo ya Kashabo na kukimbizwa katika hospitali ya Mkoa Kagera jana jumamosi na hadi sasa amelazwa hapo.

Taarifa kutoka kwa ndugu zake ni kuwa ugonjwa unaomsumbua mwandishi huyo bado haujajulikana na kwamba alianguka na kupoteza fahamu

tutawajuza maendeleo ya mchapakazi huyo.

imetolewa na Chama cha waandishi wa Habari Mkoani Kagera(KPC)

Tuesday, September 7, 2010

Huyu 'Muhuni" kwenye msafara wa Kikwete analipwa na nani

Na Antony Mayunga

NDEGE wa aina moja huruka kwa pamoja ,ni msemo wa wahenga wetu waliotutangulia,wakimaanisha watu wa itikadi moja hufanya mambo yao kwa pamoja.

Lakini msemo huo unakuwa kinyume kwa viongozi na wanachama wa baadhi ya vyama vya siasa kutokana na kampeni za uchaguzi mkuu unaoendelea kutawaliwa na vibweka vingi .

Miongoni mwao ni kauli ya iliyotolewa na Katibu wa CCM Taifa Yusuph Makamba kuhusiana taarifa kuwa kuna baadhi ya waandishi wa Habari walizuiwa kushiriki katika msafara wa Mgombea urais kupitia CCM

Makamba alikaririwa na vyombo vya Habari akidai kuwa mtu aliyefanya hivyo ni mhuni mmoja bila kumtaja jina.

“Huyo si uamuzi wa Chama ,ili uwe wa chama lazima uafikiwe na kamati kuu,Nec au uamzi afanye Katibu mkuu,vikao hivi havikufanyika kokote na mimi
katibu mkuu sijaagiza mtu awafukuze waandishi,fuatilia vizuri habari yako utagundua kuwa yupo mhuni amekosana nao akawafukuza,”mwisho wa kumnukuu Makamba wakati akihojiwa na gazeti la kila siku la Mwananchi.

Mimi nikiwa Mwandishi wa Habari kauli hiyo inanipa mashaka juu ya umakini wa chama hicho kikongwe
kuwa na ‘mhuni’ mmoja katika timu yao ya kampeini ambaye anaweza kuamua kuwafukuza waandishi harafu wakaishia kumkandia huku akiendelea na uratibu.

Kwa mjibu wa kamusi mhuni ni Mwanamme ambaye hajaoa,kapera,mseja,mtu asiyekuwa na mahali maalum pa kuishi,mwizi ,mvunjaji
sheria,mnyang’anyi,mchopozi.

Kama maana ni hiyo Makamba anataka kuwaambia wanachama wake kuwa wamekosa watu makini mpaka wakachukua watu wa namna hiyo.


Anataka watanzania waamini kuwa Mgombea Urais wa CCM katika timu ya kampeini ya mgombea huyo kuna baadhi ya watu ambao ni wavunjaji wa sheria,wasiojulikana makazi yao.

Hivi kweli mhuni ambaye hajulikani anawezaje kupewa jukumu kubwa kama hilo na akaharibu wakaishia kudai ni mhuni mmoja bila kuchukua hatua,hii si ni danganya toto?
Kama ni kweli ‘mhuni’ huyo aliwafukuza waandishi kwenye msafara wa Kikwete ataachwa aendelee na kuratibu kazi za wasiokuwa wahuni, tutaraji nini.

Hivi watazinduka siku akimfukuza kiongozi wa CCM kwenye msafara ,na ni nani anamlipa mhuni huyo kwa kuzunguka na msafara huo?.

Inawezekanaje mhuni akapewa kitengo kizito cha kuamua mwandishi gani ashiriki msafara na nani abaki.

Je kwa kauli hiyo inamaanisha nani alimchagua na alipewaje nafasi hiyo ili hali wakijuakuwa
ni mhuni.

Nadhani ipo haja ya kutueleza jina kamili la mhuni huyo kwani Makamba alidhani kwa kusema hivyo kunatosha kuwaridhisha wananchi kuwa chama kimesikitishwa na kitendo hicho haramu.

Kwa kweli hizo ni porojo ambazo kwa zama hizi hazitakiwi kuvumiliwa maana kwa kufanya hivyo ,inatia shaka juu ya utendaji wa chama hicho kinachojigamba kila kukicha kuwa ni makini .

Maana huwezi kupata chama makini bila kuwa na watendaji makini,kwanza.

Kwanini uhuru wa waandishi uingiliwe, na kwa maslahi ya nani.

Katika katiba ya Jamhuriya Muungano ya mwaka 1977 ibara ya18(d),kifungu hiki kinampa haki mwananchi ya kupewa taarifa mbalimbali muhimu kuhusu maisha na shughuli za wananchi na pia kuhusu masuala
muhimu kwa jamii na watu wa kufanya kazi hii ni waandishi wa Habari kama waliofukuzwa.

Hivyo kwa chama makini kukaa kimya kwa mtu kuvunja katiba ibara hiyo kwa kifungu (b)na (c)kwa waandishi wa habari,inawapa mashaka watanzania wanaotaraji kufanya maamzi yao sahihi oktoba 31 .

Maana kwa kuwazuia waandishi kulikuwa na agenda ya siri isiyotakiwa kujulishwa jamii,ambayo inahitaji taarifa nani anafanya nini na wapi ,na anamkakati wa kuwafanyia nini watanzania.

Hivyo kumwachia “mhuni” rungu ya kubagua waandishi katika kampeini za Kikwete ni hatari sana.

Aidha waandishi wanaoandamana na wagombea waanchu ushabiki,kuvaa sare za vyama kwani hivyo ni kinyume na maadili ya taaluma.

Kwa kuacha hulka hizo watatenda kazi zao wakiwa huru,bila kuvalishwa nguo za chama ,na hayo ndiyo matarajio ya jamii kwa kipindi hiki ambacho
wanahitaji uchambuzi wa kina wa sera ,ilani na mikakati ya vyama vyote na wala si ushabiki.

