Monday, February 1, 2010

Mwandishi wa Habari Mkongwe afariki Dunia

PRESS RELEASE

TANGAZO LA KIFO CHA MWANACHAMA WA KPC

Uongozi wa chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Kagera (KPC) unasikitika kutangaza kifo cha mwanachama wake na mmoja wa waanzilishi wa chama hicho Bw.Dominick Rweyemamu.

Bw. Rweyemamu amefariki usiku wa kuamkia leo februari 1,2010 katika hospital ya Ndolage Muleba, alipokuwa akipatiwa matibabu,

Bw. Rweyemamu aliwahi kuwa mtumishi wa serikali katika Idara ya Habari Maelezo, na baada ya kustaafu alishirikiana na waandishi wenzao mwaka 1998 wakianzisha chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Kagera.

KPC,waandishi wa Habari wote mkoa wa Kagera wamepokea kwa masikitiko taarifa za kifo hicho na inaomba ndugu,jamaa ,familia yake kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu.

Mungu alitoa, Mungu ametwaa jina lake liabudiwe, AMINA.



Imetolewa na
M. Byabato
Katibu Mtendaji
Kagera Press Club

No comments:

Post a Comment