Tuesday, February 16, 2010

Gazeti Malengo Yetu litakuwa mitaani kuanzia februari 23 mwaka huu

Wapenzi wa gazeti Malengo Yetu linalotolewa na Chama cha waandishi wa Habari Mkoani Kagera(KPC) litaanza kuonekana terna mitaani kuanzia februari 23 mwaka huu siku ya jumanne likiwa na marekebisho makubwa.

Gazeti hilo lilikuwa katika marekebisho yaliyotuchukua siku kadhaa bila kuonekana mitaani

Tuongeni mkono kwa kununua gazeti hilo ukiwa Kagera,Mara,Shinyanga,Mwanza na Kigoma

Imetolewa na
Uongozi
KPC

Monday, February 1, 2010

Mwandishi wa Habari Mkongwe afariki Dunia

PRESS RELEASE

TANGAZO LA KIFO CHA MWANACHAMA WA KPC

Uongozi wa chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Kagera (KPC) unasikitika kutangaza kifo cha mwanachama wake na mmoja wa waanzilishi wa chama hicho Bw.Dominick Rweyemamu.

Bw. Rweyemamu amefariki usiku wa kuamkia leo februari 1,2010 katika hospital ya Ndolage Muleba, alipokuwa akipatiwa matibabu,

Bw. Rweyemamu aliwahi kuwa mtumishi wa serikali katika Idara ya Habari Maelezo, na baada ya kustaafu alishirikiana na waandishi wenzao mwaka 1998 wakianzisha chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Kagera.

KPC,waandishi wa Habari wote mkoa wa Kagera wamepokea kwa masikitiko taarifa za kifo hicho na inaomba ndugu,jamaa ,familia yake kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu.

Mungu alitoa, Mungu ametwaa jina lake liabudiwe, AMINA.



Imetolewa na
M. Byabato
Katibu Mtendaji
Kagera Press Club