Mwandishi anapatikana kwa simu no 0787239480.

Makala hii imetolewa kwenye gazeti Malengo Yetu Toleo la leo septemba 7,2010

Mapungufu kwa wagombea wote haya hapa !


Na Mwandishi Wetu.




Harakati za kampeni zikiwa zimepamba moto kwa wagombea wa nafasi za Urais,Ubunge na Udiwani tayari kumejitokeza mapungufu makubwa ambayo iwapo hayatarekebishwa yanaweza kuathiri mantiki nzima ya mchakato wa uchaguzi Mkuu.




Aidha imebainika kuwa hakuna chombo chochote kinachoratibu kampeini za wagombea kubaini kama wanayoyafanya kwenye kampeini zao ni sawa au wafanye marekebisho.




Uchunguzi wa gazeti hili tangu kuanza rasmi kwa kampeini hizo August 20 mwaka huu umebaini kuwa wagombea wa nafasi za udiwani na ubunge wanafanya kampeini ambazo hazitoi nafasi kwa wapiga kura kuwapima.




Hivyo hivyo wagombea nafasi za Urais wakiwemo Mutamwega Mutahywa(TLP),Hashimu Rungwe (NCCR-Mageuzi),Ibrahimu Lipumba,Willbroad Slaa(CHADEMA) na Jakaya Kikwete(CCM) ambao tayari wamezindua kampeini zao nao wamekumbwa na ‘ugonjwa huo’.




Kwa mjibu wa Uchunguzi huo ni kuwa kati ya wagombea hao hakuna hata mmoja anayetoa fursa za kuulizwa maswali au kuwataka wasikilizaji kupata ufafanuzi wa jambo lolote.




Imebanika kuwa wagombea wote wamekuwa wakihutubia tu na baada ya mkutano kuondoka huku wakiacha maswali mengi kwa wapiga kura ambao hukosa fursa ya kujua hasa mgombea alichosema .Na wanaotaka kupata ufafanuzi wa jambo lililosemwa huachwa njia panda




Mathalan,mgombea anasema kuwa iwapo atachaguliwa atahakikisha nchi inaondokana na umaskini kwa muda wa siku 100 lakini hatoi nafasi kwa wananchi kuuliza jambo juu ya hoja zake hizo.




Wapiga kura waliohojiwa walisema kuwa hawaoni haja ya kwenda kwenye mikutano ya kampeini kwani inakuwa kama wanapata hotuba zilizorekodiwa kupitia kwenye redio au Television.




Uchunguzi umebaini kuwa hata katika ratiba zao hakuna kipengele cha maswali bali kuna muda wa wagombea kuongea na wananchi na siyo kueleza sera zao.




“Wote hawataki tuwaulize maswali na wanatoi ahadi ambazo hata hazitekelezeki na wengine walishindwa kutekeleza kwa kipindi cha nyuma lakini kwa kuwa hawatoa fursa ya maswali wanatulisha sera zao tu na kuondoka”Alisema Bw Theresphory Maiko mkazi wa Rwamishenye Bukoba mjini.




Akihojiwa na gazeti hili Mwanasheria wa kituo cha Sheria na Haki za binadamu(LHRC) cha Jijini Dar Es Salaam Pasience Mlowe ni kuwa hayo ni mapungufu makubwa kikatiba.




Mlowe anasema kuwa iwapo wananchi hawapati fursa hivyo ni vigumu kuwapima wagombea kwani na kwamba hii inaweza kuathiri mchakato wa kampeini kwao wengine wanaweza kudhani ndiyo utaratibu kumbe siyo.




“Ni haki ya wananchi kikatiba,wananchi kuhoji mgombea juu ya jambo lolote alilosema kwenye mkutano au kupata ufafanuzi wa jambo hilo na kinyume chake ni makosa hivyo ni wajibu wa wananchi kudai haki hiyo” Alisema.




Kwa upande wake Rais wa Shirika la People Organization Transparency Agency(POTA) Idrisa Masalu ni kuwa hotuba zinazotolewa katika mikutano ya hadhara ni lazima wananchi wapate fursa ya kuuliza maswali.




“Hii ni hasara kwa wagombea na wapiga kura kwani bila maswali,mgombea atapataje uhakika kama wapiga kura wameelewa na mpiga kura atajuaje kama anachosema mgombea ni sahihi”Alisema Masalu na kuongeza




“Sera siyo biblia,ni lazima mgombea aulizwe na ukiona anayekataa kufanya hivyo ujue hajiamini na anaogopa kuumbuka na kwa lugha nyepesi anapiga propanganda tu aelezi sera”.




Mbali na kasoro za kutokubali kuulizwa maswali pia imeibuka tabia ya baadhi ya wagombea kutoa ahadi zisizo tekelezeka na baadhi yao kufanya kampeini za matusi badala ya kueleza sera zao.




Mathalan,katika mikutano ya kampeini za CHADEMA,CUF na CCM ambazo zimefanyika katika uwanja wa mafumbo(CHADEMA),uwanja wa Uhuru(CUF na CCM) wagombea wamebanika kujadili mienendo ya wagombea wa vyama vingine tofauti na kueleza sera zao.




Wagombea hao wanatumia dakika 28 kati ya 30 walizopewa kutukana,kueleza sifa mbaya za wagombea wa vyama vingine,kutoa taarifa zisizo na udhibitisho juu ya wenzao,uzuri wa chama chao na dakika mbili au tatu ndizo wanazotumia kueleza sera na nini watawafanyia wananchi iwapo watachaguliwa.




Aidha imegundulika pia kwenye ajenda za kujadili kwenye mikutano hiyo ya vyama zimo ajenda za kujadili wagombea wa vyama tofauti na vyao




Baadhi ya wanachama wa vyama vya siasa vya CHADEMA,CUF na CCM walihojiwa juu ya kasoro hizo katika kampeini wengi walionekana kutojua faida wala madhara yake huku wengine wakionekana kuwa nas jazba kwa kudai kuwa muuliza swali ametumwa na wapinzani wao.




Hakuna kiongozi yoyote wa Vyama hivyo ngazi ya mkoa aliyekuwa tayari kutoa ufafanuzi juu ya kasoro hizo kwa madai wao wanajua mbinu za kutumia wakati wa kampeini.




Aidha Jeshi la polisi nchini limenoa askari wake na kuwapatia mavazi na vifaa vipya kama wanavyoonekana pichani mbele mahususi kwa ajili ya kudhibiti vurugu wakati wa mchakato wa uchaguzi kwa nchi nzima


Hii ndiyo habari kubwa kwa gazeti Malengo Yetu Toleo la leo Septemba 7,2010

Thursday, August 26, 2010

Waandishi Kagera waanza ucgunguzi kwenye kata 30

Kufuatia waandishi wa Habari mkoani kagera,kupata fedha kutoka TMF sasa wameanza rasmi uchunguzi kutafuta chanzo cha wananchi katika wilaya ya Bukoba kutojiandikisha kwa wingi kupiga kura na hata wachache wanaojiandikisha kutojitokeza kwa wingi kupiga kura

Uongozi KPC unawatakia kazi njema

Monday, August 16, 2010

Tahariri ya Gazeti Malengo Yetu Toleo No 14

Kauli hizi za wanasiasa wanawake hazifai !

Wakati tunaunga mkono harakati za kutafuta usawa wa kijinsia zinazofanywa na Mh. Rais Jakaya Mrisho Kikwete, wanaharakati, wanawake wenyewe pamoja na sisi wanaume, katu hatuungi mkono fikra zinazopandikizwa sasa kuwa wanawake ni lazima kuwachagua wanawake wenzao.

Katika awamu hii ya uongozi wa nchi unaokaribia kumaliza muda wake ukiahidi kuwa lengo lake kuhusu wanawake ni kuwa wawe asilimia hamsini kwenye vyombo vya maamuzi zinaenezwa fikra potofu zinazoashiria kuchochea hisia za ubaguzi na mapambano ya wanawake dhidi ya wanaume.

Kuwa wanawake wako upande wao halikadhalika wanaume upande wao hali inayoashiria kujenga matabaka katika nchi yetu. Hali hii haiwezi kupewa nafasi na kuachiliwa iendelee kwa kuwa itakuwa inapotosha dhana nzima ya kuwawezesha wanawake na badala yake kuifedhehesha jamii nzima.

Tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu wapiga kura waelimishwe kumchagua kiongozi mwadilifu, anayeelewa matatizo yao, mwenye maono na ambaye ni sehemu ya jamii (‘anayekula na kuishi nao’kwa kila hali), lakini si kupiga debe achaguliwe fulani kwa sababu ya jinsi yake , kabila lake au dini yake.

Kwa hiyo tuwahamasishe wananchi wawachague viongozi bora na si kwa tofauti zao za kidini, kikabila wala kimaumbile. Hivyo yeyote atakayehamasisha watu kuwachagua wagombea kwa sababu ni wanawake na tofauti na yule anayepandikiza ubaguzi wa kidini au kikabila.

Kauli kama hizi ni maarufu sana katika kampeini ambazo tumeshuhudia hivi karibuni na hasa wakati wa kura za maoni za kuwatafuta wagombea wa vyama vya siasa. Mara utasikia, zinazotolewa kauli kwamba wanawake ni wenye huruma (kinyume chake wanaume ni wakatili ) wanawake wana upendo (wanaume wamejaa chuki ), wanawake ni waaminifu (wanaume si waaminifu)n.k.

Ni mtazamo wetu kuwa kama ilivyo kwa baadhi ya wanaume, hata katika kundi la wanawake kuna wasio na upendo, wasio waaminifu, wakatili na hata majambazi. Ndiyo maana tunawasihi watanzania tumchague kiongozi kwa kuangalia uwezo na zifa alizonazo mgombea kama kiongozi bora bila kutanguliza jinsi, kuwapa nafasi wanawake kuchukuliwa kuwa ni vita au uadui kati ya wanawake na wanaume.

Kama wanawake wote wataungana kuwaunga mkono wanawake wenzao tu,mwanaume gani atapita?.

Baadhi ya viongozi wa ngazi za juu wanawake walishawahi kutoa kauli za kuchefua hivi karibuni mfano, mmoja wapo ni kiongozi mmoja wa wanawake aliyekaririwa katika chombo kimoja cha habari akisema ‘’Rafiki wa mwanamke ni mwanamke’’.

Baada ya siku chache kiongozi mmoja mwanamke akiwa kwenye ziara mkoani Arusha alikaririwa akiwataka wanawake kuwa na umoja na kupendana ili waweze kuwashinda wanaume katika uchaguzi mkuu.

Haitoshi mwingine akiwa wilayani Arumeru alikaririwa na vyombo vya habari akisema, ‘’Wanawake ni jeshi kubwa wakishirikiana wanaweza kuwania na kugombea nafasi mbalimbali na kuwashinda wanaume’’.

Hofu yetu sisi Malengo Yetu ni kuwa kutokana na uwingi wa wanawake tutakuwa na bunge la wanawake, endapo kauli kama hizo za viongozi maarufu na wenye ushawishi katika jamii zitaachwa kuendelea kutolewa. Kwa hali kama hiyo lengo la 50 kwa 50 halitawezekana.

Hata hivyo hatari nyingine inayoonekana ni kuwa sasa kuna kundi moja katika jamii ambalo limejipanga kuanzisha mapambano. Sasa hofu yetu inajengeka katika ukweli kuwa ni athari gani zinazoweza kujitokeza endapo kundi linaloshambuliwa katika jamii wakati wa mapambano hayo litaamua kujihami?

Pengine sio rahisi kupata jibu. Sisi Malengo Yetu tunaamini kuwa mchakato kufikia malengo ya asilimia 50 kwa 50 za wanawake na wanaume katika nafasi za maamuzi hatuhitaji kutumia lugha za kuchochea mapambano bali kutumia uhamasishaji. Wengine katika lugha sanifu zaidi wanasema tunahitaji kutumia uzengeaji na uchechemuzi( lobbying and advocacy).

Katika matumizi mabaya ya Demokrasia ipo mifano ya maamuzi ya ovyo yaliyofikiwa na kuwa na athari mbaya kwa jamii kutokana na kutumia kigezo cha wengi wape. Kwamba hata kama wale wachache walikuwa na mawazo ya kufikiwa kwa maamuzi ya busara basi kwa kigezo cha upigaji kura wengi wenye maamuzi ya ovyo wakapata kura nyingi na uamuzi wao kuwa ndio utakaotumika kwa kigezo cha Demokrasia.

Katika maana yake halisi Demokrasia ni kama mkondo wa maji mbayo hutiririka siku zote kutoka kileleni hadi bondeni, maji hayawezi yenyewe kupanda kilele cha mlima hadi nguvu fulani itumike.

Kwa hiyo demokrasia ya wanawake kushika nafasi za uamuzi kwa asilimia 50 kwa 50 inabidi itumike kwa busara katika uchaguzi ujao. Isije kuwa kulazimisha maji kupanda kilele cha mlima. Lengo la uchaguzi si wanawake kuwashinda wanaume bali ni kushindanisha hoja, fikira,mitazamo,maono na uwezo wa kuwa kiongozi bora wa wanaume, wanawake na watoto.

Wednesday, July 21, 2010

Kagera Press Club yapata milioni 40 kutoka TMF !


Na Mwandishi Wetu.


Chama cha Waandishi mkoa wa Kagera(KPC) kimepata jumla ya shilingi milioni 40 kutoka mfuko wa kusaidia vyombo vya habari na waandishi wa habari nchini Tanzania(TMF) .


Fedha hizo zitatumiwa na wanachama wa KPC kufanya uchunguzi na kuripoti kwenye vyombo wanavyowakilisha kuhusuaiana na masuala ya uchaguzi katika majimbo ya uchaguzi ya Bukoba mjini na Bukoba vijiini.

Waandishi hao watawezeshwa kufika katika maeneo ya vijiji,kata na kuchunguza sababu zinazosababisha wananchi kutijipokeza kwa wingi kujiandisha kwenye daftari la wapiga kura na kupiga kura katika majimbo hayo.

Viongozi wa KPC ambao ni Mwenyekiti wa Bw Gilbert Makwabe na Katibu Bw Mathias Byabato walisaini mkataba kwa ajili ya kupokea fedha hizo kwenye Ofisi za Tanzania Media Fund(TMF) Jijini Dar Es Salaam Julai 21,2010 kwa niaba ya wanachama wa KPC.



Akiongea kabla ya kusaini mkataba huo Meneja wa TMF Bw Ernest Sungura aliwapongeza wanachama wa KPC kwa kufanikiwa kupata fedha hizo na kuwa KPC imepewa fedha baada ya andiko lao kukidhi vigezo na kwamba awali watapewa asilimia 82 ya fedha hizo na asilimia 18 watapewa baada ya kukamilisha mradi huo.



Akiongea kwa niaba ya KPC Mwenyekiti wake Bw Makwabe aliishukuru TMF kwa kutoa fedha hizo na kuhaidi kufanya kazi kulingana na makubaliano yaliyopo kwenye andiko lenyewe na mkataba.



Kwa mjibu wa andiko hilo wanachama hao watalazimika kufanya kazi kwa muda wa miezi sita kuanzia Agust 2010 hadi Januari 2011.

Pichani:Katibu wa Kagera Press Club Bw Mathias Byabato (Kulia) akisaini mkataba wa kupokea shilingi milioni arobaini kutoka TMF ,Katikati ni Meneja wa TMF Bw Ernest Sungura na kushoto ni Afisa wa TMF anayehusika na masuala ya ruzuku za mashirika Bw Derek Murusuri



Tuesday, March 23, 2010

Mzungu anayecharaza wananchi viboko mbaroni


Gazeti Malengo Yetu toleo la leo limeripoti kuwa yule mzungu ambasye taarifa zake ziliwekwa katika blog hii kuwa amekatwa na vyombo vya dola na kuwa juhudui za kukamatwa kwa raia huyo wa kifgeni zimefanywa na gazeti hilo.

vizuri sana

Tuesday, February 16, 2010

Gazeti Malengo Yetu litakuwa mitaani kuanzia februari 23 mwaka huu

Wapenzi wa gazeti Malengo Yetu linalotolewa na Chama cha waandishi wa Habari Mkoani Kagera(KPC) litaanza kuonekana terna mitaani kuanzia februari 23 mwaka huu siku ya jumanne likiwa na marekebisho makubwa.

Gazeti hilo lilikuwa katika marekebisho yaliyotuchukua siku kadhaa bila kuonekana mitaani

Tuongeni mkono kwa kununua gazeti hilo ukiwa Kagera,Mara,Shinyanga,Mwanza na Kigoma

Imetolewa na
Uongozi
KPC

Monday, February 1, 2010

Mwandishi wa Habari Mkongwe afariki Dunia

PRESS RELEASE

TANGAZO LA KIFO CHA MWANACHAMA WA KPC

Uongozi wa chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Kagera (KPC) unasikitika kutangaza kifo cha mwanachama wake na mmoja wa waanzilishi wa chama hicho Bw.Dominick Rweyemamu.

Bw. Rweyemamu amefariki usiku wa kuamkia leo februari 1,2010 katika hospital ya Ndolage Muleba, alipokuwa akipatiwa matibabu,

Bw. Rweyemamu aliwahi kuwa mtumishi wa serikali katika Idara ya Habari Maelezo, na baada ya kustaafu alishirikiana na waandishi wenzao mwaka 1998 wakianzisha chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Kagera.

KPC,waandishi wa Habari wote mkoa wa Kagera wamepokea kwa masikitiko taarifa za kifo hicho na inaomba ndugu,jamaa ,familia yake kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu.

Mungu alitoa, Mungu ametwaa jina lake liabudiwe, AMINA.



Imetolewa na
M. Byabato
Katibu Mtendaji
Kagera Press Club

Friday, January 29, 2010

Mkutano mkuu wa KPC ni Februari 12,2010 !

Wanachama wote wa Kagera Press Club mnatangaziwa kuwa mkutano mkuu wa mwaka uliokuwa ufanyike novemba 2009 sasa utafanyika februari 12,2010 kwenye ofisi za KPC.

Maelezo zaidi yatawekwa kwenye blog hii,kutumiwa barua na kupigiwa simu.

kwa waliooko bukoba mjini mnaweza kusoma tangazo la mkutano huo kwenye ubao wa matangazo wa KPC.

Imetolewa na
G.Makwabe
Mwenyekiti KPC

Wednesday, January 27, 2010

Ukweli kuhusu 'Mzungu' anayecharaza wananchi viboko Kagera !

Baadhi ya waandishi wakifanya mahojiano na wakazi wa kijiji cha Ijumbi wanaoishi kwa mashka.





Licha ya kucheka lakini wanacharazwa bakora,wengine ni wazee sana


Taarifa za kuwepo raia mmoja wa kigeni anayenyanyasa wananchi zimekuwa zikiripotiwa na vyombo kadhaa vya habari lakini kagera press club iliwatuma waandishi 7 wa vyombo kadhaa kuchunguza chanzo cha mgogoro huo.


kilichobainika ni hiki hapa.


Na Mwandishi wa Blogspot

KATIKA hali isiyo ya kawaida wananchi wapatao 100 wa kitongoji cha Bujenjeke kijiji cha Ruhija kata ya Ijumbi wamekuwa waakilazimika kuhamisha makazi yao porini kukwepa kipigo kutoka wanamgambo wakishirikiana na askari polisi wanaodaiwa kununuliwa na raia wa kigeni.

JESHI la polisi mkoani Kagera limejikuta likiwa katika lindi la mgogo mkubwa kwa kile kinachodaiwa kuwa kumkingia kifua raia wa kigeni anayedaiwa kuwanyanayasa wananchi na kuwalazimu kukimbia nyumba zao na kulala vichakani zaidi ya mwezi mmoja sasa.

Hayo yamebainika jana baada ya kundi la waandishi wa habari wa mkoani Kagera kulazimika kufanya ziara ya siku moja ya kwenda kuchunguza malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wananchi ya kudai kunyanyaswa na Mzungu ambaye ni anadaiwa kuwa ni raia wa nchini Uingereza.

Wakizungumza na waandishi wa habari wakazi wa kijijini hapo, walidai kuwa kwa kipindi kirefu wamekuwa wakilala na kushinda porini, kukwepa kupigwa na askari polisi wanaodaiwa kuwa katika ofisi ya Kamanda wa polisi Mkoani Kagera na wanamgambo wanaokodishwa kutoka maeneo yaasiojulikana kutokana na mavazi wanayovaa aina ya kininja.

Katika uchunguzi uliofanywa na kundi hilo la wandishi wa habari kutoka chama cha waandishi mkoa wa Kagera(Kagera Press Club) uliweza kubaini kutokuwepo kwa dhana ya utekelezaji wa kilimo kwanza kutokana na kutokuwepo hata shamba jipya linaloonesha kulimwa hivi karibuni zaidi ya zamani kukanda, huku wananchi wakidai kuwa wanashindwa kujishughulisha na kazi za kilimo kutokana na vitisho, vipigo na kuswekwa rumande kwa kubambikiziwa kesi.

Mmoja wa wakazi hao aliyejitambulisha kwa jina la Bahabti Mussa (32) alisema chanzo cha migogoro hiyo ni baaada ya mzungu huyo raia wa Uoingereza, Robert Maintland kwenda kijijini hapo, mwaka 2003 ambapo alifika na kuweka kuanza kuweka vigingi bila kuishirikisha jamii iliokuwa ikiishi hapo, na baadaye kuondoka na kurudi Uingereza.

Alisema mwaka 2008 Maintland alirejea tena nchini na baada ya siku tano kupita badhi ya wananchi walienda kumsalimia kama jirani yao, ambapo katika hali isiyo ya kawaida aliwataka waondoke katika eneo hilo.

Hata hivyo, Musa alisema kuwa walilazimika kumhoji wakiondoka wakiondoka atawalipa, ambapo aliwajibu kuwa angewalipa kuanzia sh. 100,000 hadi 350,000 na kumwambia Mussa kuwa kwa kuwa yeye ni msemaji sana angweweza kumlipa sh. 500,000 kitu ambacho wanchi hao hawakuweza kuafikiana naye, ambapo aliwaambia kuwa asiyeafikiana naye atakipata cha 'moto'.

Naye Elenestina Eleneus (74) alisema yeye kutokana na kutokuwa na nguvu anapata shida kwa kipindi kwa vurugu na vitisho vinavyofanywa askari hivyo amekuwa akishinda vichakani ili kunusuru uhai wake.

Alisema tangu uhai wake hajawahi kushuhudia hali hiyo hapa nchini hasa katika kitongoji hicho.
Alisema kwa sasa hata vifaa vyajke vya kupikia vimsombwa na askari hao na kwenda navyo kusikojulikana na hivyo kulazimika kulia kwenye majani ya migomba.

Jenipha Romwad (29) alidai Novemba 2, 2008 saa 2 asubuhi alipata kipigo kikali kutoka kwa askari akiongozwa na mwanagambo mmoja aliyemtambua kwa jina moja la James huku mzungu akivurumisha risasi kadhaa hewani ya kuwatishia ulifanya mimba yake miezi minane kutoka na kufariki, pamoja na maumivu hayo alisondekwa rumande siku mbili katika kituo cha Muleba kwa madai kuwa ni wavamizi wa ardhi ya Mzungu.

"Nikiwa na mtoto wa mwingine, nilipigwa teke la kiunoni na tumboni na huyo askari hadi kusababisha mimba yangu ya miezi minane kutoka, cha kushanga pamoja na ugonjwa wangu wala polisi pale Muleba hawakunijali hata kunipa huduma na hata sijui kichanga alikozikwa wala hata jinsi yake"alisema.

Mzee Kasenene (80) anayedaiwa kuwa alikuwa mpishi wa mmiliki wa shamba hilo aliyejulikana kwa jina la Peter Pantelakis alisema kwamba wamekuwa wakiishi kwa matesho makubwa kutoka na uwepo wa raia huyo wa kigeni.

Kwa upande wa Mzungu Robert Maintland ambaye hakuwepo katika eneo hilo akizungumza na waandishi wa habari kwa njia ya simu, alisema kuwa ardhi yake na hakuna hata raia wa Tanzania anayeishi pale kwani wote ni Warundi waliokuwa vibarua wa babu yake.

"Hakuna hata mtu wa Mtanzania nayeishi katika eneo lile, wote ni Warundi, ambao wanatabia mbaya za kubaka kuua,wakata miti ovyo"alisema.

Hata hivyo, Maintlanda alidai watu hao wanatumwa na Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini Wilson Masuilingi kuendeela kusihi karika ardhi yake ili aendelee kupata wapiga kura wengi.

Kuhusu kuwavamia na kuwapiga wananchi kulazimika kuhama makazi yao kwa kushirikiana na askari na wanamgambo anaowakodi kutoka katika maeneo yasojulikana, alikataa na kusema kuwa yeye hajui na wala hajui kufanya hivyo na kwamba hayo ni majungu anayopikiwa juu yake ya kumpaka matope.

Halikadhalika kuhusu kuwazuia wananchi kuchukua aina yoyote ya mazao kutoka kwenye msitu unaowanguka, mazao kuvuna mazao waliolima na hata kulima na kutumia maji ya Kurumiyo yalioko katika kitongoji hicho kwa matumizi ya nyumbani alidai kuwa hakuwahi na kwamba yote hayajui.

Mbunge wa Jimbo la Kusini, Masilingi akuzunguzia sakata hilo, alikiri kupokea taarifa za malalamiko ya manyanyaso waofanyiwa wananchi hao na huyo raia wa Kigeni na kufanya mikutano wa hadhara katika kitongoji hicho akiwa na Mkuu wa wilaya ya Muleba, Angelina Mabula ambapo waliagiza raia huyo wa kigeni akamatwe na kuchukuliwa hatua, lakini anashangaa hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kwake.

Alisema wananchi walitakiwa kubaki katika kitongoji chao na kuendelea na shughuli zao kama wananchi wa kawaida.

Alisema katika suala nzima ya Kitingoji hicho kutaka taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa kuingilia kati na kuchunguza mgogoro wake ambao umegubikwa na harufu za rushwa.

Alisema mzungu huyo anataka kumiliki kitongoji kizima wakazi wakazi hao waliwepo katika eneo hilo miaka mingi, na kwamba katika eneo hilo kuna mgogo wa wanafamilia baina ya mzungu na ndugu zake, mgogoro ambao wananchi hawahusiki kabisa.

Kuhusu ujenzi wa vigingi alisema kuwa unatokana na maafisa wa ardhi kula rushwa, kwani ujenzi huo haujahusisha wakazi wa eneo lile, kwa nini ijengwe vigingi wakati serikali.

Naye Kamanda wa polisi Mkoa Kagera Bw Henery salewi alipotakiwa na waandfishi wa habari kuelezea juu ya mgogoro huo unaodaiwa kuwa polisi wake ndiyo wamekuwa wakitumiwa na mzungu huyo kwenda katika kitongoji kuwatishia wananchi na kuwapora mali zao huku wenginew akiwapiga hadi kuharibiwa kwa mimba zao , alikataa kuonana hata kuzungumza na waandishi wa habari na kuwataka waandishi hao wamuulize mkuu wa mkoa ambaye hakuweza kupatikana mara moja.

"Ninashughuli nyeti, kama mtakataka kushuhudia njooni kwa Mkuu wa Mkoa, au nendeni mkaongee naye atawapa jibu"alisema licha ya waandishi wa habari kufika ofisini kwake jana saa 4. asubuhi na kuwajibu kupitia msaidizi wake kuwa tumpigie simu saa nane mchana ili aaweze kutuambia yuko wapi tuweze kuzungumza naye.

Eneo linalogombaniwa na mzungu na wananchi hao mwanzoni kabla ya uhuru lilikuwa na ukubwa wa hekari 900 na baadaye hekari zaidi ya 200 ziligawiwa kwa wananchi na kubaki hekari 741.34 ambapo ardhi hiyo ilipimwa mwaka Septemba 15, mwaka 1927 na kugawawia wananchi mwaka 1961.

vyombo vingine vilivyochapisha habari za raia huyo ni tanzania daima na Channel ten tv

Friday, January 22, 2010

Ni kweli Uchumi wa wanahabari Nchini Tanzania u mikononi mwa wahariri

Na Gordon Kalulunga

TASNIA ya habari ni taaluma kama zilivyo taaluma nyingine ingawa tofauti yake moja kubwa ni kwamba iko karibu zaidi na wananchi.

Vyombo vya habari vimekuwa vikiibua mijadala mingi kupitia makala mbalimbali. Si wote wangependa mijadala hiyo kuibuliwa kwa kuwa inawagusa.

Lakini pamoja na vyombo vya habari kuwa na nguvu hiyo, waandishi wamekuwa wakikabiliwa na matatizo mbalimbali.

Kuna matukio mengi yanayowakumba waandishi nchini na duniani kwa ujumla na hivyo wengi kuogopa kufanyiwa unyama kama walivyowahi kutendewa wenzao.

Hapa nataka kuweka wazi kuwa kuna waandishi wa habari wengi ambao wamekufa hapa nchini na vifo vyao havielezeki kutokana na ama kuuliwa kikatili au kuuliwa kibaiolojia. Lakini pia baadhi kulundikwa kwenye mahabusu za polisi kwa visingizio vya sheria.

Hali ya namna hii inawatia hofu waandishi wengi hasa yanapotokea matukio ya kutisha ya namna hii kama lile lililotokea mkoa wa Mbeya ambako mwandishi John Lubungo amekufa na kifo chake kimeacha maswali mengi yasiyo na majibu kwa wanahabari wenyewe na wadau wengine wa habari hapa nchini.

John Lubungo alikuwa Mtangazaji wa ITV; alifariki akiwa na umri wa miaka 34 siku ya Ijumaa ya Januari 25, 2008 majira ya saa 5.00 usiku akiwa anaendesha gari dogo akitokea mjini Mbeya akielekea Tunduma, wilayani Mbozi, mkoa wa Mbeya yalikoweko makazi yake.

Nikimnukuu aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Mbozi, Halima Kihemba, aliyesema kwa masikitiko: “Lubungo alikuwa mtu wa karibu sana na serikali na alipigania sana maendeleo ya mji wa Tunduma, wilaya ya Mbozi na mkoa kwa ujumla; na hapa nimetumwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile, kuweka shada la maua kama ishara ya pole kwa familia na ndugu wengine.”

Naye aliyekuwa kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya, wakati huo, Suleiman Kova, ambaye ni mdau mkubwa wa wanahabari nchini, alisema alisikitishwa sana na kifo cha John Lubungo ambapo alimtaja John Lubungo kuwa mmoja wa waandishi ambao walikuwa wakiutetea na kuutangaza mkoa wa Mbeya na Tanzania kwa ujumla.

Kwa upande wake aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoani hapa kwa kipindi hicho, Christopher Nyenyembe, alisema kuwa kifo cha mwanahabari huyo kilitokea ghafla na kilileta mshtuko mkubwa kwa taaluma ya wanahabari na wadau wote waliokuwa wakishirikiana vyema na marehemu katika uhai wake.

Si hayo tu bali hata ofisi aliyokuwa akiitumikia wakati wa uhai wake ilitoa masikitiko makubwa sana kwa kumpoteza kati ya makamanda wake wa kampuni lakini cha ajabu licha ya kusikitika kote huko likaibuka sula moja nyeti kuwa mwandishi huyo hakuwa na mkataba na kampuni hiyo!

Jambo hilo halikuwashangaza waandishi wengi bali lilisikitisha sana kutokana na kumjua vema marehemu Lubungo wakati wa uhai wake hasa uchapaji kazi wake wa muda mrefu katika chombo chake.

Sina nia ya kumwelezea binafsi ndugu yetu huyo aliyetangulia mbele ya haki lakini nia ya makala hii ni kuweka bayana mateso wayapatayo waandishi wa habari hapa nchini hasa waandishi wa mikoani.

Moja ya kero kubwa kwa waandishi hao hasa wa mikoani ni malipo kidogo wanayoyapata kutoka kwenye vyombo vyao vya habari wanavyovifanyia kazi na kutopewa mikataba kama sheria za kazi za nchi zinavyoelekeza.

Suala hilo limezua kansa ya manug’uniko kwa waandishi wa habari kutokana na kutoweza kutafutiwa ufumbuzi wala mjadala wa kitaifa jambo ambalo linatafsiriwa na baadhi yao kuwa ni kuvunja haki za binadamu na kiraia.

Mmoja wa waandishi ambao wamelaani vikali suala la mapunjo ya malipo kwa waandishi wa habari hapa nchini ni Mkurugenzi wa Chuo cha Uandishi wa Habari (MIJO) kilichoko mkoani Mbeya, Jonas Mwasumbi.

Katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima kuhusu suluhisho la malalamiko ya muda mrefu ya waandishi wa habari juu ya malipo madogo wanayoyapata kutoka kwenye vyombo vyao wanavyofanyia kazi, alisema kuwa umefika wakati wahariri wa vyombo vya habari kubadilika kifikra na kimtazamo na waandishi wenyewe kujiendeleza zaidi kitaaluma.

Mwasumbi ambaye ni mwandishi mwandamizi wa magazeti ya Serikali hapa nchini na kiongozi wa muda mrefu wa MISA na taasisi nyeti za habari alisema kuwa tatizo hilo ni kubwa na linatokana na waandishi wenyewe na baadhi ya wahariri wao.

“Malalamiko hayo yanatokana na elimu ndogo waliyonayo baadhi ya waandishi ambayo haimwezeshi mwandishi kupata ajira na baadhi hawafahamu haki zao za msingi juu ya ajira.”

“Pamoja na hilo tatizo, lingine liko kwa wahariri ambao hawana utu wala dini na kuendelea kuwanyonya waandhishi wao hasa wa mikoani huku wakiendelea kutumia kwenye magazeti yao habari za waandishi hao ambao hawawalipi ipasavyo jambo ambalo ni dhambi mbaya sana,” alisema Mwasumbi.

Mkurugenzi huyo aliendelea kueleza kwamba wahariri wa vyombo mbalimbali hapa nchini wanapaswa kubadilika na kuheshimu haki za binadamu; vilevile kwa upande wa waandishi wa habari wanapaswa kuongeza viwango vyao vya elimu ili kupambana na utandawazi na soko la ajira kwa ujumla hasa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kwa mtazamo wangu na kutokana na malalamiko ya waandishi wa habari hapa nchini ni muhimu ikaibuliwa hoja na mjadala stahiki juu ya mustakabali wa waandishi wa habari Tanzania ili kutambua dhana nzima ya utawala bora kwa viongozi wetu waliokabidhiwa dhamana na kuwawezesha waandishi wa nchi hii kukabiliana na hali mbaya ya kiuchumi inayowakabili.

Pamoja na kuibua hoja ya maslahi ya waandishi wa habari hapa nchini, pia mjadala ulenge kutambua na kuthamini kivitendo si kinadhalia thamani ya waandishi wa habari katika taifa hili ili kujua mustakabali wa waandishi wa habari wa Tanzania.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.


Imetolewa kwenye gazeti la Tanzania Daima Toleo la januari 19,2010

unaweza kuisoma kwa kuki click hapa

kazi njema.

Thursday, January 14, 2010

Grants for investigative reporters to attend Global Investigative Journalism Conference 2010 at Geneva, Switzerland.

Jamani tunaendelea kuwaltea link ambazo mnaweza kunufaika

ebu jisomee mwenyewe kwa kugonga hapa
Imetolewa na Uongozi
Kagera Press Club

Wanaotaka kujitosa kwenye tuzo za CNN

Ndugu
Napenda kuwajulisha kwamba wale wote wanataka kushiriki katika tuzo za CNN muda unakaribia kwisha.

wenye kazi zao na maelezo zaidi ebu fungua hapa

au soma maelezo haya hapa chini(not edited)

2010 CNN MultiChoice African Journalist Awards>> CNN International and MultiChoice recently launched the CNN> MultiChoice African Journalist 2010 Awards.>> The winners will be announced at a gala ceremony to be held in> Kampala, Uganda in May 2010.>> John-Allan Namu, from Kenya, was awarded the top prize at the CNN> MultiChoice African Journalist 2009 Awards ceremony. Namu, reporter> for Kenya Television Network, won for his stories "In the shadow of> the Mungiki" and "Inside Story: Scars and Sufurias," which were chosen> from among 1665 entries from 38 nations across the African continent.>> Over the past fifteen years, the competition has grown in size and> status. In 2009, it attracted entries from 38 African countries and a> Highlights Programme of the ceremony, held in Durban, South Africa,> was broadcast in 44 African countries, on the Africa Channel in the> US, OBE TV and Southern Africa Direct in the UK and RTP Africa.>> Awards categories:>> - Arts & Culture Award> - Digital Journalism Award> - Economics & Business Award> - Environment Award> - Free Press Africa Award> - The HIV/AIDS Reporting Award> - Mohamed Amin Photographic Award> - MSD Health & Medical Award> - Print General News Award> - Radio General News Award> - Sport Award> - Television Features Award> - Television News Bulletin Award> - Tourism Award> - Francophone General News Awards> - Portuguese Language General News Award> - From these category winners, the judges choose the overall winner -> the CNN MultiChoice African Journalist 2010.>> Finalists in the 2010 competition will participate in a four day> finalists' programme that will include a media forum and networking> opportunities with senior journalists, editors, business leaders and> media owners from across the continent, culminating in a gala awards> ceremony in May, 2010.>> All finalists receive a cash prize and each category winner also> receives a laptop and printer. The CNN MultiChoice African Journalist> 2010 will receive an additional cash prize and a trip to the CNN> Center in Atlanta.>> The competition is open to African nationals who are professional> journalists including freelancers across print, television, internet,> photographic and radio.>> Full details on how to enter can be found by logging on at> www.cnn.com/africanawards.>> The closing date for entries is 28 January 2010. There will not be any> extensions of this closing date, and entries received after this date> may be disqualified.>> The judging will take place in March 2010.>> All entries should be broadcast or published during January 2009 -> December 2009.

Thursday, January 7, 2010

Waandishi tuweni makini kipindi cha lawama kwetu kimekwisha anza !



Wapendwa wanachama wa Kagera Press Club wanaofuatilia taarifa kama hizi kupitia blog hii na hasa waliko nje ya Manispaa ya Bukoba tunawaomba na kuwatahadharisha sana kuwa makini katika shuguli zao za kila siku za kuhabarisha jamii hasa katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

mfano tazama taarifa kama hii hapo juu iliyotolewa na CCM Bukoba mjini,ni taarifa nzuri lakini yenye kuitaji uangalizi mkubwa wakati wa kuandika stori kutoka kwenye taarifa hiyo kwa kutazama taratibu za kupata wagombea wa vyama,mapenzi ya watu nk.

Tumeweka taarifa hii si kwa lengo la kuibeza bali kuwalewesha kwamba kupitia taarifa hii waandishi wanaweza kulisha wananchi umbea,au kutumika kama kasuku tu.

Hata hivyo tunachukua nafasi hii kuwapongeza redio Kasibante Fm ya mjini bukoba kwa jinsi ilivyotanagaza habari hiyo (ya jana saa 3:00 usiku) kutoka kwenye taarifa hii na kuwaomba waandishi wengine ambao ni wanachama wa Kagera Press Club kuiga mfano wa uhariri uliofanywa na wahariri wa redio hiyo.

Tofauti na hapo waandishi tutaendelea kuwa 'makasuku' tu na kutumiwa na vyama badala ya kuchambua hoja kuhusu yale wanayotueleza na mwisho wake ni kupotosha jamii ambayo inakosa umakini katika kuchagua viongozi wanaowafaa na wenye kuwaletea tija.

Imetolewa na Uongozi
Kagera Press Club
Januari 7,2009

Tuesday, January 5, 2010

'Dili' la mafunzo huko Geneva Uswizi kuhusu Habari za Uchunguzi

Wapenzi Wanachama wa Kagera Press Club na wadu wengine wa habari,

Kama unataka kujiongeza ujuzi wa namna ya kuandika habari za uchunguzi unaweza kuomba kuhudhuria mafunzo yatakayofanyika Geneva Uswizi hapo April mwaka huu.

Kama una nia soma hapa kujua namna ya kuomba kuhudhuria kwa kufadhiliwa

kazi kwenu

Imetolewa na uongozi
Kagera Press Club